Kesi 379 za upotezwaji wa lazima ziliwasilishwa kwa Tume ya Uchunguzi juu ya Kupotezwa kwa Kulazimishwa (COIOED) mnamo 2024. Watawala wa Waislamu huwateka nyara wale wanaowawajibisha, ni wakali kwa Waislamu na wana huruma na maadui. Hawakumnyonga jasusi na muuaji wa Kihindi Kulbhushan Yadav. Walimwachilia huru jasusi na muuaji wa Kimarekani Raymond Davis. Hata hivyo, walimteka nyara Naveed Butt, msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Pakistan, mnamo Mei 11, 2012. Naveed Butt alitoa wito wa ukombozi kutokana na ukoloni wa Marekani na kusimamishwa kwa Khilafah Rashida. Baada ya zaidi ya miaka kumi na mbili, watawala wangali hawajamwachilia huru. Ni lazima kwa umma na majeshi yake kuwang’oa madhalimu miongoni mwa watawala na kusimamisha Khilafah Rashida.