Ijumaa, 27 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir:

Kitengo cha Wanawake “Kampeni ya Kimataifa - Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Mgogoro wa kikatili nchini Sudan kati ya Vikosi vya Wanajeshi wa Sudan vinavyoongozwa na Jenerali Abdel Fattah al-Burhan, mtawala mkuu wa Sudan, na Vikosi vya kijeshi vya Msaada wa Haraka vinavyoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti), naibu wa zamani wa Burhan katika Baraza la Utawala, sasa umeingia mwaka wa tatu. Baadhi ya makadirio yanaweka idadi ya waliouawa kuwa 150,000, na ukatili wa kutisha uliofanywa na pande zote mbili, ikiwa ni pamoja na mauaji ya kinyama, mateso, na ubakaji mkubwa. Mauaji ya kikabila na kikatili pia yameripotiwa katika miji mbalimbali, vijiji na kambi za watu waliohama. Vita hivyo vimesababisha mzozo mkubwa zaidi wa kibinadamu, mzozo mkubwa zaidi wa wakimbizi, na janga kubwa zaidi la njaa ulimwenguni, huku nusu ya watu milioni 50 wakikabiliwa na njaa. Hata hivyo, mzozo huu umeelezewa kuwa "vita vilivyosahaulika" na "mgogoro uliofichwa na usioonekana" kwa sababu haujapata usikivu wa kimataifa na utangazaji wa vyombo vya habari vya kimataifa unaostahili. Kwa hiyo, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Kimezindua kampeni ya kimataifa kuangazia maafa yanayozidi kuwa mabaya ya kibinadamu yanayowakabili Waislamu wa Sudan. Kampeni hii pia itashughulikia: siasa na ajenda zilizofichwa nyuma ya mzozo huu, dola za kikanda na kimataifa zinazofadhili vita na sababu zake, historia ya Sudan na mambo yaliyosababisha migogoro ya hivi karibuni na kufeli kiuchumi, kwa nini mfumo wa kidemokrasia umefeli kutatua matatizo mengi ya kisiasa, kiuchumi, kikabila na kijamii ya Sudan, na jinsi uongozi wa Kiislamu wa Dola ya Khilafah Rashida, unaweza kujenga mustakabali mzuri wa Sudan na nchi nyingine za Kiislamu zenye mafanikio.

﴿يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ اسْتَجِيبُواْ لِلّهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُم لِمَا يُحْيِيكُمْ﴾

“Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele.” [Surah Al-Anfal: 24]

Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Jumatatu, 10 Safar Al-Khair 1447 H sawia na 04 Agosti 2025 M

- Fuatilia Kampeni kwa Lugha Nyenginezo -

Ar En
FR Tr
Gr Ur
Pe

Kusoma Taarifa kwa Vyombo vya Habari ya Kitengo cha Wanawake

ambayo ilitangaza uzinduzi wa kampeni yake ya kimataifa yenye kichwa:

“Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu”

Jumatatu, 10 Safar Al-Khair 1447 H sawia na 04 Agosti 2025 M

Bonyeza Hapa

 

Video ya Ualishi wa Uzinduzi wa Kampeni ya Kimataifa

“Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti, na Udanganyifu”

Uislamu Uliingiaje Sudan?

Video hii inaelezea uhusiano wa kwanza kati ya Uislamu na Sudan, na jinsi Uislamu ulivyoenea nchini kote kupitia uhamiaji wa Waarabu, biashara na uenezaji wa amani. Ni sehemu ya kampeni ya kimataifa iliyozinduliwa na Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir yenye kichwa, “Vita vya Sudan: Hadithi ya Ukoloni, Usaliti na Udanganyifu” ambayo inalenga kuleta mwanga juu ya janga la kibinadamu linalozidi kuwasibu Waislamu wa Sudan kama matokeo ya mzozo wa sasa unaoikumba nchi hii ambao umepewa lakabu ya “Vita Vilivyosahauliwa”.

Hali kutokana na Mzozo nchini Sudan!

Dada Umm Ali kutoka Sudan anaelezea hali mbaya wanayopitia kutokana na mzozo wa kisilaha unaoendelea huko kati ya Jeshi la Sudan, linaloongozwa na Abdel Fattah al-Burhan, na Vikosi vya Msaada wa Haraka, vinavyoongozwa na Mohamed Hamdan Dagalo (Hemedti).

Sudan chini ya Dola ya Kiislamu!

Dada Maryam anazungumzia jinsi Sudan itakavyokuwa chini ya Dola ya Kiislamu (Khilafah Rashida kwa njia ya Utume) ambayo tunafanya kazi ili kuisimamisha. Sudan itaunganishwa ndani chungu kimoja chini ya bendera moja inayotawaliwa na Uislamu, ambayo itaregesha ustawi na izza na kuirudisha nchi hii kuwa kapu la chakula duniani.

 

Kipeperushi cha Kampeni

Kupakua Nakala ya PDF Bonyeza Hapa 

 post 5 ENG  post 6 ENG
post 7 ENG  post 8 ENG

MATOLEO

Hizb ut Tahrir

Wilayah Sudan

Amerika inaharakisha Mpango wake wa Kulitenganisha Eneo la Darfur
Hakuna Suluhisho Isipokuwa kwa Kuufanya Umoja wa Dola kuwa Suala Nyeti

18 Safar 1447 H - 12 Agosti 2025 M

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Sudan Wilayah – Mji wa Kosti, Jimbo la White Nile Wakutana na Dkt. Muhammad al-Haitham, Katibu Mkuu wa chama cha National Unionist Party katika Jimbo la White Nile

21 Rabi' I 1447 H - 13 Septemba 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayat Sudan kukwamisha mpango wa kutenganisha Darfur, Hizb ilifanya Visimamo katika miji kadhaa ya Sudan

21 Rabi' I 1447 H - 13 Septemba 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan - mbele ya Msikiti Mkuu jijini Port Sudan
Wito kwa Watu wa Sudan... Msiiruhusu Amerika Kuichana Nchi Yenu na Kuivua Darfur

20 Rabi' I 1447 H - 12 Septemba 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan
Wakutana na Mkurugenzi wa Khalawi na Idara za Misikiti katika Mji wa Port Sudan

17 Rabi' I 1447 H - 09 Septemba 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan
Wakutana na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Wanazuoni katika Jimbo la White Nile

17 Rabi' I 1447 H - 09 Septemba 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Ndani ya Muundo wa Kampeni ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Kuvuruga Mpango wa Kutenganisha Darfur
Wanachama wa Hizb ut Tahrir katika Mji wa Al-Obeid Wahutubia Wito Mzito kwa Waislamu katika Msikiti Mkuu wa Al-Obeid na Kubeba Mabango katika Amali Nyengine katika Kituo cha Usafiri

15 Rabi' I 1447 H - 07 Septemba 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan
Wakutana na Mkuu wa Chama cha Adalah nchini Sudan

14 Rabi' I 1447 H - 06 Septemba 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Maslahi ya Nani Yanatumikiwa kwa Uamuzi wa Serikali wa Kufungua Tena Kivuko cha Mpakani cha Adre huku Watu wa Fashir Wakifa kwa Njaa?!

12 Rabi' I 1447 H - 04 Septemba 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Enyi Watu wa Sudan, Mnaweza Kutibua Mpango wa Kuitenga Darfur, Basi Inukeni Kumtii Mwenyezi Mungu!

10 Rabi' I 1447 H - 02 Septemba 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Mpango wa Amerika wa Kuitenganisha Darfur... Na Jinsi ya Kuutibua

10 Rabi' I 1447 H - 02 Septemba 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Watu wa Al-Fashir Baina ya Nyundo ya Vita na Kinoo cha Njaa, na Hawana Wokovu isipokuwa kwa Dola ya Khilafah

8 Rabi' I 1447 H - 31 Agosti 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Taqli Watoa Wito Mkali kwa Waislamu Kutibua Mpango wa Marekani wa Kutenganisha Darfur

7 Rabi' I 1447 H - 30 Agosti 2025 M

Ripoti ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan 

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan
Wanamtembelea Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist mjini Al-Obeid

4 Rabi' I 1447 H - 27 Agosti 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan
Waitembelea Idara ya Muongozo na Ushauri katika Jimbo la White Nile

1 Rabi' I 1447 H - 24 Agosti 2024

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari mnamo Jumamosi, 22 Safar 1447 H sawia na 16/08/2025 M, yenye kichwa:
Wito kwa Watu wa Sudan... Ikamateni Darfur Ili Isiungane na Kusini

22 Safar 1447 H - 16 Agosti 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Mbwa Mwitu Hapaswi Kulaumiwa kwa Uvamizi wake ikiwa Mchungaji ndiye Adui wa Kondoo

13 Safar 1447 H - 7 Agosti 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Mahusiano ya Kigeni ni Jukumu la Dola Pekee, kwa kuwa Dola Pekee ndiyo iliyo na Haki ya Kuchunga Mambo ya Ummah Kivitendo

10 Safar 1447 H - 4 Agosti 2025 M

Taarifa kwa Vyombo vya Habari katika Wilayah Sudan

Hotuba Iliyotolewa na Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan
Mbele ya Msikiti Mkongwe jijini Port Sudan mnamo Ijumaa tarehe 1/8/2025 M

7 Safar 1447 H - 1 Agosti 2025 M

MAKALA

Sudan: Giza la Muundo wa Makubaliano au Nuru ya Katiba Inayotokana na Kitabu cha Mwenyezi Mungu na Sunnah ya Mtume Wake?

Na: Bayan Jamal

25 Rabi' I 1447 H - 17 Septemba 2025 M

“Kujitawala Wenyewe” kwa Mujibu wa Matakwa ya Wakoloni!

Na: Rana Mustafa

18 Rabi' I 1447 H - 10 Septemba 2025 M

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Watangaza: Tibueni Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Gazeti la Al-Rayah - Toleo 564 - 10/09/2025 M

18 Rabi' I 1447 H - 10 Septemba 2025 M

Marekani inatia Mikono yake Michafu katika Kila Mzozo; Sudan sio Tofauti

Na: Sarah Mohammed – Amerika

16 Rabi' I 1447 H - 08 Septemba 2025 M

Hakuna Suluhisho kwa Suala la Sudan Isipokuwa Kutawalisha Uislamu

Na: Zeena As-Samit

8 Rabi' I 1447 H - 31 Agosti 2025 M

Mauaji ya Halaiki ya Sudan: Dori ya Omar al-Bashir

Na: Amatullah Hechmi

6 Rabi' I 1447 H - 29 Agosti 2025 M

Mpango wa Mipaka ya Damu na Uhalifu wa Kujitenga kwa Darfur

Na: Ustadh Muhammad Jami (Abu Ayman)

Msaidizi wa Msemaji wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan

4 Rabi' I 1447 H - 27 Agosti 2025 M

Fahali Wanapopigana, Zinazoumia ni Nyasi
“Sudan ni Mfano”

Na: Bayan Jamal

3 Rabi' I 1447 H - 26 Agosti 2025 M

Historia ya Ukoloni wa moja kwa moja na usio wa moja kwa moja wa Sudan
kati ya 1889-2019

Na: Tsuroyya Amal Yasna
Mwanachama wa Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

28 Safar 1447 H - 23 Agosti 2025 M

Umuhimu wa Kimkakati wa Siasa za Kijiografia za Sudan

Na: Sumaya Bint Khayyat

27 Safar 1447 H - 21 Agosti 2025 M

Umuhimu wa Kimkakati wa Eneo la Sudan

Na: Dkt. Fika Komara
Mwanachama wa Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

24 Safar 1447 H - 18 Agosti 2025 M

Uislamu Uliingiaje Sudan?

Na: Mhandisi Dorra Baccouche

20 Safar 1447 H - 14 Agosti 2025 M

Vita vya Sudan Vilivyosahauliwa: Janga kwa Ummah

Na: Yasmin Malik
Mwanachama wa Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

16 Safar 1447 H - 10 Agosti 2025 M

Sudan: Janga la Karne Lililofichika Machoni mwa Ulimwengu

Na: Muslimah Ash-Shami (Umm Suhaib)

13 Safar 1447 H - 07 Agosti 2025

- Alama Ishara za Kampeni -

#أزمة_السودان

#SudanCrisis

#SudanKrizi

#SoudanCrise

Fuatilia Kampeni ya Kimataifa katika Mitandao ya Kijamii

Facebook: QANITATHT1

https://www.facebook.com/QanitatHT1

X: @ALQANITAT

https://x.com/alqanitat

Instagram: @WOMEN_SHARIA

https://www.instagram.com/women_sharia?igsh=NTc4MTIwNjQ2YQ==

post 1 ENG post 2 ENG
post 3 ENG post 4 ENG

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu