Jumapili, 27 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/19
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Marekani inatia Mikono yake Michafu katika Kila Mzozo; Sudan sio Tofauti

Katika kipindi cha muongo mmoja uliopita, Amerika imejidhihirisha kama mpangaji mkuu nyuma ya baadhi ya mizozo ya kunyama na ya ghasia zaidi kote duniani. Kutoka Urusi na Ukraine hadi India na Pakistan hadi China na Taiwan hadi Syria, Iraq, Afghanistan, Yemen, Kenya, Mali, Cameroon, na hii ni mifano michache tu! Hata hivyo, hakuna kilichoifichua Marekani zaidi ya uungaji mkono wake usio na haya na ushiriki wake katika mauaji ya halaiki yanayotokea Gaza dhidi ya watu wa Palestina. Kabla ya uvamizi, kuzingirwa kabisa, na kuangamizwa kwa Gaza, watu wengi hawakujua jinsi serikali ya Marekani ilivyokuwa chafu na jinsi wanavyoweza kuwatembeza wachezaji kama poni kwenye bao la chess.

Soma zaidi...

Kuzaliwa kwa Uongofu: Nuru Inayoondoa Giza Lililopo

Sayari ya Dunia, na hasa Bara Arabu, lilikuwa likiishi katika giza kuu lililofanya maisha ya binadamu yafanane na kuzimu. Kulikuwa na giza katika nyanja za itikadi, siasa, uchumi, mahusiano ya kijamii, na nyanja zote za maisha. Vita viliwasaga watu bila sababu, wenye nguvu walikuwepo huku wanyonge wakipotea na kutokuwepo, dhulma ilitanda maeneo yote, na utumwa ulifikia viwango vyake vya chini kabisa na vya udhalilishaji kabisa.

Soma zaidi...

Usaliti wa Magharibi kwa Wale Wanaoitumikia Katika Vita Dhidi ya Uislamu

Mkakati na sera ya Wakoloni wa Magharibi kuelekea Umma wa Kiislamu imejikita katika kupiga vita Uislamu kama fahamu ya kihadhara na kimfumo. Ilifanya kazi kupitia njama kubwa na ovu za kuivunja Dola ya Kiislamu, kuikata vipande vipande, na kuzuia kuregea kwake madarakani na kuwaunganisha Waislamu. Ili kutekeleza sera na njama zake, Wakoloni wa Magharibi waliwaajiri baadhi ya wana wa Waislamu, wakiwalea kwa uangalifu katika fikra, siasa, utawala na vyombo vya habari. Kama vile orientalisti mmoja alivyosema, “Mti wa Uislamu lazima ukatwe kupitia mmoja wa watoto wake.”

Soma zaidi...

Hakuna Suluhisho kwa Suala la Sudan Isipokuwa Kutawalisha Uislamu

Tangu uhuru wake mnamo tarehe 1/1/1956, Sudan imeshuhudia mfululizo wa mapinduzi ya kijeshi. Ya kwanza ilikuwa jaribio lililofeli lililoongozwa na Ismail Kabida, ambaye alijaribu kupindua serikali ya kwanza ya kitaifa iliyoongozwa na Ismail al-Azhari. Hii ilifuatiwa na mapinduzi ya kwanza yaliyofaulu yaliyoongozwa na Luteni Jenerali Ibrahim Abboud mnamo Novemba 1958 dhidi ya serikali iliyochaguliwa ya al-Azhari.

Soma zaidi...

Mauaji ya Halaiki ya Sudan: Dori ya Omar al-Bashir

Ingawa mengi yanajulikana kuhusu mauaji ya halaiki yanayowakumba ndugu na dada zetu nchini Palestina, machache sana yanajulikana—au yanasambazwa—kuhusu wale walio nchini Sudan, ambao kwa muda wa miezi 18 iliyopita wamevumilia mauaji ya halaiki ya kimya kimya. Ukatili huo umeua zaidi ya watu 15,000, zaidi ya milioni 10 wamekimbia makazi yao, na kuacha nusu ya watu—watu milioni 25—wakikabili uhaba wa chakula na njaa.

Soma zaidi...

Ubwana Unaofifia: Mpango Mpya wa Mafuta wa Pakistan, Vita vya Kale na Sera ya AI

Mnamo Julai, Rais Trump wa Amerika alichapisha kwenye jukwaa lake la Ukweli wa Jamii. “Hivi punde tumemaliza mkataba na nchi ya Pakistan, ambapo Pakistan na Marekani zitafanya kazi pamoja katika kuendeleza hifadhi yao kubwa ya mafuta.” Mkataba wa mafuta ni sehemu ya mkataba mpana wa kibiashara kati ya nchi hizo mbili, ambapo Marekani imekubali kupunguza ushuru kwa bidhaa za Pakistan kutoka 29% hadi 19%, huku ikitishia kuweka ushuru wa adhabu kwa India, isipokuwa New Delhi imalize uagizaji mafuta ghafi kutoka Urusi.

Soma zaidi...

Waafghani Baina ya Nyundo ya Siasa za Pakistan na Kinoo cha Agenda ya Kikanda

Tangu mwaka wa 2023, serikali ya Pakistan imezidisha uhamishaji wa wakimbizi wa Afghanistan, hatua inayolenga kuishinikiza serikali ya mpito ya Afghanistan inayoongozwa na Taliban jijini Kabul kuwasilisha kikamilifu matakwa ya Amerika. Mawimbi ya Waafghani kuhamishwa kwenda Pakistan yana mizizi ya kihistoria tangu Jihad dhidi ya Muungano wa Kisovieti katika miaka ya 1980, vita vya wenyewe kwa wenyewe vilivyofuata, na uvamizi wa Marekani na kuikalia kijeshi Afghanistan kuanzia 2001 hadi 2021. Pakistan kihistoria imetoa kina cha kimkakati kwa Waislamu wa Afghanistan, shukran kwa mafungamano ya karibu ya kabila yanayovuka Mstari wa Durand.

Soma zaidi...

Mpango wa Mipaka ya Damu na Uhalifu wa Kujitenga kwa Darfur

Baada ya kuanguka kwa kutia shaka kwa miji mikubwa ya Darfur, na kuondolewa kwa jeshi kutoka kwao, mbele ya utekaji nyara wa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), pamoja na kuzingirwa kwa nguvu na vikosi hivi katika jimbo la mwisho lililosalia, Darfur Kaskazini na mji mkuu wake, Al-Fashir, wakati jeshi likishindwa kuwafukuza, ghafula yanakuja mazungumzo ya serikali sambamba yakiongozwa nao huko Nyala, mji mkuu wa Darfur Kusini, ambao wanaudhibiti, kwa ushiriki wa vibaraka wa Amerika kama vile Al-Hilu, na uungaji mkono wake kwa serikali hii, hata kuwa naibu ndani yake.

Soma zaidi...

Fahali Wanapopigana, Zinazoumia ni Nyasi “Sudan ni Mfano”

Sijapata katika historia msemo wenye ufasaha zaidi wa uovu wa ukoloni kuliko maneno ya Rabi ibn Amir, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kwa kamanda wa Kifursi: “Sisi ni watu ambao Mwenyezi Mungu amewatuma kuwatoa wanadamu kutoka katika ibada ya waja wengine hadi kwenye kumwabudu Mola wa waja wote.” Ijapokuwa kauli hii ilitolewa ili kubainisha lengo la ujumbe mtukufu wa Uislamu, unaowakirimu watu kutokana na kumwabudu kwao Mwenyezi Mungu, na kuhifadhi maisha yao, mali zao na heshima zao, hii wakati fulani hujidhihirisha kama kauli iliyo kinyume chake. Rehema ya Uislamu na uhuru unaowadhaminia watu unakinzana na utumwa wa watu na mataifa kwenye ukoloni, ambao unawaona kuwa ni mashini tu za kuzalisha dhahabu na pesa.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu