Jumamosi, 23 Sha'aban 1446 | 2025/02/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Trump asingeweza Kututawala kama Tungekuwa na Khalifa, na Umbile la Kiyahudi Lisingekuwepo bila Usaliti wa Watawala wetu

Viongozi wa ukafiri nchini Amerika na Ulaya, pamoja na chombo chao, umbile la Kiyahudi, wanajua kwamba misimamo ya watawala wa Waislamu, duara zao za kisiasa, na wapambe wao—wanaowatukuza—hawawakilishi wengi wa Waislamu, wala hawaakisi matumaini yaliyo ndani ya nyoyo zao kwa ajili ya kuregeshwa kwa mamlaka yao. Ukitaka kuelewa msimamo wao wa kweli na jibu lao kwa maamrisho ya Mwenyezi Mungu mbele ya chuki kwenu na kuwaua duniani kote, na kusubutu kwenu kutishia kukalia ardhi zao zaidi na kupora mali zao, musiangalie zaidi ya kiburi cha kiongozi wenu Trump. Kwa kutokuwa na haya mbele ya ulimwengu, ameonyesha kiburi cha Amerika kafiri na msaada wake kwa wale walioshukiwa na ghadhabu ya Mwenyezi Mungu.

Soma zaidi...

Hatari ya Uhamisho Inayotafutwa na Trump na Umbile la Kiyahudi Inalazimu Hatua Kali katika Kuamiliana nao kama Maadui

Utawala wa Jordan na kundi la watu wake wakati wote wa vita vya Kiyahudi dhidi ya Gaza walikuwa na bado wangali wanatetea kutowanusuru watu wa Gaza kijeshi, na angalau sio kufutilia mbali makubaliano ya udhalilishaji na aibu na umbile la Kiyahudi, lakini kwa busara na hekima na ujanja wa kisiasa hii ni hatua na udhoofishaji wa amani, usalama na chemchemi ya utulivu ambayo Jordan inaishi ndani yake. Mfalme alifikiri kwamba Uingereza ilimuamuru kurukuu na kujibu ajenda ya Amerika ambayo imelitawala eneo hilo tangu aingie madarakani, kufuatia mbinu ya baba yake, na kile ilichomuagiza kuhitimisha makubaliano ya pamoja ya ulinzi nayo mwaka 2021 ambayo yanahujumu kila maana ya ubwana wa nchi yoyote, na kuifungua nchi kwa ujumla kwa kambi za Amerika pekee na viwanda na vikosi vyake.

Soma zaidi...

Kuondolewa kwa Umbile la Kiyahudi ndio Suluhisho Pekee, Sio Suluhisho la Dola Mbili, Safadi

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jordan Ayman Safadi, wakati wa kushiriki kwake katika Kongamano la Kiuchumi la Dunia huko Davos mnamo Jumatano, 22/01/2025, alisema kuwa mbinu yoyote ya baadaye ya Gaza lazima iegemee juu ya umoja wa Ukanda wa Gaza na Ukingo wa Magharibi na lengo la kufikia amani tu kwa msingi wa suluhisho la dola mbili. Alisema: “Katika muktadha wa suluhisho la kisiasa, serikali ya Palestina ndiyo pekee inayoshikilia uamuzi wa amani na vita, na hakupaswi kuwe na makundi ya kisilaha nje yake.”

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi Hajj Mustafa Abdullah Al-Issa Al-Jaber Al-Aboushi (Abu Anas)

Kwa imani katika qadhaa ya Mwenyezi Mungu (swt) na kutaka malipo Yake, Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Jordan inamuomboleza Mbebaji Da’wah katika safu zake: Hajj Mustafa Abdullah Al-Issa Al-Jaber Al-Aboushi (Abu Anas) Aliyefariki kwenda kwenye rehema za Mwenyezi Mungu Mtukufu asubuhi ya leo, Jumanne, 3/12/2024, akiwa na umri wa miaka 80.

Soma zaidi...

Operesheni ya Kishujaa ya Wanajihadi Hossam na Amer Dhidi ya Wanajeshi wa Kiyahudi Inakanusha Udhuru Wowote kwa Jeshi Kushindwa Kuchukua Hatua dhidi ya Umbile lao

Vitendo hivi vya kishujaa vya kibinafsi, kukabiliana na adui muoga kwa kuvuka mipaka, na kuuawa kishahidi katika njia ya Mwenyezi Mungu ili kuyakomboa maeneo matakatifu, Msikiti wa Al-Aqsa, na Palestina yote kutoka kwa Mayahudi na Amerika, ambayo inaendelea kuwapa silaha, vifaa, na ujasusi huku likieneza ufisadi, vinapaswa kuchochea ndani yenu hisia ya heshima na uanaume. Nyinyi watu wenye nguvu mnaoitwa “ndugu wenye silaha” mnapaswa muinuke kumtetea Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na Waislamu, na sio watawala wenu wanaowapeleka kwenye maangamivu na kuwatumikisha kwa maadui zenu.

Soma zaidi...

Mwaka Umepita, na Mauaji ya Kikatili ya Halaiki mjini Gaza Yanazidi na Kuenea. Je, Sio Wakati sasa kwa Ummah Kuwaondoa Watawala wake Waoga Ambao Wameshindwa Kuinusuru?!

Umbile hili ovu sio tu ni kadhia ya kiusalama, kijeshi, au ya kisiasa. Inawezekana kulitokomeza na kuliondoa kwenye uso wa ardhi milele, kwa nguvu ya jeshi la Jordan pekee. Hii si ndoto au nadharia; wale wanaotilia shaka wanahitaji tu kuitazama Gaza, fahari, ambayo kwayo ilisimama kidete dhidi ya Mayahudi, ambao sura yao ilichanwa chanwa mbele ya ulimwengu, ikidhihirisha umbile lao halisi.

Soma zaidi...

Mgogoro wa Nishati nchini Jordan na Suala la Ufisadi wa Kiuchumi wa Mradi wa Al-Attarat, Utiifu wa Kisiasa, na Kuongezeka kwa Deni

Ripoti ya habari ya Shirika la Habari la Jordan, Petra, ya tarehe 6 Agosti 2024, ilisema kwamba “Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi iliamua kwamba serikali wala Kampuni ya Kitaifa ya Umeme hazihitajiki kulipa sehemu yoyote ya gharama kwa Kampuni ya Umeme ya Al-Attarat.” Habari hizi za upotoshaji zinakusudiwa kuficha hasara inayotarajiwa ambayo serikali ya Jordan itaipata kutokana na ukweli wa hukumu hiyo, inayosema: “Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi inaamuru kwamba mkataba huo ni halali na hauhusishi ukosefu mkubwa wa haki.”

Soma zaidi...

Serikali nchini Jordan Inatumikia Malengo ya Kikoloni ya NATO: Jaribio Lililofanywa Upya la Kuitenga Jordan kutoka kwa Ummah Wake wa Kiislamu

Wizara ya Mambo ya Nje na Wageni ya Jordan ilitangaza kuanzishwa kwa Afisi ya Mahusiano ya NATO (North Atlantic Treaty Organization) katika Ufalme huo, ambayo itachangia kuimarisha uhusiano wa ushirikiano na muungano huo. Wizara hiyo ilitoa taarifa ya pamoja na NATO kuhusu uamuzi wa kufungua afisi hiyo jijini Amman.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu