Jumapili, 24 Jumada al-thani 1447 | 2025/12/14
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mapambano Dhahiri ya Kikoloni huko Hadramawt juu ya Mafuta Na Kuegemea Upande Wowote Ni Hasara Katika Dunia Hii na Akhera

Mnamo Jumamosi, 29/11/2025, vikosi vya jeshi vya Kikosi cha Ulinzi cha Hadramawt chenye uhusiano na Amr bin Habrish Al-Ali viliingia katika vituo vya mafuta vya Petro Masila katika Bonde la Hadramawt, vikinyanyua kauli mbiu ya kulinda vituo vya mafuta, huku vikiwaondoa wale waliokuwa hapo vikosi vya kawaida vya jeshi vilivyokuwa na uhusiano na Baraza la Octet.

Soma zaidi...

Kukamatwa Kupya kwa Wanachama wa Hizb ut Tahrir nchini Yemen na Mahouthi Je, kauli mbiu “Kifo kwa Amerika” inawezaje kuishi sambamba na Kutetea Mpango wa Trump kuhusu Gaza?!

Mnamo Alhamisi, 27/11/2025, vikosi vya usalama vya Mahouthi vilimkamata Saddam Ali Qa’id al-Mukirdi, mwenye umri wa miaka 28, kutoka wilaya ya Ṣabr al-Mawadim katika Mkoa wa Taiz ulio chini ya udhibiti wa Mahouthi katikati mwa Yemen. Kukamatwa huku ni kwa pili, kufuatia kukamatwa kwa ndugu Osama na Mohammad Mas’ad Al-Wurafi katika Mkoa wa Ibb mnamo 21/11/2025, baada ya kugawanya toleo lenye kichwa: “Trump Awaongoza Wafuasi Wake Miongoni mwa Watawala katika Ardhi za Waislamu kwenye Mpango wa Fedheha na Aibu, Wanaosujudu Vichwa Vyao Nyuma Yake kwa Kuiweka Gaza ya Hashim Chini ya Udhamini na Ukoloni.”

Soma zaidi...

Mahouthi Wawakamata Mashababu wa Hizb ut Tahrir kwa Kufichua Mkataba wa Trump!

Mnamo Ijumaa, 21/11/2025, kundi la Mahouthi katika Jimbo la Ibb liliwakamata wanachama wawili wa Hizb ut Tahrir, ndugu: Osama Muhammad Mas’ad Al-Wurafi (umri wa miaka 19) na Ibrahim Muhammad Mas’ad Al-Wurafi (umri wa miaka 15) kufuatia usambazaji wao wa toleo lililotolewa na Hizb ut Tahrir lenye kichwa: “Trump Anawaongoza Wafuasi Wake miongoni mwa Watawala katika Ardhi za Waislamu Kwenye Mkataba wa Fedheha na Aibu, Wakiinamisha Vichwa Vyao Nyuma Yake kwa Kuiweka Gaza Hashem chini ya Usimamizi na Ukoloni!” Toleo hili lilisambazwa nchini Yemen na nchi nyingi za Waislamu.

Soma zaidi...

Uingereza, kupitia Wafuasi wake na Mabwege wake, Imarati na Serikali ya Al-Alimi, Yamezea Mate Aden na Bahari Nyekundu, Lakini Je, Kuna Mtu Yeyote Aliye Tayari Kuifukuza?

Vyombo vya habari ndani na nje ya Yemen vilisambaza, mnamo Jumanne, 18/11/2025, habari za kuwasili kwa Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza anayeshughulikia Masuala ya Mashariki ya Kati na Afrika Kaskazini, Hamish Falconer, mjini Aden; ambapo alikutana na Rashad Al-Alimi, Mwenyekiti wa Baraza la Rais lenye wanachama wanane, na waziri huyo wa Uingereza pia alikutana na Waziri Mkuu Salem bin Buraik na Waziri wa Mambo ya Nje Dkt. Shaya Zindani, na mawaziri kadhaa, na Mwewe huyo aliandamana na Balozi wa Uingereza mjini Aden, Abda Sharif.

Soma zaidi...

Kwa Kuongezeka kwa Ajali za Barabarani, Pindi Uchungaji unapokuwa Haupo na Kubadilishwa na Kulaumu na Kurushiana Lawama!

Mnamo Jumatano, 5 Novemba 2025, ajali mbaya ya barabarani ilitokea katika Barabara ya Al-Arqoub katika wilaya ya Shuqra, jimbo la Abyan, kusini mwa Yemen, ambayo ilisababisha kuchomeka kwa basi la usafiri wa umma lililokuwa njiani kuelekea Aden, likitoka mji wa Jeddah, mali ya Kampuni ya Saqr Al-Hijaz, na lililokuwa limebeba abiria 42.

Soma zaidi...

Mfuko wa Fedha wa Kimataifa wafikia Kukaba Uchumi wa Yemen ili Kukamata Rasilimali Zetu za Kiuchumi

Mnamo tarehe 15/10/2025, Gavana wa Benki Kuu ya Aden, Ahmed Al-Maabqi, alikutana jijini Washington D.C., na mkuu wa ujumbe wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) nchini Yemen, Esther Pérez Ruiz, na mwakilishi wa IMF, Mohamed Maait, akiandamana na Naibu Waziri wa Fedha Hani Wahab na Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Waziri Msaidizi wa Fedha Abdul Qader Amin. Hii ilifuatiwa na mkutano kati ya Waziri wa Mipango na Ushirikiano wa Kimataifa na Gavana wa Yemen kwa Benki ya Dunia, Waed Badhib, na Riccardo Puliti, Makamu wa Rais wa Shirika la Fedha la Kimataifa wa Kanda ya Mashariki ya Kati, pamoja na ushiriki wa Naibu Waziri wa Mipango Nizar Basuhaib, Naibu Waziri wa Fedha Hani Wahab, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha Abdul Qader Amin, kwa uwepo wa Stefan G. G. Reimbert, Mkurugenzi wa Kanda wa Benki ya Dunia katika Mashariki ya Kati, na Dina Abu Ghaida, Meneja wa Benki ya Dunia nchini Yemen.

Soma zaidi...

Msimamo kwa Sherehe za Maadhimisho ya Mapinduzi Mawili ya Septemba Moja yaliingiza Usekula nchini Yemen na Mengine Yalitoa Wito wa Kuuimarisha!

Katika mwezi wa Septemba wa kila mwaka Yemen ina matukio mawili; la kwanza mnamo tarehe 26 Septemba 1962 ambayo ni kumbukumbu ya kupinduliwa kwa mfumo wa kifalme nchini Yemen Kaskazini, na la pili mnamo tarehe 21 Septemba 2014 ambayo ni kumbukumbu ya kuingia kwa Mahouthi jijini Sana’a ambayo ilisababisha udhibiti wao wa mikoa ya kaskazini.

Soma zaidi...

Chama cha Jumuiya ya Mageuzi ya Yemen (Islah), Sura ya Kiislamu ya Serikali Inayodai kuwa ni ya Kiislamu, Lakini iko Mbali Nao!

Mohammad Abdullah Al-Yadoumi, Mwenyekiti wa Baraza Kuu la chama cha Jumuiya ya Mageuzi ya Yemen (Islah), alitoa hotuba Ijumaa jioni, 12/9/2025, kuadhimisha miaka 35 tangu kuanzishwa kwa chama hicho, ambayo ilikuwa Septemba 13. Hotuba hiyo, iliyopeperushwa na Suhail TV na kudumu kwa zaidi ya dakika  arubaini, ilijumuisha msimamo wa chama hicho juu ya masuala ya ndani na ya kimataifa.

Soma zaidi...

Chuki na Uhalifu wa umbile la Kiyahudi mjini Gaza na Yemen Haitakomeshwa isipokuwa kwa Khilafah Rashida ya Pili kwa Njia ya Utume, Mlinzi wa Matukufu ya Waislamu

Kulengwa kwa Yemen na umbile la Kiyahudi kusingetokea isipokuwa kwa kukosekana utawala wa Uislamu, na kutabanniwa kwa sheria ya kimataifa inayowakilishwa na Umoja wa Mataifa na wale walio nyuma yake kama kibla chao, na malipo kama hayo ya kuacha kutawala na Uislamu ni matokeo ya kutarajiwa tu – hadi wanasiasa wa Yemen waregee kwenye fahamu zao na kuuweka Uislamu katika utabikishaji ndani ya Khalifah ya pili kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Wakati Mahouthi Wakishangilia Uhamasishaji wa Makabila ya Bakil na Hashid na Kupigwa kwa Ngoma za Vita Baina Yao!

Mnamo Jumamosi, 26/07/2025, Sheikh Hamid Mansour Radman aliuawa katika eneo la Al-Hayit, Wilaya ya Ayal Surayh, katika Mkoa wa Amran, na mkwe wake, Hamir Saleh Rattas Falyatah (Abu Udhr) mkuu wa idara ya polisi ya Al-Hayit. Mauaji ya Sheikh Radman yalikuja baada ya kuondoka nyumbani kwake, kufuatia mzozo wa kifamilia. Muuaji anashikilia wadhifa wa mkuu wa idara ya polisi, ambaye wajibu wake ni kulinda maisha, mali, na heshima, na kuhakikisha faraja na usalama wa jamii, kuondoa shida zake, kudumisha amani kote, na kuwazuia wakjukaji na wavamizi dhidi ya maisha ya watu – sio kumuua bamkwe wake kwa kukusudia kwa kumpiga risasi kwenye barabara ya umma!

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu