Ijumaa, 11 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Musibabaishwe na Mikutano, Fungueni Mipaka

Katika Mkutano wa Kilele wa Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) na Ligi ya Nchi za Kiarabu uliofanyika jijini Doha, mji mkuu wa Qatar, Rais Erdoğan alisema: “Tunafahamu kuwa Israel haitasimama katika muda mfupi isipokuwa itakabiliwa na hisia kali na vikwazo. Tunafahamu kwamba tunazo mbinu za kuzuia hili.” (Agencies 15.09.2025)

Soma zaidi...

Tamasha la OIC Lahitimisha kwamba Qatar na Dola za Kiarabu Zisalie Waaminifu kwa Kuwa Kiatu Kilicho Chakaa cha Amerika Huku Zikibweka Vikali Mawinguni

Kufuatia shambulizi la kombora la umbile la Kizayuni dhidi ya wanachama wa Hamas nchini Qatar, taarifa ya mwisho ya mkutano wa dharura wa kilele wa Waarabu-Waislamu (OIC na Ligi ya Waarabu) uliofanyika jijini Doha mnamo 15 Septemba 2025, “unashutumu vikali uvamizi wa Israel dhidi ya Qatar, na kuutaja kuwa ni kama pigo kwa matarajio yoyote ya amani katika eneo hilo. Tangazo hilo zilizisihi nchi wanachama kuzingatia upya mafungamano yao ya kidiplomasia na kiuchumi na Israel na kufuata hatua za kisheria dhidi yake.”

Soma zaidi...

Ametokea kwa Mlango, Anaingia kwa Dirisha

Kwa mara nyengine tena, Amerika inafichua kiburi chake mbele ya ulimwengu. Onyo la Donald Trump kwamba “mambo mabaya yatatokea” isipokuwa Afghanistan ikabidhi Kambi ya Anga ya Bagram inaakisi sauti ile ile ya kibeberu ambayo kwa muda mrefu imekuwa ikifafanua sera ya Marekani kwa ardhi za Waislamu. Maneno kama haya sio lugha ya dola huru zinazoamiliana kwa usawa, bali ni maagizo ya mkoloni ambaye anaziona ardhi za Waislamu kama kituo cha kijeshi kwa ajili ya matamanio yake. Hii ndiyo hali halisi ya siasa za Magharibi: ushurutishaji, vitisho, na kudharau ubwana wa nchi zetu.

Soma zaidi...

Si Mtazamaji: Dori ya Marekani katika Shambulizi la ‘Israel’ dhidi ya Doha

Mnamo Septemba 2025, “Israel” ilishambulia Doha, na kuua viongozi wa Hamas na mlinzi wa Qatar. Gazeti la ‘The Independent’ liliripoti kuwa Trump alikasirika kwa sababu Netanyahu alimfahamisha katika dakika za mwisho tu – “He's f***ing me” – huku vyanzo vya “Israel” badala yake vilizungumza kuhusu “idhini” ya Trump.

Soma zaidi...

Ummah Unahitaji Khilafah Kulinda Matukufu Yake Sio Mikataba ya Ulinzi ya Kuwalinda Watawala Vibaraka

Pakistan na Saudi Arabia zimeingia katika makubaliano ya kihistoria ya ulinzi wa pande zote, ambapo uvamizi wowote dhidi ya dola moja utachukuliwa kuwa shambulizi kwa pande zote mbili. ‘Mkataba wa Kimkakati wa Ulinzi wa Pamoja’ ulitiwa saini na Waziri Mkuu wa Pakistan Shehbaz Sharif na Mfalme Mtarajiwa wa Saudia Mohammad Bin Salman katika Kasri la Al-Yamamah jijini Riyadh mnamo Jumatano, 17 Septemba 2025.

Soma zaidi...

Mradi wa Reli wa China–Indonesia: Mkakati wa China Kuidhibiti Indonesia

Indonesia inafikiria kujadili upya deni la mradi wa reli ya mwendo kasi wa Jakarta–Bandung, unaojulikana kama Whoosh, kutokana na mzigo mzito wa kifedha unaouweka kwa mwendeshaji wa reli ya serikali Kereta Api Indonesia (KAI). Waziri wa Biashara Zinazomilikiwa na Serikali Erick Thohir alisema mpango huo utaruhusu KAI kusimamia treni huku serikali ikisimamia miundombinu. Mradi huo wenye thamani ya dolari bilioni 7.3 ulifadhiliwa hasa kupitia mikopo kutoka Benki ya Maendeleo ya China, awali kwa riba ya asilimia 2. Hata hivyo, kukatizwa na maambukizi na masuala ya ardhi yalisukuma gharama zaidi, na kuhitaji ufadhili wa ziada kwa riba ya asilimia 3.4.

Soma zaidi...

Uchaguzi wa Kidemokrasia si Lolote ila Minong'ono ya Ibilisi

Mnamo 13 Septemba 2025 kinyang’anyiro cha kuwania urais wa Zanzibar kilianza rasmi huku chama tawala – Chama Cha Mapinduzi (CCM) na chama cha upinzani cha ACT-Wazalendo kikizindua kampeni zao. CCM ilisisitiza ‘utulivu’, ‘amani’ na ‘umoja’, huku chama cha ACT Wazalendo kikiweka kipaumbele katika uwajibikaji, usawa, na fursa za kiuchumi.

Soma zaidi...

Kukamatwa kwa Mamia ya Waandamanaji Wanaounga Mkono Palestina kwa Amani nchini Uingereza Yaonyesha Uhalisia wa Kinaya cha Demokrasia

Mnamo Jumamosi, tarehe 6 Septemba, karibu watu 900 walikamatwa katika maandamano ya kuunga mkono Palestina jijini London. Walikuwa wakipinga kuendelea kwa mauaji ya halaiki na njaa kwa raia wasio na hatia mjini Gaza, pamoja na kupigwa marufuku kwa kundi la Palestine Action ambalo serikali ya Uingereza iliharamisha kuwa shirika la kigaidi mwezi Julai. Waliokamatwa ni pamoja na maaskofu, makasisi, walimu, madaktari, wahudumu wengine wa afya, na vizazi vya wahanga wa mauaji ya Holocaust pamoja na waandamanaji walemavu. Wengi walikuwa wazee – katika miaka yao ya 60, 70 na hata 80 – na walijumuisha mzee mmoja kipofu mwenye umri wa miaka 62 aliye katika kiti cha magurudumu.

Soma zaidi...

Matarajio Yasio na Msingi: Nchini Uzbekistan, Mhubiri Aliyetoka Nchini Uturuki Ashtakiwa

Mahakama ya Jinai ya Wilaya ya Uchtepa ya Tashkent ilianza kusikiliza mnamo Agosti 19 kesi ya jinai dhidi ya mtu wa dini Alisher Tursunov, anayejulikana kwa umma kwa jina bandia la Mubashshir Ahmad. Habari hiyo iliripotiwa na Aziz Abidov, mkuu wa huduma ya vyombo vya habari wa Mahakama ya Upeo ya Uzbekistan. Kulingana na tuhuma ya mashtaka, Tursunov anashtakiwa chini ya vifungu vitatu vya Kanuni ya Jinai ya Uzbekistan.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu