Jumamosi, 23 Sha'aban 1446 | 2025/02/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Umbile la Kigaidi la Kizayuni Limeufanya Ukingo wa Magharibi kuwa Makaburi ya Watoto kama vile Gaza, Huku Majeshi ya Nchi za Waislamu Yakitazama

Mnamo tarehe 7 Februari, shirika la ‘Save the Children’ liliripoti kwamba watoto wasiopungua 224 wameuawa katika Ukingo wa Magharibi na wanajeshi au walowezi wa Kizayuni tangu Januari 2023, mdogo zaidi akiwa na umri wa miaka 2 pekee. Kulingana na Umoja wa Mataifa, watoto 171 waliuawa katika Ukingo wa Magharibi tangu tarehe 7 Oktoba 2023 - sawia na karibu 1 kila siku. Hakuna mwanajeshi wa Kizayuni aliyefunguliwa mashtaka au kuwajibika kwa mauaji haya. Afisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu ilisema kuwa kumekuwa na ongezeko la mara 20 la idadi ya watoto wa Kipalestina waliouawa na mashambulizi ya anga ya umbile la Kiyahudi katika Ukingo wa Magharibi katika miaka ya hivi karibuni.

Soma zaidi...

Kutangaza Jamhuri nchini Syria ni Usaliti wa Mapinduzi ya Kiislamu!

Ahmed al-Shara, ambaye alifanya ziara yake ya kwanza ya kigeni nchini Saudi Arabia baada ya kuchukua kiti cha Urais nchini Syria, alitoa taarifa muhimu kuhusu mustakabali wa Syria sambamba na ramani ya utendakazi ya kisiasa ambayo amedumisha katika mahojiano na televisheni ya Syria. Akiahidi kukuuza uchumi wa soko huru na vifaa vya uwekezaji, Shara alisema, "Syria ni nchi ambayo itahifadhi hali yake ya asili, muundo wa serikali utakuwa wa jamhuri, kutakuwa na bunge, tawi la utendaji na mamlaka zinazofanya kazi kwa ushirikiano kati yao." alitumia maneno yake. (Mawakala)

Soma zaidi...

Mauaji Baada ya Mauaji Yanaendelea Gaza Huku Marekani Ikiendelea Kuwezesha Mauaji ya Halaiki na Dunia Imetulia Tuli

Mnamo tarehe 5 Januari, iliripotiwa kwamba umbile la mauaji la Kizayuni lililishambulia kwa mabomu Ukanda wa Gaza zaidi ya mara 100 katika muda wa siku 3 tu, na kuua zaidi ya watu 200 - wengi wanawake na watoto. Shabaha hizo zilijumuisha majengo ya makaazi, vikundi vya watu waliokusanyika barabarani na sokoni, na wale walio ndani ya makaazi yao. Pia iliripotiwa kuwa mtoto wa 8 aliganda hadi kufa katika Ukanda huo kutokana na baridi kali inayovumiliwa na wale wanaoishi katika mahema ya muda ambayo hayatoi ulinzi dhidi ya hali ya hewa ya baridi kali, na pia kutokana na kikwazo katili cha Wazayuni ambacho kinazuia mahitaji muhimu kama vile chakula, mafuta na nguo za majira ya baridi na blanketi kutokana na kuingia Gaza.

Soma zaidi...

Mgawanyiko wa Umma wa Kiislamu na Athari zake za Sumu

Kuongezeka kwa kasi kwa uhasama kati ya Pakistan na Afghanistan katika wiki iliyopita kumesababisha kifo cha mwanajeshi mmoja wa vikosi vya usalama vya Pakistan na makumi ya raia nchini Afghanistan. Raundi hii ya hivi punde ya mapigano ya kuvuka mpaka inatokana na kile Pakistan ilisisitiza kuwa ni jibu lake kwa mashambulizi ya mara kwa mara ya kundi lenye silaha la Tehreek-e-Taliban Pakistan (TTP), ambalo Islamabad ilisema limepata kimbilio katika mpaka wa Afghanistan. Shambulizi la hivi punde zaidi la TTP, mnamo Disemba 21, lilisababisha vifo vya wanajeshi 16 wa Pakistan.

Soma zaidi...

Kutekwa Nyara na Kupotezwa kwa Lazima: Ishara ya Mfumo Uliofeli

Kenya inashuhudia wimbi kubwa la utekaji nyara na mauaji yanayolenga watu mbalimbali. Tume ya Kitaifa ya Haki za Kibinadamu ya Kenya (KNCHR) inaelezea wasiwasi wake juu ya ongezeko la kutisha la utekaji nyara, kupotezwa kwa lazima na mauaji ya kiholela kote nchini. Mwenendo huu ni wa kuchukiza. Baadhi ya makundi ya vijana waandamanaji waliandamana katikati mwa jiji la Nairobi mnamo siku ya Jumatatu, tarehe 30 Disemba, huku makundi madogo ya watu wengine wakipanga kuketi vikao vya kulaani huku mawingu ya vitoa machozi yakitanda hewani. Waliimba kauli mbiu dhidi ya serikali, huku wengine wakiwa na mabango ya kulaani kuwekwa kizuizini kinyume cha sheria huku polisi waliokuwa wamepanda farasi wakishika doria karibu na hapo.

Soma zaidi...

Unyonyaji Mbaya wa Bima ya Afya na Takaful

Tangazo la hivi majuzi la Chama cha Bima ya Uhai ya Malaysia (LIAM), Shirika la Takaful la Malaysia (MTA), na Jumuiya ya Bima Jumla ya Malaysia (PIAM) la kuongeza bima ya afya na malipo ya takaful kwa kiwango kikubwa mno cha 40% hadi 70% ni jambo la kushangaza. Dhihirisho la ulafi wa kirasilimali. Ingawa mashirika haya yanahusisha kupanda kwa gharama za matibabu na kuongezeka kwa mahitaji ya huduma ya afya, nia halisi ni dhahiri: kuongeza faida kwa gharama ya umma.

Soma zaidi...

Kizungumkuti cha Syria: Kati ya Ukosefu wa Utambuzi na Tumaini la Kweli

Baada ya miaka 14 ya vita na ukandamizaji, Syria inaonekana iko tayari kwa mabadiliko huku utawala wa Bashar al-Assad ukianguka na vikosi vya upinzani, vinavyoongozwa na Abu Mohammad al-Julani, vikichukua Damascus. Hata hivyo, matumaini ya mustakabali mzuri zaidi yanavurugwa na ushawishi mkubwa wa dola za nje kama vile Marekani na Uturuki, ambao zinaongoza njia ya Syria chini ya mifumo ya kisekula, inayoungwa mkono na Magharibi kama vile Azimio 2254 la Umoja wa Mataifa. Hili linazua maswali muhimu sana kuhusu iwapo tumaini la kweli linaweza kuwepo bila kukataa utawala wa kigeni na kuzipa kipaumbele kanuni za Kiislamu.

Soma zaidi...

Amerika ya Trump Itashindwa Kufanya Kile ambacho Kikongwe Biden Hakuweza Kukifanya

“Rais mteule wa Marekani Donald Trump ametoa kauli kadhaa zenye utata ambazo zinaakisi waziwazi ukubwa wa tofauti katika sera za ndani na nje za Marekani na za Rais anayeondoka wa chama cha Democrat Joe Biden. Kwa upande wa sera ya mambo ya nje, Trump alisema atakomesha kile alichokitaja kuwa machafuko katika Mashariki ya Kati, kusitisha vita nchini Ukraine, na kuzuia kuzuka kwa Vita vya Tatu vya Dunia, bila kueleza jinsi atakavyofanya haya yote...

Soma zaidi...

Ziara ya Biden ya Dakika za Mwisho Afrika: Kuimarisha Ajenda ya Ukoloni na Unyonyaji wa Marekani

Jumatano ya tarehe 04/12/2024 Rais wa Marekani Joe Biden alihitimisha ziara yake ya siku tatu nchini Angola. Katika siku ya mwisho ya ziara yake, Biden alitembelea mradi wa Ukanda wa Lobito, mradi wa reli inayojengwa kwa ufadhili wa Marekani yenye kilomita 1,300 inayoanzia Zambia kwenye utajirim kubwa wa madini ya shaba hadi bandari ya Lobito kusini magharibi mwa taifa la Angola. Pia, Biden alifanya mkutano na maraisi wa Angola, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, Zambia na Makamu wa Rais wa Tanzania (VOA Africa 05/12/2024).

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu