Jumamosi, 23 Sha'aban 1446 | 2025/02/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Je, Ugaidi ni Quran na Vitabu, Enyi Mliofilisika

Tovuti ya Russia Today ilichapisha ripoti ya habari mnamo tarehe 5/2/2025 ikisema kwamba "Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilisambaratisha seli ya magaidi yenye mafungamano na Hizb ut Tahrir katika Rasi ya Crimea na kuwakamata watu watano waliokuwa wakisajili wafuasi wa Hizb, ambayo imepigwa marufuku nchini Urusi." Ripoti hiyo ilijumuisha video inayoonyesha operesheni ya ukamataji na uvamizi wa nyumba, ambapo ilionekana wazi kwamba kile ambacho idara ya usalama ya Urusi ilichukua kutoka kwa nyumba za Mashababu ni nakala za Al-Quran Al-Kareem, vitabu, na vijitabu vya kisiasa na kifikra vya Kiislamu - machapisho maarufu ya Hizb ut Tahrir kwa jina pamoja na maalumati yaliyomo.

Soma zaidi...

Usasa wa Kiislamu (الحداثة الإسلامية): Shambulizi kwa Sunnah ya Mtume

Usasa wa Kiislamu (الحداثة الإسلامية) unakusudia fikra inayotaka kutafsiri upya Uislamu ili kuwiana na maadili na miundo ya mfumo wa kilimwengu wa kiliberali wa Kimagharibi. Ikiibuka katika karne ya 19, wimbi hili la mageuzi lilisukumwa na watu mashuhuri kama vile Jamal ud Din Afghani, Muhammad Abduh, Rashid Rida, na Syed Ahmed Khan. Juhudi zao zililenga kufanya maridhiano ya Uislamu na mifumo ya kisasa ya kisiasa, kijamii na kiuchumi. Ufafanuzi huu upya, hata hivyo, mara nyingi ulihusisha upotoshaji wa kanuni za Kiislamu ili kuendana na desturi zinazobadilika za ulimwengu wa kisasa, ikiwa ni pamoja na fahamu za Kimagharibi kama vile utaifa, urasilimali, sheria za binadamu, haki za binadamu, usawa wa kijinsia, na maelewano ya dini mbalimbali.

Soma zaidi...

Ni ipi Hatua Inayofuata?

Tangu kuvunjwa kwa Khilafah, tunaona kwamba siku baada ya siku Ummah wetu unadhalilika zaidi na zaidi. Kuanzia vita dhidi ya nyumba ya familia, hadi mabomu yanayoangushwa, na hadi watawala wanaotuma vikosi vyetu vya majeshi kwenye matukio kama vile Phoenix Express. Haya ndiyo ambayo sisi kama Ummah tunayaona na hatuwezi kufahamu jinsi tulivyofika mbali hivi sana na pale tulipowahi kuwa mahali pa heshima na adhama. Tulikuwa Ummah ambao ulikuwa juu ya dunia, ambao wanadamu walitamani kuwa sehemu yake kuanzia kwa mfumo wetu wa elimu hadi mfumo wetu halisi wa mahakama. Tulikuwa na haki na uadilifu tofauti na mfumo mwingine wowote duniani, unaoleta amani na utulivu kwa wanadamu wote.

Soma zaidi...

Uhadaifu wa Utaifa

Baada ya wakoloni kuugawanya ulimwengu wa Kiislamu, walifanya kazi kuelekea kubadilisha mfumo wake wa utawala. Mifumo ya bunge ilianzishwa na maafisa wa kikoloni wangejihusisha na raia wao iwapo tu wangekubali kujipanga katika muundo wa vyama vya kidemokrasia. Walioletwa madarakani na wakoloni ni wale waliokubali sheria na kanuni zao. Kuibuka kwa dola za kitaifa katika ulimwengu wa Kiislamu kwa hiyo kunahusishwa kwa namna isiyoweza kutenganishwa na historia ya ukoloni na kulazimishwa na dola za Ulaya zilizotaka kuona ulimwengu wa Kiislamu ukigawanyika.

Soma zaidi...

Gaza: Mwaka Mmoja ndani ya Mauaji ya Halaiki, Na Hakuna Msaada kutoka kwa Vikaragosi vya Magharibi

Ni dhahiri kwamba mwaka mmoja baada ya kuanza kwa mauaji ya halaiki, viongozi wa Waislamu hawajaweza kukata kamba wanazoshikilia mabwana zao. Kwa kufanya hivyo wanauthibitishia Ummah kwamba wao hawasimami pamoja na Waislamu. Wanasimama na pamoja uvamizi, na dola za Magharibi. Kwa hiyo ni wakati wa Ummah kuamka kama kizazi kipya. Ni wakati wa Umma kuungana chini ya Dini moja, bendera moja, kiongozi mmoja. Ni wakati wa sisi kuacha kuomba amani na usitishaji vita na kuanza kuitisha suluhisho halisi.

Soma zaidi...

Kufahamu Uke na Uume katika Uislamu

Mtazamo wa Kimagharibi kuhusu jinsia unasalia kuwa umejaa ukinzani na unafiki, hasa unapotazamwa kupitia jicho la matukio ya hivi majuzi kama vile sintofahamu inayomhusisha bondia wa Algeria kwenye Michezo ya Olimpiki ya Paris. Bondia huyo ambaye ni mwanamke kibaiolojia, amekosolewa na baadhi ya vyombo vya habari vya nchi za Magharibi na mamlaka za michezo kwa madai ya kumiliki viwango vya juu vya homoni za “kiume” na kupendekeza kuwa asiruhusiwe kushindana na wanawake wengine.

Soma zaidi...

Marekani Inatafuta Ushindi Madhubuti nchini Afghanistan

Serikali ya Marekani, kupitia taasisi za kimataifa, hasa Umoja wa Mataifa, inalenga kupata ushindi madhubuti. Ni ushindi ambao haikuweza kuupata, licha ya zaidi ya miaka ishirini ya vita dhidi ya Uislamu na Mujahidina nchini Afghanistan. Utafutaji ushindi huu ulianza pale Marekani ilipoiruhusu Qatar kuwa mwenyeji wa vuguvugu la Taliban, na kufungua afisi kwa ajili ya vuguvugu hilo huko Doha mwaka 2013. Kupitia afisi hii, Marekani ilijihusisha kisiasa na harakati hiyo, na kusababisha duru kadhaa za mazungumzo yaliyohusisha Marekani na waamuzi, ukiwemo ujasusi wa Pakistan.

Soma zaidi...

Kwa Mujibu wa Uislamu, Hairuhusiwi Kugombea, au Kupiga Kura kwenye Chaguzi za Kidemokrasia

Ushiriki wa Muislamu katika Demokrasia ni jambo lenye kuwashughulisha watawala, wanasiasa, wasomi na watungaji sera. Hii ni ima Waislamu wakiwa katika Ulimwengu wa Kiislamu, au wakiishi ughaibuni katika nchi za Magharibi. Hivyo kuna mjadala kuhusu ushiriki wa Muislamu katika Demokrasia nchini Australia, Uingereza na Amerika, kama ulivyo mjadala kuhusu ushiriki wa Waislamu katika uchaguzi nchini Uturuki, Pakistan na Misri.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu