Mkutano wa Cairo Unathibitisha Usaliti wa Watawala wa Kiarabu kwa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina
- Imepeperushwa katika Misri
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mkutano huo wa dharura wa Waarabu ulifanyika jijini Cairo katikati ya mazingira machungu ambayo Umma wa Kiislamu unapitia, hasa hujuma za Kiyahudi mjini Gaza, na shinikizo la kimataifa linaloongezeka kuhusu kadhia ya Palestina. Kama ilivyotarajiwa, mkutano huo ulitoa taarifa ya mwisho ambayo ilikuwa na maneno ya kulaani na kukashifu, na kutaka masuluhisho ya viraka ambayo hayashughulikii mizizi ya mgogoro huo. Je, tunautazamaje mkutano huu? Na ni upi msimamo juu ya matokeo yake?