“Maslahi Makuu ya Serikali” Yanakula Watoto Wake Yenyewe!
- Imepeperushwa katika Ujerumani
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Chansela wa Ujerumani yuko chini ya shinikizo kutoka kwa kanuni ile ile ya kisiasa ambayo hivi majuzi aliitangaza kuwa “kiini cha uwepo wa Wajerumani.” Licha ya matamshi yake ya mara kwa mara ya kujitolea kikamilifu kwa kanuni ya maslahi makuu ya dola (ambayo ina maana ya uungaji mkono kamili kwa umbile la Kiyahudi), majeshi ya Kizayuni katika siasa na vyombo vya habari yanahamasisha juhudi za kuhujumu uamuzi wake wa hivi karibuni wa kuzuia usafirishaji nje wa silaha kwa umbile hilo kupitia mashambulizi yaliyoratibiwa!