Ijumaa, 28 Ramadan 1446 | 2025/03/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mafanikio ya Kweli Mpaka Siku ya Mwisho ni kwa Umma wa Kiislamu Pekee

Hata leo, katikati ya misiba isiyohesabika na isiyoweza kuvumilika, Ummah huu umethibitika kuwa thabiti katika kitambulisho chake na hivyo hauwezi kuangamizwa. Imethibitika kuwa unastahiki vyeo ulivyotunukiwa na Mola wa walimwengu, Mwenyezi Mungu Azza wa Jall! Angalia Kashmir, India, Afghanistan... Angalia Waislamu wa Syria, Turkestan Mashariki, Myanmar, katika nchi za Afrika, duniani kote, na mwisho kabisa Waislamu wa Palestina na hasa Gaza! Magaidi hao wa Kizayuni wameshindwa katika kila lengo lao kuhusu Gaza. Ummah huu umethibitisha mara kwa mara, kwamba uwepo wake hauzimiki! Hata adui zake wawe wakatili kiasi gani!

Soma zaidi...

Je, Mafanikio kwa Waislamu yanaweza Kupatikana kupitia Siasa za Kidemokrasia?

Kutokana na mauaji makubwa ya halaiki yanayotokea Gaza na dori ya Marekani katika kusaidia na kuunga mkono yaendelee, kumekuwa na mijadala mingi miongoni mwa Waislamu kuhusu jinsi ya kujihusisha zaidi kisiasa na jinsi jamii ya Kiislamu inavyoweza kuwa mstari wa mbele katika kuunda siasa za Marekani ili kubadilisha dunia kuwa bora. Ndani ya mijadala hii, mengi yanasemwa kuhusu kujishughulisha na uraia, kujiunga na kuunga mkono wagombea mahususi wa kisiasa, kunyima kura zao kama aina ya adhabu, na hatimaye kupata Waislamu zaidi, au "washirika" kwenye nyadhifa katika ngazi za dola na majimbo. Kuna gumzo hata miongoni mwa kina dada wakidai kwa furaha kwamba wanajaribu kumlea kijana au binti yao kuwa Rais wa kwanza wa Marekani Muislamu. Haya yanawekwa kama mafanikio sio tu kwa Waislamu wa Amerika, lakini Waislamu kote ulimwenguni. Huu unawekwa kama mpango wa mafanikio licha ya ukweli kwamba vyama vyote vya kisiasa, iwe vya rangi ya samawati, nyekundu, au kijani vinaunga mkono umbile la Kizayuni, au dola zengine zenye kufanya mauaji ya halaiki mithili ya China na India.

Soma zaidi...

Wanawake Waliofaulu katika Uislamu wana Sifa hizi

Katika Uislamu, hakuna fahamu ya kuingia Jannat kulingana na nani unamjua na hadhi yako ya kidunia ni ipi. Wote walisifiwa na Mwenyezi Mungu (swt) kwa sababu ya sifa zao za pamoja za kuwa karibu katika utendaji wao wa kuwa kama mfano wa Mtume (saw). Ikiwa tunataka hadhi sawa ya kuingia Jannat lazima basi tufuate mfano wao wa kufanikiwa. Sifa zifuatazo basi zinahitajika.

Soma zaidi...

Vipi Tunaweza Kuwa Miongoni Mwa Wenye Mafanikio hapa Duniani na Akhera?

Mafanikio yanazunguka ulimwengu huu na Akhera, anayemcha Mwenyezi Mungu (swt) humsahilishia mambo yake, hubariki matendo yake, huitengenezea nafsi yake, mke wake na watoto wake, humpa njia ya kutokea katika matatizo, humruzuku kutoka katika vyanzo asivyotarajia, na humtosheleza. Zaidi ya hayo, Yeye (swt) humlipa sana subira yake wakati wa matatizo. Wengine wamesema: "Mafanikio ni kupata ushindi na kufikia lengo la mtu. Katika dunia hii, maana yake ni kupata furaha inayoleta kutosheka katika maisha. Katika Akhera, ina jumuisha mambo manne: uwepo milele usio na mwisho, heshima bila fedheha, mali bila umasikini, na elimu bila ya ujinga."

Soma zaidi...

Mafanikio ya Kweli: Safari Inayoanza Ramadhan

Ramadhan inapoingia katika maisha yetu kila mwaka, huleta mabadiliko-wakati wa uwazi ambapo tunarudi nyuma kutoka kwa mazoea yetu ya kila siku na kujiuliza maswali ya kina. Ni mwezi ambapo kwa kawaida tunatathmini upya uhusiano wetu na Mwenyezi Mungu (swt), vipaumbele vyetu, na mwelekeo wa maisha yetu. Katika wakati huu mtakatifu, tunaanza kutafakari: Je, Mafanikio yanamaanisha nini hasa?

Soma zaidi...

Ramadhan, Fursa ya Kutafakari na Kubadilika

Ramadhani ni mwezi wa kheri na baraka, na fursa adhimu ya kujitahidi kupata mafanikio ya duniani na akhera. Ni msimu wa utiifu, na uwanja wa kushindana katika mambo ya kheri na kufikia uchamungu ili kupata radhi za Mwenyezi Mungu, ambayo ndio mafanikio ya kweli. Ni mwezi maalum wa fadhila, si kwa sababu tu ni mwezi wa saumu na ibada, bali pia kwa sababu ni fursa adhimu ya kutafakari uhusiano wetu na Mwenyezi Mungu na kutathmini upya mwenendo wa maisha yetu ili kubadilika na kuwa bora zaidi, na kuzingatia malengo yetu ya kweli na kufafanua fahamu ya mafanikio katika maisha yetu, si kwa mtazamo wa Kidunia, bali kwa mtazamo wa kidini, kiroho na kiakhlaqi.

Soma zaidi...

Je, Ugaidi ni Quran na Vitabu, Enyi Mliofilisika

Tovuti ya Russia Today ilichapisha ripoti ya habari mnamo tarehe 5/2/2025 ikisema kwamba "Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilisambaratisha seli ya magaidi yenye mafungamano na Hizb ut Tahrir katika Rasi ya Crimea na kuwakamata watu watano waliokuwa wakisajili wafuasi wa Hizb, ambayo imepigwa marufuku nchini Urusi." Ripoti hiyo ilijumuisha video inayoonyesha operesheni ya ukamataji na uvamizi wa nyumba, ambapo ilionekana wazi kwamba kile ambacho idara ya usalama ya Urusi ilichukua kutoka kwa nyumba za Mashababu ni nakala za Al-Quran Al-Kareem, vitabu, na vijitabu vya kisiasa na kifikra vya Kiislamu - machapisho maarufu ya Hizb ut Tahrir kwa jina pamoja na maalumati yaliyomo.

Soma zaidi...

Usasa wa Kiislamu (الحداثة الإسلامية): Shambulizi kwa Sunnah ya Mtume

Usasa wa Kiislamu (الحداثة الإسلامية) unakusudia fikra inayotaka kutafsiri upya Uislamu ili kuwiana na maadili na miundo ya mfumo wa kilimwengu wa kiliberali wa Kimagharibi. Ikiibuka katika karne ya 19, wimbi hili la mageuzi lilisukumwa na watu mashuhuri kama vile Jamal ud Din Afghani, Muhammad Abduh, Rashid Rida, na Syed Ahmed Khan. Juhudi zao zililenga kufanya maridhiano ya Uislamu na mifumo ya kisasa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ufafanuzi huu upya, hata hivyo, mara nyingi ulihusisha upotoshaji wa kanuni za Kiislamu ili kuendana na desturi zinazobadilika za ulimwengu wa kisasa, ikiwa ni pamoja na fahamu za Kimagharibi kama vile utaifa, urasilimali, sheria za binadamu, haki za binadamu, usawa wa kijinsia, na maelewano ya dini mbalimbali.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu