Je, Ugaidi ni Quran na Vitabu, Enyi Mliofilisika
- Imepeperushwa katika Uchambuzi
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Tovuti ya Russia Today ilichapisha ripoti ya habari mnamo tarehe 5/2/2025 ikisema kwamba "Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilisambaratisha seli ya magaidi yenye mafungamano na Hizb ut Tahrir katika Rasi ya Crimea na kuwakamata watu watano waliokuwa wakisajili wafuasi wa Hizb, ambayo imepigwa marufuku nchini Urusi." Ripoti hiyo ilijumuisha video inayoonyesha operesheni ya ukamataji na uvamizi wa nyumba, ambapo ilionekana wazi kwamba kile ambacho idara ya usalama ya Urusi ilichukua kutoka kwa nyumba za Mashababu ni nakala za Al-Quran Al-Kareem, vitabu, na vijitabu vya kisiasa na kifikra vya Kiislamu - machapisho maarufu ya Hizb ut Tahrir kwa jina pamoja na maalumati yaliyomo.