Jumamosi, 18 Rajab 1446 | 2025/01/18
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Wilayah Uturuki: Amali Kubwa “Usiisahau Gaza wala Usikubali Kusahauliwa Kwake!”

Kwa kuzingatia mauaji ya kikatili ya halaiki ambayo yamekuwa yakiendelea kwa zaidi ya miezi kumi na tano, yanayofanywa na umbile halifu la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza, ambayo yamesababisha kuuawa shahidi na kujeruhiwa kwa Waislamu zaidi ya 170,000, wanaume na wanawake hadi sasa, Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Uturuki iliandaa amali kubwa kote nchini Uturuki chini ya Kichwa: “Usiisahau Gaza wala Usikubali Kusahauliwa Kwake!”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia: Matembezi ya Ukombozi: “Na Saidianeni katika Wema na UchaMungu wala Msisaidiane katika Uovu na Uadui”

Matembezi ya 65 yalianzia mbele ya Msikiti wa Al-Fath katika mji mkuu wa Tunis, baada ya swala ya Ijumaa, mnamo tarehe 3 Januari 2025 yalioandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia kuwanusurur watu wa Palestina na Al-Aqsa iliyo mateka, na kichwa chake kilikuwa “Na Saidianeni katika Wema na UchaMungu wala Msisaidiane katika Uovu na Uadui!”

Soma zaidi...

Hotuba Inayohusu Bendera za Rayah na Liwaa za Mtume (saw) Ilipambwa kwa Takbira na Machozi katika Soko Kuu la Port Sudan

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba yake ya kisiasa ya kila wiki, iliyokuwa na kichwa: “Je, Mtume (saw) alikuwa na bendera na Rayah?”, mnamo Jumatatu tarehe 28 Jumada al-Akhirah 1446 H sawia na 30/12/2024 M. Ustadh Muhammad Jami’ (Abu Ayman), Msaidizi wa Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan, alizungumza akisisitiza kuwa bendera ya Liwaa na Rayah katika Uislamu ni suala la dini, itikadi, mfumo na nembo ya Uislamu. Mtume (saw), ana benera (Liwaa) nyeupe kama bendera ya amiri jeshi, na bendera (Rayah) nyeusi kwa makamanda wa majeshi na vikosi, na inaitwa Uqab, zimeandikwa juu yazo “La Ilaha illa Allah Muhammad Rasulullah”.

Soma zaidi...

Hotuba ya Kisiasa mjini Port Sudan Haki ya Kisheria ya Waislamu katika Dhahabu, Petroli, na Rasilimali Nyenginezo

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan ilitoa hotuba ya kisiasa mbele ya Klabu ya Al-Shabiba katika Soko Kuu la Port Sudan, mnamo siku ya Jumatatu tarehe 7 Jumada al-Akhirah 1446 H, sawia na 9/12/2024 M, yenye kichwa: “Haki ya Kisheia ya Waislamu katika dhahabu, petroli na rasilimali nyenginezo”, ambapo Ustadh Ahmed Abkar, wakili, mjumbe wa baraza la Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan alizungumza, ambapo ilifafanua mali ya umma kuwa ni vitu vilivyoainishwa na sheria kwa ajili ya jamii, vinavyoshirikiwa kati yao, na kukatazwa kumilikiwa na mtu binafsi peke yake.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Ripoti ya Jukwaa la Masuala ya Ummah la Kila Mwezi: Wingi wa Majeshi na Wanamgambo ni Ishara ya Kuangamia kwa Dola, kwa hivyo ni ipi Njia ya Kutokea?

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir/Wilayah ya Sudan ilifanya Jukwaa la Kila Mwezi la Masuala ya Ummah, mnamo siku ya Jumamosi, tarehe 5 Jumada Al-Akhir 1446 H sawia na tarehe 7 Disemba 2024 M lenye kichwa: “Wingi wa Majeshi na Wanamgambo ni Ishara ya Kuangamia kwa Dola, kwa hivyo ni ipi Njia ya Kutokea?”

Soma zaidi...

Waziri wa Masuala ya Kidini na Wakfu awa Mgeni wa Hizb ut Tahrir

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan ukiongozwa na Ustadh Nasser Ridha (Abu Ridha), Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan, na pamoja naye Ustadh Ibrahim Othman (Abu Khalil), Msemaji Rasmi wa Hizb utTahrir katika Wilayah ya Sudan, na msaidizi wake, Ustadh Muhammad Jameh (Abu Ayman) ulimpokea Ndugu Dkt. Omar Bakhit Muhammad Adam, Waziri wa Masuala ya Kidini na Wakfu wa Kifederali katika afisi ya Hizb mjini Port Sudan, jana, Jumamosi, 21 Jumada al-Awwal 1446 H sawia na 23/11/2024 M.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Indonesia: Amali kubwa ya Khilafah na Jihad Kuikomboa Palestina na Gaza!

Kwa mnasaba wa kupita mwaka mmoja wa mauaji ya kikatili yanayoendelea (mauaji ya halaiki) yanayofanywa na umbile nyakuzi la Kiyahudi dhidi ya Waislamu wasio na ulinzi katika Ukanda wa Gaza, ambayo yamepelekea kuuawa shahidi na kujeruhiwa Waislamu zaidi ya 160,000 wanaume na wanawake hadi sasa, Hizb ut Tahrir / Indonesia iliandaa amali kubwa kwa anwani “Kukomesha mauaji ya halaiki nchini Palestina kunaweza tu kutekelezwa kwa kusimamisha Khilafah na kuhamasisha majeshi ya Kiislamu.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu