Alhamisi, 24 Rabi' al-thani 1447 | 2025/10/16
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kadri Wakati Unavyosonga Mbele, Thaqafa ya Kimagharibi Unarudi Nyuma

Mnamo tarehe 9 Oktoba, Gazeti la ‘the Guardian’ liliripoti kwamba mkuu wa shirika la kutoa misaada la Waislamu wa Uingereza Shaista Gohir, alikuwa na 'wasiwasi mkubwa' huku uhalifu wa chuki dhidi ya Uislamu ukiongezeka kwa theluthi moja kulingana na takwimu za hivi punde za serikali. Alisisitiza kuwa hata takwimu hizi zinazosumbua pengine ni ‘sio halisi’ kwani matukio mengi hayaripotiwi.

Soma zaidi...

Kuunganisha Fikra na Wabebaji Wake Ndio Njia ya Mabadiliko ya Kweli

Ni wazi, kwa wale wanaofanya kazi kwa ikhlasi kwa ajili ya kuhuisha Umma wa Kiislamu kupitia Uislamu, kile ambacho hali ya Ummah imefikia, kushambuliwa na mataifa mengine kama mwindaji anapolenga kwenye mawindo yake. Vile vile, ni dhahiri kwa wachunguzi jinsi Ummah unavyoelewa kwa uwazi uhalisia wake na kutambua sababu za mateso na maumivu yake. Kinachojulikana kwa Ummah kwa kiasi kikubwa kimefungika kwa makafiri wakoloni, watawala vibaraka, na tawala zilizowekwa na dola hizi za kikoloni juu ya shingo za Ummah ili kuukandamiza, kupora rasilimali zake, na kuuzuia kujikomboa kutoka kwa mshiko wa wakoloni kwa kusimamisha Khilafah kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Ujumbe kwa Watu Wetu mjini Gaza

Enyi watu wa Gaza: nyinyi leo mmesimama katika msimamo wa Mitume (as) na watu wema, mkisimama kidete kwa ajili ya haki dhidi ya dhulma. Kila dhiki, kila jeraha, kila Shahidi ni riziki katika mizani yenu ya mema, na kunyanyua daraja yenu. Ukuruba wa Mwenyezi Mungu uko pamoja nanyi, na ushindi wake uko karibu, basi subirini na muwe thabiti, na furahieni kwa yale aliyoyaahidi Mwenyezi Mungu (swt) ya bustani na daraja, na heshima ya dunia ambayo hupatikana kwa uthabiti na kujitolea mhanga.

Soma zaidi...

Kilio kwa Wabebaji Dawah “Mulikuwa wapi Muda wote huu?!”

Katika ghururi ya maisha na kutojali kwa jamii, neno moja pekee linabaki kuwa na uwezo wa kutikisa milima, kuchochea dhamiri, na kuamsha ari ya uwajibikaji katika nyoyo za Umma wa Uislamu. Ni neno lililotoka katika vinywa vya wale ambao miili yao ilichakaa kwa mateso na ambao fremu zao zilisagwa kwa dhulma ndani ya magereza ya madhalimu: “Mulikuwa wapi muda wote huu?!” Ilisemwa na mmoja wa wale walioachiliwa huru kutoka magereza ya mtoro Bashar al-Assad, wale walioonja majanga na ambao miaka yao ilizimwa gerezani; alipokutana na baadhi ya watu waliokuwa wameachiliwa huru, hakuuliza kuhusu idadi ya miaka gerezani, badala yake alipiga kelele usoni mwake: “Mulikuwa wapi, mulikuwa wapi muda wote huu? Kwa nini hamkutuachilia huru wakati tulipokuwa tunazikwa tukiwa hai?”

Soma zaidi...

Sudan: Mfano Mwengine wa Utaifa Uliofeli

Tangu 1945 kumekuwa na angalau nchi mpya 34 ambazo zimetambuliwa na Umoja wa Mataifa. Hili lilitokana na wimbi la utaifa ambalo lilienea kote ulimwenguni kwa miongo kadhaa tangu katikati ya miaka ya 1900. Mipaka ya kindoto ilichorwa ili kutoa uhuru kwa makundi mbalimbali na haki ya kutawala, kwani nchi kama vile Sudan iliyoungana hapo awali zilitumbukia ndani ya mizozo na machafuko.

Soma zaidi...

Khilafah kwa Njia ya Utume: Uadilifu na Rehma kwa Walimwengu

Uislamu ni dini ya haki ya Mwenyezi Mungu, ujumbe wa mwisho wa wahyi wa Mwenyezi Mungu na haki pekee ya kweli. Sheria na itikadi zengine zote duniani leo ni ya batili na potofu. Dini hii imekamilika katika sheria zake, inadhamini uadilifu kamilifu, rehma kamilifu, uongofu kamili, heshima kamilifu, na utumwa kamili kwa Mwenyezi Mungu, kwa sababu inatoka kwa Mwenyezi Mungu peke yake.

Soma zaidi...

Kwa Uislamu, Watu wa Sudan Wanayeyushwa ndani ya Chungu Kimoja, na Wanaishi Maisha yenye Staha na Haki Chini ya Dola Yake

Idadi ya watu wa Sudan inakadiriwa kufikia milioni 49.4, kulingana na Shirika la Umoja wa Mataifa la Idadi ya Watu (UNFPA) mwaka 2024. Asilimia tisini na sita ya wakaazi wote ni Waislamu, huku jamii ndogo ya Wakristo na watu binafsi wakifuata dini za kipagani. Jamii ya Wasudan inaundwa na makabila ya asili ya Waarabu, Waafrika, na Wanubi, yakiwakilisha zaidi ya makabila 500. Waarabu wanaunda kabila kuu, linalojumuisha 70% ya idadi ya watu, pamoja na makabila mengine, yakiwemo Beja, Nuba, Fulani, Geberti, Fur, Masalit, na mengineyo.

Soma zaidi...

Khilafah pekee ndio inayojali Maslahi ya Watu na ndio Mlinzi wa Haki na Mahitaji yao

Hali mbaya ambayo Sudan imefikia kufuatia vita vya kikatili vilivyoanza miaka miwili iliyopita kati ya vikosi vya jeshi na Vikosi vya Msaada wa Haraka sio siri. La kusikitisha, watu wasio na hatia wa Sudan wamelipia, na wanaendelea kulipia, gharama ya mzozo huu mbaya wa kimataifa unaoendeshwa na silaha za ndani kwa lengo la kuichana nchi na kulinda maslahi ya Amerika, Ulaya, na wengineo!!

Soma zaidi...

Hakuna Wokovu kwa Watu wetu nchini Sudan Wala Amani au Usalama isipokuwa chini ya Mfumo wa Uislamu

Katika yote historia, wingi wa makabila nchini Sudan kamwe haukuwa sababu ya mizozo na vita. Bali, kilichosababisha haya ni mapambano makali ya kisiasa na kijeshi baina ya dola za kikoloni na vibaraka wao, ambayo yaliharibu mazao na vizazi, hasa baada ya wao kuigawanya nchi na kupanda mbegu za fitina na mapigano ya kikabila na kimapendeleo, sawa kabisa na yale yanayotokea leo na kwa usahihi kabisa kama ilivyotokea katika siku za mwanzo za Ujahiliya.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu