Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 598
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kwa kuzingatia mamlaka ya Lebanon kushiriki katika mazungumzo ya moja kwa moja ambayo hakika yatapelekea katika amani na uhalalishaji mahusiano na umbile nyakuzi na halifu la Kiyahudi, na kama sehemu ya kampeni ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon kuwatembelea wanasiasa, mamufti, wasomi, nyanja ya kisiasa, na watu mashuhuri, wajumbe kutoka Kamati Kuu ya Mawasiliano na kamati za shughuli za kikanda walifanya ziara. Hizi zilianza katika mji wa Sidon kusini mwa Lebanon kwa ziara ya Mbunge Dkt. Osama Saad, Katibu Mkuu wa Shirika Maarufu la Wananasseristi, na ziara ya Mufti wa Sidon na wilaya zake, Sheikh Salim Sousan. Hii ilifuatiwa na ziara katika mji mkuu, Beirut, kwa Naibu Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Kiislamu la Shia, msomi Sheikh Ali Al-Khatib.
Mnamo Jumatano tarehe 12 Dhu al-Qa‘dah 1447 H sawia na tarehe 28 Aprili 2026 M, dada mwema, mbebaji da’wah aliyefanya kazi kwa ajili ya kusimamisha Khilafah Rashidah ya pili kwa njia ya Utume, mwanachama katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen, Dada Lamya bint Bashar alifariki.
Je, ni nini maana ya kauli za Trump zenye kusitasita—kutoa Iran masaa 48, kisha siku 5, kisha siku 10—na pendekezo lake la mpango wenye nukta 15? Namna gani ujanja wa kauli, nyingi kutoka kwa Trump na chache kutoka kwa Iran, na tangazo la televisheni ya Iran kukataa pendekezo la Trump? Matokeo ya hayo yote ni nini?
Mnamo Jumamosi 02 Mei 2026 M, Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia iliandaa kongamano la kila mwaka la Khilafah katika ukumbi wa mikutano na makongamano ulio katika makutano ya Sakiet Ariana katika mji mkuu wa Tunis, lenye kichwa: “Kufeli kwa Dola ya Kisasa na Kutoepukika kwa Dola ya Khilafah”
Mnamo Ijumaa, 17 Aprili 2026, matembezi yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia, yalianza kutoka Msikiti wa Al-Fath jijini Tunis, mji mkuu, baada ya swala ya Ijumaa. Matembezi hayo yalikuwa na kichwa: “Ujanja wa Kijeshi wa Marekani kwenye Ardhi ya Tunisia ni Uhalifu.”
Hizb ut Tahrir/Wilayah Sudan iliongeza shughuli zake za umma wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, ikihimiza jamii ya Waislamu kufanya kazi nayo ili kuanzisha jengo kuu la Uislamu: Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, ambayo ilivunjwa miaka 105 iliyopita. Iliendesha hotuba za kisiasa, mihadhara, na visimamo katika viwanja vya misikiti, masoko, na maeneo mengine ya umma, pamoja na programu zake za kawaida katika afisi zake katika miji mbalimbali ya Sudan.