Jumamosi, 23 Sha'aban 1446 | 2025/02/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Jibu la Swali: Kuongezeka kwa Uhasama nchini Sudan

Al Arabiya Net ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 4/2/2025: "Jeshi na vikosi vyake vya usaidizi viliingia katika maeneo ya kusini-mashariki ya Jimbo la Khartoum wakati wa saa zilizopita, wakitokea Jimbo la Al-Jazeera.." na tovuti ya Youm7 ilichapishwa mnamo tarehe 2/2/2025: "Mwandishi wa Kituo cha Habari cha Cairo aliripoti katika habari mpya zinazochipuka kwamba jeshi la Sudan linachukua idadi kadhaa ya vijiji mashariki mwa mto Nile katika Jimbo la Khartoum." Kabla ya hapo, mnamo tarehe 11/ 1/2025, Vikosi vya Msaada wa Haraka vilishindwa na jeshi la Sudan katika mhimili wa Jimbo la Al-Jazeera na mji mkuu wake, Wad Madani, “na kamanda wa Vikosi vya Msaada wa Haraka, Hemeti, alikiri katika kanda ya sauti iliyohusishwa naye kwamba vikosi vyake vilishindwa katika Jimbo la Al-Jazeera...” (Al-Jazeera 1/13/2025).

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Uhamishaji wa Watu wa Gaza

Al Jazeera ilichapisha kwenye tovuti yake mnamo tarehe 26/1/2025: “Rais wa Marekani Donald Trump alisema kwamba anaishinikiza Jordan, Misri na nchi nyingine za Kiarabu kupokea wakimbizi zaidi wa Kipalestina kutoka Gaza, baada ya vita vya Israel dhidi ya Ukanda huo kusababisha mgogoro wa kibinadamu. Alipoulizwa ikiwa hili lilikuwa pendekezo la muda au la muda mrefu, Trump alisema, “Inaweza kuwa hili au lile.”

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Mabadiliko Mapya ya Kisiasa nchini Lebanon

Ni yapi yanayojiri nchini Lebanon kuhusu wepesi wa makubaliano juu ya uteuzi wa Kamanda wa Jeshi Joseph Aoun kama rais mnamo 9 Januari 2025 baada ya nafasi hiyo kudumu kuwepo kwa zaidi ya miaka miwili, kisha siku chache baadaye makubaliano kwa Salam Nawaf kuwa kama waziri mkuu mnamo 13 Januari 2025? Haya yote yalitokeaje haraka hivyo? Je, kasi hii ina maana kwamba kazi ilikuwa na bado ingali inatayarishwa kubadilisha uso wa Lebanon ndani na nje, au ni mabadiliko ya kawaida, kama inavyotokea katika kanda hiyo?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Biashara ya Mtandaoni (E-Commerce)

Je, biashara ya mtandaoni (e-commerce) na kampuni ya DXN ya Malaysia inaruhusiwa? Kampuni hii inategemea uuzaji wa virutubisho vya lishe, shampoo, krimu za ngozi...nk. Unapo  nununua kutoka kwake kiasi fulani, inatoa punguzo (discount). Pindi pointi zako zikifika 100 inakupa punguzo la asilimia sita. Kadiri unavyopata pointi zaidi, ndivyo inavyokupa punguzo kubwa zaidi, na pointi hizi hubadilishwa kuwa kiasi cha pesa ambacho huhamishiwa kwako ama kwa njia ya bahasha au barua ambayo hutolewa kwako kila mwezi, au kuhamishiwa kwenye salio (balance) lako la benki.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Matukio nchini Syria na Kuanguka kwa Utawala wa Assad

Asharq Al-Awsat ilichapishwa mnamo tarehe 8 Disemba 2024: (Utawala wa Assad umeanguka: Upinzani wa Syria umetangaza leo, Jumapili, kwamba umeikomboa Damascus na kuupindua utawala wa miaka 24 wa Rais Bashar al-Assad. Taarifa ya upinzani kwenye televisheni ya taifa ilisomeka: “Sifa zote ni za Mwenyezi Mungu, mji wa Damascus umekombolewa na dhalimu Bashar al-Assad amepinduliwa.” Upinzani uliongeza kuwa wafungwa wote wameachiliwa huru.)

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Hukmu ya Miamala ya Kifedha na Kibiashara kupitia Mtandao wa Intaneti

Je, ni ipi hukmu ya biashara, kwa mfano, kununua dinari, mafuta, dhahabu nk kwa dolari wakati wa bei nafuu, kisha kuiuza kwa wakati wa bei ya juu ili kupata faida, huku ukijua kwamba yote haya yanapatikana kwenye mtandao, na anaweza kuhamisha pesa benki na kuzitoa wakati wowote anapotaka?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Mazungumzo ya Geneva na Jaribio la Kumaliza Vita nchini Sudan

Kikao cha ufunguzi wa mazungumzo ya Geneva ya kumaliza vita nchini Sudan ambayo yamekuwa yakiendelea kwa takriban miezi 16 kilifanyika mnamo Jumatano (14/8/2024) mbele ya washirika wa upatanishi wa kimataifa, Marekani, Uswizi, Saudi Arabia. Misri, Imarati, Muungano wa Afrika na Umoja wa Mataifa, huku jeshi la Sudan halikuwepo kwenye mazungumzo hayo. Ni nini sababu ya wito wa Marekani kufanya kongamano jijini Geneva badala ya Jeddah na kupanua ushiriki?

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Je, Yajuzu Mtu Kumpa Zaka Dadake au Binti Yake?

Uislamu umewajibisha kushibisha mahitaji haya ya kimsingi na kuwapa wale wasioweza kuyapata. Ikiwa mtu binafsi anajipatia wenyewe, ni vizuri; ikiwa hawawezi kujiruzuku kwa sababu ya ukosefu wa pesa za kutosha au kutokuwa na uwezo wa kupata pesa za kutosha, Shariah inawajibisha wengine kuwasaidia hadi mahitaji haya ya kimsingi yatimizwe.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu