Je, Erdogan Anasubiri Mayahudi Waipige Mabomu Ankara Kabla ya Kuhamasisha Jeshi Lake?!
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan, katika hotuba aliyotoa wakati wa mkutano wa kundi la wabunge wa Chama cha Haki na Maendeleo katika Bunge la Uturuki, alisema: "Tunafahamu vyema lengo kuu la udanganyifu wa 'Ardhi iliyo Ahidiwa', na Mungu akipenda, hatutaruhusu kamwe." Alifafanua kwamba usalama wa Uturuki hauanzii katika mkoa wa Hatay kusini mwa Uturuki, bali Aleppo, Damascus, na Beirut. Aliendelea: "Ikiwa uonevu wa Israel hautasimamishwa, gharama haitalipwa na eneo hilo pekee, bali na wanadamu wote." Erdoğan alizisihi dola kuu duniani kuchukua msimamo wazi dhidi ya umbile hilo la Kizayuni, akisema: "Kuirudisha Israel katika kufuata sheria sio tena jukumu la baadhi ya nchi tu, bali ni jukumu la pamoja linalowaangukia wanadamu wote."



