Baada ya Mashambulizi ya Umbile la Kiyahudi kwa Sumud Flotilla Wito wa Dharura kwa Maafisa na Askari katika Majeshi ya Waislamu Jeshi Husagwa sagwa na Jeshi Pekee
- Imepeperushwa katika Tunisia
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Enyi Wanajeshi: Mumeshuhudia shambulizi la umbile la Kiyahudi dhidi ya Sumud Flotilla iliyosafiri bahari ili kuvunja kuzingirwa kwa kaka na dada zenu mjini Gaza, na mkasikia vilio vyao vya kuomba msaada, na mkaona kwa macho yenu uovu wa watawala, ufisadi wao, ukosefu wao wa hisia, na kufeli kwao kuinusuru Gaza na wanaharakati wa flotilla. Imekudhihirikieni pia kwamba watawala hao walimfanyia khiyana Mwenyezi Mungu na Mtume wake na kuwaangusha Waumini walipoangusha hadharani kile walichokiita “chaguo la vita” kwa kunyenyekea matamanio ya viongozi wa ukafiri.