Jumapili, 22 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/14
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ghasia za Indonesia: Mabadiliko Ambayo (Bado) Yamefungwa?

Msiba wa Affan Kurniawan, dereva wa teksi ya pikipiki wa mtandaoni wa Indonesia aliyeuawa baada ya kugongwa na gari la polisi aina ya barracuda mnamo 28 Agosti 2025, uliishia katika msururu wa maandamano katika miji mingi kote Indonesia. Makala haya hayakusudii kujibu maswali, bali kuibua maswali kwa yeyote anayedai kuwa mwanaharakati wa Kiislamu.

Soma zaidi...

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Watangaza: Tibueni Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan kutibua mpango wa kuichana Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kwa kuzingatia kwamba umoja wa Ummah ni suala nyeti, ambalo ni lazima hatua za uhai au kifo zichukuliwe, Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi’ al-Awwal 1447 H, sawia 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa, katika Msikiti wa Sheikh Yahya wa Kuhifadhi Qur'an. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa makundi yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, maulamaa, maafisa na wanajeshi, na wengineo, wakiwataka watimize wajibu wao wa Shariah wa kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Upenyaji wa Mayahudi wa Jeshi la Misri

Tangu serikali ya Misri itie saini Makubaliano ya Camp David mwaka 1979, jeshi la Misri limeingia katika njia ya utegemezi na upenywaji, likijitenga na kanuni yake ya awali ya kuulinda Ummah na kulinda mipaka yake dhidi ya maadui wake wa kweli, wa kwanza miongoni mwao ni Mayahudi walioinyakua Palestina. Hatua kwa hatua, taasisi hii imebadilika na kuwa chombo kilichozuiliwa, chini ya masharti ya adui, hata kushiriki katika kuilinda na kuiwezesha kupitia mikataba ya kijeshi, usalama, kiuchumi, na ushauri ambayo iliunda utaratibu kamili wa ushawishi wa Kiyahudi, ndani ya jeshi na dola.

Soma zaidi...

Tofauti Kubwa Kati ya Azimio la Istanbul na Fatwa Zilizotangulia!

Mwishoni mwa kongamano lao waliloliita “Gaza ni Jukumu la Kiislamu na la Kibinadamu” lililofanyika jijini Istanbul kwa siku sita la maulamaa, lililoandaliwa na Erdogan, walitoa tamko la mwisho. Walianza na aya za Qur’an kuhusu maandalizi na Jihad katika Njia ya Mwenyezi Mungu (swt), ili kwamba yeyote anayeisoma afikirie kwamba kitakachofuata kingekuwa ni programu ya kivitendo ya jinsi ya kujishughulisha mara moja na Jihad ambayo sio tu inaiondolea Gaza bali pia inaikomboa Palestina na al-Masjid al-Aqsa. Hata hivyo, uhalisia ulikuwa kinyume.

Soma zaidi...

Utegemezi wa Dola za Kikoloni za Kikafiri Humpora Mtu Utashi wa Kisiasa, Hupotosha Dira ya Mtu na Kupoteza Nguvu za Mtu

Kwa kuzingatia ukandamizaji unaoendelea Syria kwa matakwa ya Amerika na mfumo wa kimataifa, watu wanahisi wameporwa utashi wao, kukosa uwezo wa kufanya maamuzi yao wenyewe, na kuhofia mustakabali wao. Ili kuelewa ni nani anayeamua mambo nchini Syria na kwa nini tumepoteza uwezo wetu wa kufanya maamuzi, lazima tuhakiki mkondo wa mapinduzi ya Syria tangu mwanzo wake.

Soma zaidi...

Marekani inatia Mikono yake Michafu katika Kila Mzozo; Sudan sio Tofauti

Katika kipindi cha muongo mmoja uliopita, Amerika imejidhihirisha kama mpangaji mkuu nyuma ya baadhi ya mizozo ya kunyama na ya ghasia zaidi kote duniani. Kutoka Urusi na Ukraine hadi India na Pakistan hadi China na Taiwan hadi Syria, Iraq, Afghanistan, Yemen, Kenya, Mali, Cameroon, na hii ni mifano michache tu! Hata hivyo, hakuna kilichoifichua Marekani zaidi ya uungaji mkono wake usio na haya na ushiriki wake katika mauaji ya halaiki yanayotokea Gaza dhidi ya watu wa Palestina. Kabla ya uvamizi, kuzingirwa kabisa, na kuangamizwa kwa Gaza, watu wengi hawakujua jinsi serikali ya Marekani ilivyokuwa chafu na jinsi wanavyoweza kuwatembeza wachezaji kama poni kwenye bao la chess.

Soma zaidi...

Kuzaliwa kwa Uongofu: Nuru Inayoondoa Giza Lililopo

Sayari ya Dunia, na hasa Bara Arabu, lilikuwa likiishi katika giza kuu lililofanya maisha ya binadamu yafanane na kuzimu. Kulikuwa na giza katika nyanja za itikadi, siasa, uchumi, mahusiano ya kijamii, na nyanja zote za maisha. Vita viliwasaga watu bila sababu, wenye nguvu walikuwepo huku wanyonge wakipotea na kutokuwepo, dhulma ilitanda maeneo yote, na utumwa ulifikia viwango vyake vya chini kabisa na vya udhalilishaji kabisa.

Soma zaidi...

Usaliti wa Magharibi kwa Wale Wanaoitumikia Katika Vita Dhidi ya Uislamu

Mkakati na sera ya Wakoloni wa Magharibi kuelekea Umma wa Kiislamu imejikita katika kupiga vita Uislamu kama fahamu ya kihadhara na kimfumo. Ilifanya kazi kupitia njama kubwa na ovu za kuivunja Dola ya Kiislamu, kuikata vipande vipande, na kuzuia kuregea kwake madarakani na kuwaunganisha Waislamu. Ili kutekeleza sera na njama zake, Wakoloni wa Magharibi waliwaajiri baadhi ya wana wa Waislamu, wakiwalea kwa uangalifu katika fikra, siasa, utawala na vyombo vya habari. Kama vile orientalisti mmoja alivyosema, “Mti wa Uislamu lazima ukatwe kupitia mmoja wa watoto wake.”

Soma zaidi...

Mauaji ya Halaiki ya Sudan: Dori ya Omar al-Bashir

Ingawa mengi yanajulikana kuhusu mauaji ya halaiki yanayowakumba ndugu na dada zetu nchini Palestina, machache sana yanajulikana—au yanasambazwa—kuhusu wale walio nchini Sudan, ambao kwa muda wa miezi 18 iliyopita wamevumilia mauaji ya halaiki ya kimya kimya. Ukatili huo umeua zaidi ya watu 15,000, zaidi ya milioni 10 wamekimbia makazi yao, na kuacha nusu ya watu—watu milioni 25—wakikabili uhaba wa chakula na njaa.

Soma zaidi...

Ubwana Unaofifia: Mpango Mpya wa Mafuta wa Pakistan, Vita vya Kale na Sera ya AI

Mnamo Julai, Rais Trump wa Amerika alichapisha kwenye jukwaa lake la Ukweli wa Jamii. “Hivi punde tumemaliza mkataba na nchi ya Pakistan, ambapo Pakistan na Marekani zitafanya kazi pamoja katika kuendeleza hifadhi yao kubwa ya mafuta.” Mkataba wa mafuta ni sehemu ya mkataba mpana wa kibiashara kati ya nchi hizo mbili, ambapo Marekani imekubali kupunguza ushuru kwa bidhaa za Pakistan kutoka 29% hadi 19%, huku ikitishia kuweka ushuru wa adhabu kwa India, isipokuwa New Delhi imalize uagizaji mafuta ghafi kutoka Urusi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu