Jumanne, 15 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/07
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Baada ya Mashambulizi ya Umbile la Kiyahudi kwa Sumud Flotilla Wito wa Dharura kwa Maafisa na Askari katika Majeshi ya Waislamu Jeshi Husagwa sagwa na Jeshi Pekee

Enyi Wanajeshi: Mumeshuhudia shambulizi la umbile la Kiyahudi dhidi ya Sumud Flotilla iliyosafiri bahari ili kuvunja kuzingirwa kwa kaka na dada zenu mjini Gaza, na mkasikia vilio vyao vya kuomba msaada, na mkaona kwa macho yenu uovu wa watawala, ufisadi wao, ukosefu wao wa hisia, na kufeli kwao kuinusuru Gaza na wanaharakati wa flotilla. Imekudhihirikieni pia kwamba watawala hao walimfanyia khiyana Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kuwaangusha Waumini walipoangusha hadharani kile walichokiita “chaguo la vita” kwa kunyenyekea matamanio ya viongozi wa ukafiri.

Soma zaidi...

Marekani Yaendesha Uharibifu... Na Watawala ni Watiifu kwa Miradi Yake ya Kikoloni!

Mamlaka zilizofuatana juu ya nchi yetu hazikujiepusha na kutii mashinikizo ya Marekani, kwa kukubali kushiriki katika kuimarisha mkakati wake wa kikoloni katika kuitawala dunia nzima, ikiwemo kanda yetu ya Waarabu na eneo letu la Afrika. Hii ni kama vile kusainiwa na utawala wa Sebsi juu ya uamuzi wa Barack Obama wa kuipa Tunisia hadhi ya Mshirika Mkuu Asiyekuwa mwanachama wa NATO, au kufungua nchi yetu kwa mpango wake barani Afrika kwa kuandaa, kwa mwaka wa nane mfululizo, mazoezi ya kijeshi ya African Lion 2025, ambapo Jenerali Dagvin Anderson, kamanda wa Kamandi ya Marekani ya Umoja wa Mataifa Afrika (AFRICOM) alisema mbele ya Kamati ya Huduma za Silaha katika Bunge la Congress la Marekani kwamba Morocco na Tunisia ni miongoni mwa washirika wenye uwezo mkubwa wa kusafirisha usalama barani humo.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi Salih bin Muhammad al-Shafrah

Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Tunisia inaomboleza mmoja wa Mashababu wake, ndugu Salih bin Muhammad al-Shafrah, aliyefariki mnamo Jumamosi, tarehe ishirini na moja ya Rabi’ al-Awwal 1447 H sawia na 13/09/2025 M. Alikuwa miongoni mwa Mashababu wa Hizb ut Tahrir katika eneo la al-Qayrawān, ambaye alifanya kazi katika safu zake wakati wa zama zenye giza kuu za ukandamizaji na dhulma. Hakika alikuwa ameshikilia imara da‘wah yake, akijitolea katika kuibeba, akilingania Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, mwenye kuiamini ahadi ya Mola wake Mlezi na bishara njema ya Mtume wake Mtukufu (saw), mpaka alipofariki dunia. Hivyo ndivyo tunavyomhisabu, na wala hatumtakasi yeyote mbele ya Mwenyezi Mungu.

Soma zaidi...

Wilayah Tunisia Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Ndugu Basheer Qassila

Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Tunisia inaomboleza mmoja wa watu wake waliojitolea na wabebaji wa da'wah: mzee na kaka, simba wa da'wah, Basheer Qassila, ambaye alifariki mnamo Jumapili, tarehe 26 Dhul-Hijjah 1446 H, sawia na 22 Juni 2025 M, baada ya kupambana na maradhi yaliyomdhoofisha mwili wake lakini katu hayakuzima moto wa ujumbe wake wala azma yake ya kufanya kazi pamoja na safu akijitahidi kurudisha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu kwa kusimamisha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Ustadh Hassan Nouair

Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Tunisia inaomboleza kifo cha mmoja wa watu wake miongoni mwa Wabebaji Da’wah, Ustadh Hassan Nouair, aliyefariki dunia leo, Ijumaa, tarehe 24 Dhu al-Hijjah 1446 H, sawia na 20/06/2025 M, baada ya mapambano na maradhi ambayo yalidhoofisha mwili wake lakini hayakuzima moto wa ujumbe wake wala azma yake ya kufanya kazi katika safu za wale wanaojitahidi kuregesha mfumo kamili wa maisha wa Kiislamu kwa kusimamisha Khilfah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Tanzia ya Mbebaji Ulinganizi: Mabrouk Ben Nasser

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia inaomboleza kwa huzuni na majonzi makubwa kuondokewa na ndugu yetu Mabrouk Ben Nasser, aliyefariki siku ya Alhamisi, 23 Dhu al-Hijjah, 1446 H, sawia na 19 Juni 2025 M. Alikuwa mmoja wa Mashababu (wanachama) wa Hizb ut Tahrir ambao walifanya kazi ndani ya safu zake wakati wa nyakati za giza za dhulma na ukandamizaji, akiwa amezuiliwa kwenye jela za Bourguiba na kisha Ben Ali. Alitumia muda wake kwa subira na imani, akiendelea kushikamana na ulinganizi wake na kujitolea kuubeba, akilingania Khilafah Rashida kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir Wakutana na Mkuu wa Harakati ya Wokovu wa Kitaifa

Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia inakutana na Bw. Ahmed Najib Al-Shabi, mkuu wa Harakati ya Wokovu wa Kitaifa, jana, Jumanne 11/02/2025. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hizb kwenye makao makuu ya Sakra Ariana, na uliongozwa na Bwana Al-Arabi Karbaka, mwanachama wa Hizb ut Tahrir. Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Bw. Al-Habib Hajji, Tamim Noura, Dkt. Faisal Darghouth, na Mhandisi Yasser Al-Anwar, wanachama wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir/Wilayah Tunisia.

Soma zaidi...

Ni Rasmi: Mamlaka nchini Tunisia Zinasaidia Amerika na Umbile la Kiyahudi katika Mauaji ya Halaiki dhidi ya Watu Wetu huko Gaza na Palestina yote

Mji wa Vicenza wa Italia ulishuhudia hafla ya kusainiwa kwa itifaki ya mwisho ya taratibu za kupanga mazoezi ya kijeshi ya Simba wa Afrika 2025 nchini Tunisia. Makubaliano hayo yalitiwa saini kati ya Kanali Mwandamizi wa Tunisia Mguidich Mejid na Kanali wa Marekani Drew Conover, Mkurugenzi wa Mafunzo wa Jopo Kazi la Jeshi la Marekani la Kusini mwa Ulaya.

Soma zaidi...

Kushiriki katika Mafunzo ya Kijeshi pamoja na Adui wetu ni Fedheha kwa Majeshi yetu na Usaliti kwa Watu wetu mjini Gaza

Mnamo tarehe 1/11/2024, Wizara ya Ulinzi ilitoa taarifa ikisema: “Tunisia itakuwa mwenyeji, kuanzia Novemba 4 hadi 15, wa zoezi la majini la kimataifa “PHOENIX EXPRESS 24”, kwa ushirikiano na Kamandi ya Marekani ya Afrika, kwa ushiriki wa takriban wanajeshi 1,100 na waangalizi wanaowakilisha nchi dada na rafiki 12, ambazo ni Algeria, Libya, Morocco, Mauritania, Senegal, Uturuki, Italia, Malta, Ubelgiji, Georgia, na Marekani, pamoja na Tunisia, nchi mwenyeji.”

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake cha Hizb ut Tahrir katika Wilayah Tunisia kinazindua kampeni yenye kichwa “Ufisadi wa Elimu Unatokana na Ufisadi wa Serikali, na Marekebisho Yanahitaji Mabadiliko ya Utawala.”

Kwa kuzingatia mgogoro mkubwa unaoathiri sekta zote muhimu nchini kutokana na ushawishi mkubwa wa wakoloni wanaodhibiti taasisi zake kuu, kuzorota kwa sekta ya elimu kumekuwa na athari kubwa sana. Kuzorota huku kunaathiri kila mtu nchini Tunisia— kina baba, kina mama, walimu, na wanafunzi vilevile—kutokana na mshikamano wake tata na pande nyingi zinazopishana.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu