Trump asingeweza Kututawala kama Tungekuwa na Khalifa, na Umbile la Kiyahudi Lisingekuwepo bila Usaliti wa Watawala wetu
- Imepeperushwa katika Jordan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Viongozi wa ukafiri nchini Amerika na Ulaya, pamoja na chombo chao, umbile la Kiyahudi, wanajua kwamba misimamo ya watawala wa Waislamu, duara zao za kisiasa, na wapambe wao—wanaowatukuza—hawawakilishi wengi wa Waislamu, wala hawaakisi matumaini yaliyo ndani ya nyoyo zao kwa ajili ya kuregeshwa kwa mamlaka yao. Ukitaka kuelewa msimamo wao wa kweli na jibu lao kwa maamrisho ya Mwenyezi Mungu mbele ya chuki kwenu na kuwaua duniani kote, na kusubutu kwenu kutishia kukalia ardhi zao zaidi na kupora mali zao, musiangalie zaidi ya kiburi cha kiongozi wenu Trump. Kwa kutokuwa na haya mbele ya ulimwengu, ameonyesha kiburi cha Amerika kafiri na msaada wake kwa wale walioshukiwa na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu.