Mstari Mwekundu wa Unafiki: Jinsi Mauaji ya Halaiki mjini Gaza, Yanavyofichua Nyuso
- Imepeperushwa katika Uchambuzi
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Mnamo Jumamosi, tarehe 17 Mei 2025, kitovu cha kisiasa cha Uholanzi kiligeuka kuwa chekundu. Maelfu ya watu walijiunga na maandamano jijini The Hague, ambapo mstari mwekundu wa ishara ulichorwa - mstari unaoashiria mpaka wa maadili wa kile ambacho bado kingali kinaweza kutetewa. Kichocheo hakikuwa tu ushiriki wa ‘Israel’ katika Shindano la Nyimbo la Eurovision, bali zaidi ya yote ni kuongezeka kwa hasira juu ya baa la njaa mjini Gaza na kutochukua hatua kwa aibu kwa serikali za Magharibi.