Jumapili, 24 Dhu al-Hijjah 1445 | 2024/06/30
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mashirika ya Leo ya Vyombo vya Habari si Chochote isipokuwa ni Chombo cha Dola Ovu za Kilimwengu

Ingawa vyombo vya habari vinaitwa “nguzo ya nne ya demokrasia,” vikionyesha kutoegemea upande wowote na fikra yake, kama mamlaka ya mahakama kwa mfano, uhalifu uliofanywa na serikali ya Kiyahudi huko Gaza, na katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, ulitosha kufichua madai haya. Uhalifu huo ulifichua ukweli kuhusu vyombo vya habari na wanahabari. Jinai hizo zilionyesha wazi kwamba hakuna mamlaka ya kimaadili au uhalali, bali kwa ajili ya nguvu ya unyama, inayowakilishwa na dola za kimataifa na silaha zao duniani, ikiwemo Ulimwengu wa Kiislamu, ikiwa ni pamoja na watawala, serikali, na taasisi za vyombo vya habari.

Soma zaidi...

Operesheni Nyengine Dhidi ya Ugaidi

Uongozi wa juu wa Pakistan umeidhinisha kuanzishwa kwa operesheni mpya ya kijeshi Inayoitwa Azm-e-Istehkam. Mpango huo mpya wa kijeshi unatarajiwa kuangazia vitisho vya usalama wa ndani na wapiganaji wenye silaha wanaovuka kutoka Afghanistan, huku kukiwa na taharuki inayoongezeka kati ya Islamabad na watawala wa Taliban jijini Kabul.

Soma zaidi...

Sintofahamu ya Benki ya Maziwa ya Binadamu: Khilafah kwa Njia ya Utume Inatatua Matatizo ya Kibinadamu kwa Kuregelea Uislamu

Gazeti la ‘The Daily Times’ liliripoti kuwa, “Sindh anasimamisha benki ya maziwa ya binadamu, inauregesha mpango huo kwa Baraza la Itikadi la Kiislamu... Benki ya kwanza ya maziwa ya binadamu nchini Pakistan iliundwa mapema mwezi huu na Taasisi ya Sindh ya Afya ya Mtoto na Matibabu ya Watoto (Neonatology)

Soma zaidi...

Kifurushi Kipya cha Ushuru Kinathibitisha Jinsi Wale Wanaojipamba kwa Neno “Uadilifu” Walivyo Wakatili

Ufahamu wa mfumo wa mahakama wa Uturuki kuhusu uadilifu ni kuwaadhibu Waislamu wanaopinga ukatili unaofanywa dhidi ya Waislamu nchini Uturuki na duniani kote, na kuwaachilia huru wanasiasa wanaolaghai umma, na ni kuwatangaza Waislamu wenye fikra za Kiislamu, na wanaotamani maisha ya Kiislamu, ambao hawajatenda jinai yoyote, kuwa ni magaidi na kuwahukumu kwenye dhulma, mateso na kifungo.

Soma zaidi...

Mayatima wa Gaza Wamwaga Machozi kwa ajili ya Wazazi Waliotoweka na Uchungu wa Njaa siku ya Idd

Miezi 8 ya awamu mpya ya vitendo vya uvamizi, UNICEF inakadiria kuwa angalau watoto 17,000 mjini Gaza wako peke yao au kutenganishwa na familia zao. Tedros Adhanom Ghebreyesus, mkuu wa Shirika la Afya Duniani la Umoja wa Mataifa, alionya kwamba “idadi kubwa ya wakaazi wa Gaza sasa wanakabiliwa na janga la njaa na hali za uhaba wa chakula."

Soma zaidi...

Mbweha ni Mbwa Mwitu Anayetuma Maua… Mbweha Ana Hila Nyingi…

Aliyekuwa balozi wa Marekani katika umbile la Kiyahudi, Martin Indyk, mnamo Alhamisi tarehe 20 Juni aliamua kuondoa mwaliko kwa Waziri Mkuu wa Kiyahudi Benjamin Netanyahu kutoa hotuba mbele ya Bunge la Congress. Hii ni ili aombe radhi kwa kuutuhumu utawala wa Rais Joe Biden kwa kuinyima silaha “Israel,” huku vyombo vya habari vya Kiyahudi vikisema kuwa Netanyahu anapendelea makabiliano ya hadharani na Washington.

Soma zaidi...

Matukio mjini Gaza Yanaonyesha Kwa Uwazi Jinsi Uislamu Ulivyo Bora Kiakhlaki na Kifikra kuliko Thaqafa Danganyifu ya Kimagharibi ambayo Kirongo Inaitwa ni Mwangaza

Shirika karagosi la vyombo vya habari liitwalo CNN lilichapisha makala ya propaganda ya Wazayuni mnamo Juni 12, 2024 yenye kichwa: “Mateka wa Israel” walikabiliwa na “adhabu” wakati wa miezi minane katika uzuizi wa Hamas, familia moja yasema.” Makala hiyo iliundwa na watu watano na inazungumza juu ya kile familia ya mmoja wa mateka, Andrey Kozlov -27, ilisema baada ya IDF kuua watu 274 ili kumwachilia yeye na mateka wengine watatu mnamo Juni 9.

Soma zaidi...

Tanzania na Janga la Utegemezi

Jumapili ya tarehe 02 Juni, Juni 2024, Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na serikali ya Korea Kusini zilitia saini mikataba ya makubaliano ya ushirikiano kati ya nchi hizo mbili jijini Seoul. Mikataba hiyo ilijumuisha mkopo wa dolari bilioni 2.5 (Tsh trilioni 6.5) uliotolewa na Korea Kusini chini ya Mfuko wa Ushirikiano wa Maendeleo ya Kiuchumi wa Korea Kusini (EDCF) kwa ajili ya miradi mbalimbali ya miundombinu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu