Jumamosi, 23 Sha'aban 1446 | 2025/02/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Miaka Miwili Iliyopita Baada ya Tetemeko la Ardhi la Februari 6 Bado Mateso Hayana Mwisho

Mnamo Februari 6, 2023, matetemeko makubwa mawili ya ardhi yenye kipimo cha 7.8 na 7.5, yaliyopiga kusini na katikati mwa Uturuki na kaskazini mwa Syria, yaliathiri mikoa 11 na kusababisha uharibifu mkubwa na kupoteza maisha. Takriban watu 54,000 nchini Uturuki na 8,500 nchini Syria walipoteza maisha katika matetemeko haya ya ardhi huku kitovu cha matetemeko hayo kikiwa Kahramanmaraş. Jumla ya waliopoteza maisha ilizidi 62,000, na mamilioni ya watu wakabaki bila makao. Hata hivyo, baadhi ya wataalamu wa huru na rasilimali za ndani zinaonyesha kuwa idadi halisi inaweza kuwa kubwa zaidi.

Soma zaidi...

Marufuku ya Kyrgyzstan dhidi ya Niqab ni Jaribio la Kutapatapa la Utawala wake wa Kisekula Kukandamiza Kuibuka kwa Kitambulisho cha Kiislamu Miongoni mwa Watu wake

Kyrgyzstan imekuwa nchi ya hivi punde zaidi katika Asia ya Kati kupiga marufuku Niqab. Hatua hii ya kisheria ilianza kutekelezwa mnamo tarehe 1 Februari 2025 na ukiukaji huu utatozwa faini ya 20,000 som ($230). Nguo za Kiislamu za wanawake na ndevu za wanaume zimekuwa zikilengwa na serikali za Asia ya Kati kwa muda mrefu, ambapo dola zenye nguvu ya kisekula zinaogopa ushawishi unaoongezeka wa Uislamu. Wabunge wa Kyrgyzstan wametoa kisingizio duni kwamba marufuku hiyo inahitajika kwa sababu za usalama, ili nyuso za watu zionekane na watu binafsi kutambuliwa. Lakini wapinzani wanasema marufuku hiyo inawanyima wanawake uhuru wa kuvaa wanavyotaka.

Soma zaidi...

Wauyghur Pia Ni Sehemu ya Umma Bora, Musiwasahau

Tunapokaribia kumbukumbu ya mwaka wa 104 wa kuvunjwa kwa Khilafah, Umma wa Kiislamu unaendelea kupokea habari za ukandamizaji kutoka kwa maadui wake kila mahali, kuanzia Palestina hadi Syria, Sudan, Misri na China, ambako Waislamu wa Uyghur wanavumilia mateso na vikwazo vikali katika kila nyanja ya maisha yao.

Soma zaidi...

Kuganda Baridini hadi Kufa kwa Watoto Wachanga, na Njaa na Uuaji wa Watoto Hayatoshi Kukomesha Mauaji ya Halaiki huko Gaza!

Mnamo tarehe 30 Disemba, iliripotiwa kuwa mtoto wa 6 waliganda hadi kufa mjini Gaza ndani ya wiki mbili kutokana na hali ya baridi inayovumiliwa na wakimbizi wa Kipalestina katika mahema ya muda, waliohamishwa kutoka kwa nyumba zao kutokana na mashambulizi ya mara kwa mara ya Ukanda huo na uvamizi wa Kiyahudi. Ali al-Batran mwenye umri wa mwezi mmoja alifariki siku moja baada ya kaka yake pacha, Jumaa al-Batran, huko Deir el-Balah. Baba yao, Yahya Muhammad al-Batran, alisema kuwa Jumaa alipatikana kichwa chake kikiwa kama “donge la barafu”. Nariman, mama wa Sila Mahmoud al-Fassih mwenye umri wa siku 20, ambaye pia alifariki kutokana na kupungua kwa joto la mwili, alielezea kumkuta mtoto wake akiwa rangi ya bluu na kuuma ulimi wake huku damu ikimtoka mdomoni. Zaidi ya watu milioni 1.6 wa Gaza wamelazimishwa kuingia kwenye makaazi ya muda, wakiishi katika mahema hafifu ambayo hayatoi ulinzi kutokana na hali ya hewa ya baridi kali.

Soma zaidi...

Je! Mauaji na Jinai Hizi Zote Hazijachochea Hisia ya Wajibu kwa wale wenye Vyeo na Medali Kusonga katika Ulinzi wa Watu wa Gaza?!

Alfajiri ya mnamo Jumanne, Oktoba 29, 2024, vikosi vya Kiyahudi vilifanya mauaji mengine ya kutisha kwa kulipua jengo la orofa tano la familia ya Abu Nasr, ambalo lilikuwa lahifadhi watu waliokimbia makaazi yao katika Mradi wa Beit Lahiya kaskazini mwa Gaza. Mauaji haya yalisababisha vifo vya watu 93, wakiwemo watoto wasiopungua 25, huku zaidi ya 40 wakipotea na kadhaa kujeruhiwa, wengi wao wakiwa wamenaswa chini ya vifusi.

Soma zaidi...

Heshima ya Wanawake wa Kiislamu ni ya Khiyari katika Demokrasia za Kiliberali

Mnamo tarehe 3 Oktoba, CBS News iliripoti kwamba mwanamke mmoja Muislamu alizuiliwa na polisi wa Philadelphia ambao walimvua hijabu yake. Wakati wa saa 20 ya kukamatwa kwake, aliachwa wazi na hakupewa njia ya kubadilisha nguo zake. Kwa sasa ameajiri mshauri wa kisheria kutoka Baraza la Mahusiano ya Kiislamu la Marekani (CAIR) na anataka haki kwa unyanyasaji wake.

Soma zaidi...

Mauaji Mapya na Msimamo wa Majeshi yetu ni Ule Ule! Je, hakuna Mwenye Hekima Miongoni mwenu Awezaye Kurudisha Izza Tena?!

Mwenyezi Mungu Mtukufu alitufahamisha kuwa sisi ni Umma wa kheri na jihad, na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) alitupa bishara njema ya kwamba tutaifungua Roma, kwa hivyo Al-Quds iko karibu na ukombozi, Mwenyezi Mungu akipenda, kuwa mji mkuu wa dola inayokuja ya Khilafah, na historia kwa mapana yake yote inathibitisha kwamba sisi ni Ummah ambao hata tukilala kwa muda gani, tutaamka na kuwaondoa maadui zetu kwa pigo kubwa ambalo baada ya hapo hawana pa kukimbilia.

Soma zaidi...

Mauaji Yasiyokwisha ya Wanawake na Watoto wa Gaza Kamwe Hayatamalizika hadi Mlinzi na Ngao ya Ummah, Khilafah, Itakaposimamishwa tena

Huu ni mwaka ambao umeonyesha kwa mara nyingine tena ugumba wa mfumo wa sasa wa dunia, na serikali zake, Umoja wa Mataifa na kila mahakama na taasisi za kimataifa kuwalinda Waislamu wanaodhulumiwa dhidi ya dhalimu wao. Umbile la Kiyahudi limevuka kila mstari mwekundu, limevunja kila mwiko na limekiuka kila kanuni na sheria ya kibinadamu, lakini hakuna serikali ambayo ina utashi wa kisiasa wa kukomesha mauaji haya yasiyokoma.

Soma zaidi...

Kitengo cha Wanawake cha Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir Chafanya kwa Mafanikio Kongamano la Kimataifa la Wanawake Mtandaoni “Ukombozi wa Palestina... Changamoto na Bishara Njema”

Kitengo cha Wanawake cha Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir, kwa uratibu na wanawake wa Hizb ut Tahrir kote ulimwenguni, kilifanya kongamano la kimataifa la wanawake mtandaoni lenye mafanikio kwenye jukwaa la Zoom kwa kichwa “Ukombozi wa Palestina: Changamoto na Bishara Njema” mnamo siku ya Jumamosi, Oktoba 5, 2024. Mamia ya wanawake wanaozungumza Kiarabu kutoka kote duniani walihudhuria kongamano hilo, katika ukumbi wa mikutano na kwenye kurasa za Facebook za Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir. Wazungumzaji kutoka Palestina, Tunisia, Syria, Lebanon, Indonesia na Amerika walishiriki katika kongamano hilo.

Soma zaidi...

Kongamano la Kimataifa la Wanawake la Mtandaoni Lililoandaliwa na Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir, kwa Uratibu na Wanawake wa Hizb ut Tahrir Ulimwenguni

Mwaka mzima umepita tangu kuanza kwa Kimbunga cha Al-Aqsa na vita vikali vilivyofuata huko Gaza. Tangu tarehe 7 Oktoba mwaka jana, watu wa Gaza wamevumilia mitihani mikubwa, wakiishi katika machungu, mateso, na majanga yasiyohesabika.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu