Alhamisi, 05 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/08/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kuhuisha Uislamu: Njia Pekee ya Kuepuka Majanga

Mafuriko ya hivi majuzi nchini Pakistan yameharibu Khyber Pakhtunkhwa na Sindh, huku maeneo mengine yakipambana na barabara zilizojaa maji ambayo yamegeuza maisha ya kila siku kuwa hatari. Masaibu ya kupoteza maisha na riziki katika KPK yamewaacha watu na hofu. Kinachosumbua zaidi ni kukosekana kwa vifaa sahihi vya uokoaji – na kufanya wengi kuhoji uwezo wa serikali kujibu. Wafanyikazi wa uokoaji wanaachwa wakifanya kila kitu kwa mikono, na kwa mara nyingine tena, ni watu wa eneo hilo ambao, waliopata ukakamavu kwa miaka ya kupuuzwa, wanajua lazima wajitegemee wenyewe kwa sababu ima utakuja msaada mdogo hautakuja kabisa.

Soma zaidi...

Uongozi wa Kiislamu Unapokosekana, Ukandamizaji Hutawala

Marekani kwa mara nyengine tena imefichua hali yake ya kiuadui ya sera yake ya kibeberu ya mambo ya nje kwa kutuma manuari tatu kuelekea pwani ya Venezuela. Washington inahalalisha hatua hiyo kupitia tuhuma za muda mrefu kwamba Venezuela inashiriki katika ulanguzi wa madawa ya kulevya-shtaka ambalo Caracas inakataa vikali kama lisilo na msingi na linalochochewa kisiasa.

Soma zaidi...

Uislamu ni Ujumbe kwa Wanadamu Wote!

Leo hii, watawala mafisadi na wasio na thamani ambao wamejinyakulia madaraka katika ardhi za Waislamu kwa kujidai kuwa wao ndio viongozi wa Uislamu, wanaonyesha na kujifakharisha juu ya mafanikio ya Waislamu huko nyuma, kuwa ni tunu za kihistoria na kiroho, bila ya kuhusisha amri za Shariah kwao wenyewe na mfumo wao wa utawala. Wanazitumia hisia za Waislamu kwa kuwalaza usingizi na kuzikandamiza hasira zao, ambazo hukimbilia uhuru na kujitahidi kutabikisha Shariah katika maisha yao.

Soma zaidi...

Uhuru wa Kweli kwa Indonesia

Sherehe ya miaka 80 ya Siku ya Uhuru wa Indonesia ilichangamshwa na mavazi ya kitamaduni ya kupendeza katika Kasri la Merdeka, Jakarta, Jumapili, Agosti 17, 2025. Waziri wa Afya Budi Gunadi Sadikin alihudhuria akiwa amevalia vazi la Batak, akisema alilichagua kwa sababu ya turathi ya mke wake. Waziri wa Nishati na Rasilimali za Madini Bahlil Lahadalia alivalia vazi la kitamaduni la Solo, akibainisha kuwa hapo awali alikuwa amevaa mavazi ya Papua, Sulawesi, na Maluku. Rais Prabowo Subianto alionekana akiwa amevalia Nusantara yenye rangi ya pembe za ndovu akiwa na peci nyeusi, songket sarong, yenye maua ya yasmini. Watu mashuhuri Raffi Ahmad na Nagita Slavina walivalia mavazi ya Kijava, huku Raffi akiwakumbusha wananchi kuchangia vyema kwa taifa. Mabalozi kutoka nchi marafiki walihudhuria wakiwa wamevalia suti rasmi, huku wananchi wengi pia wakiwa wamevalia mavazi ya kikanda, yakionyesha umoja katika utofauti katika sherehe hizo.

Soma zaidi...

Ndoto ya Kikoloni ya ‘Dola Mbili’ kwa Palestina

Wakati Gaza ikiendelea kuungua, huku makumi ya watu wakiuawa katika Ukanda huo kila siku, huku wakaazi wake wakiendelea kufa kwa njaa, na wakati ghasia zikiongezeka katika Ukingo wa Magharibi mikononi mwa uvamizi wa kinyama wa Kizayuni, kumekuwa na msukumo mpya, hasa wa baadhi ya nchi za Magharibi, kwa ajili ya ‘Suluhisho la Dola Mbili’ kwa Palestina ambayo wanatoa hoja kuwa litaweza kutatua mzozo wa muda mrefu katika eneo hilo. Ufaransa, Uingereza na Canada miongoni mwa mataifa mengine zimetangaza nia yao ya kuitambua dola ya Palestina, ikiwa masharti maalum yatatimizwa.

Soma zaidi...

Marufuku ya Vitabu ya Serikali ya Kibaniani: Jaribio la Kufuta Mapambano na Mihanga ya Kiislamu katika Kashmir Inayokaliwa Kimabavu

Katika onyesho la wazi la ukosefu wa usalama na unafiki, serikali inayoitwa ya “kidemokrasia” ya India, chini ya utawala wake wa kibaniani wa BJP, imetoa amri ya kupiga marufuku vitabu 25 vinavyoandika uhalisia wa kihistoria wa ukaliaji wake wa kimabavu wa Kashmir. Hatua hii, ya tarehe 5 Agosti 2025, inatoka kwa Idara ya Mambo ya Ndani ya idara wa Jammu na Kashmir, ikitangaza kwamba kazi hizi “feki” chini ya Kifungu cha 98 cha Bhartiya Nyaya Sanhita 2023, ikizituhumu kwa kueneza “simulizi za uwongo”, kupigia debe kujitenga, na kutukuza “ugaidi”.

Soma zaidi...

Wamisri Wawili Wapotezwa Kwa Nguvu Baada ya Kuwataka Maafisa wa Usalama Kupinga Mzingiro wa Gaza

Vijana wawili wametoweka baada ya video yao kusambaa mitandaoni inayoonyesha wakivamia kituo cha polisi katika makao makuu ya Usalama wa Dola katika kituo cha polisi cha Ma’asara huko Helwan kusini mwa Cairo, ambapo waliwaweka wanausalama kwenye seli ya gereza. Kusudio la hatua hii ilikuwa kupinga utepetevu wa maafisa kwa watu wa Gaza.

Soma zaidi...

Heshima yote ni kwa Mwenyezi Mungu

Bunge la Seneti mnamo Alhamisi lilipitisha azimio kwa kauli moja, kulaani tukio la mauaji ya wenza mchana kweupe kwa maagizo ya Jirga kwa jina la kile kinachoitwa “mauaji ya heshima” huko Balochistan. Lilisema mauaji haya ya kinyama hayawezi na hayapaswi kufunikwa na hoja yoyote ya kitamaduni, kikabila, au kimila kwa kisingizio cha kile kinachojulikana kama ghairat au “heshima.” Kwa kweli ni uhalifu ambao umelivunjia heshima taifa. Jaribio lolote la kuhalalisha uhalifu kama huo kwa msingi wa “desturi au heshima” halikubaliki kabisa, kama ilivyo kwa mchakato mzima wa kulaumiwa kwa mwathiriwa.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu