Alhamisi, 09 Jumada al-awwal 1447 | 2025/10/30
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Lebanon Wamemtembelea Mheshimiwa Mbunge Dkt Osama Saad

Kwa kuzingatia shambulizi la Marekani dhidi ya Lebanon na kanda hii kupitia uhalalishaji mahusiano na kujisalimisha, na juhudi za Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Lebanon kuzuia shambulizi hili, ujumbe kutoka hizb, ukiwakilishwa na wanachama wa Kamati Kuu ya Mawasiliano na Kamati ya Amali katika Eneo la Kusini, ulimtembelea Mheshimiwa Mbunge Dkt. Osama Saad afisini kwake Sidon mnamo Jumatatu, 27/10/2025.

Soma zaidi...

Kipindi cha “Nampenda Muhammad” nchini India Chafichua Udhalilifu wa BJP Uliofinikwa na Imani ya Wengi

Kipindi cha “Nampenda Muhammad” kilichozuka kote Uttar Pradesh Septemba hii kimefichua tena utata wa kisaikolojia na kisiasa unaoendesha Chama tawala cha Bharatiya Janata (BJP) cha India. Kile kilichoonekana, juujuu, kuwa mzozo wa sheria na utaratibu kuhusu mabango ya kidini na machapisho ya mitandao ya kijamii, kwa kweli, kinaakisi wasiwasi mkubwa zaidi – udhalilifu unaojificha nyuma ya onyesho la imani ya wengi.

Soma zaidi...

Tafakari Muhimu Kuhusu Taarifa ya Chama cha Maimamu nchini Uholanzi

Taarifa ya Chama cha Maimamu nchini Uholanzi (VIN) inadai kwamba ushiriki wa kisiasa ndani ya jamii za Ulaya ni “njia inayoruhusiwa na halali,” na kwamba ushiriki unaweza hata wa kupendekezwa au wa lazima kulingana na hali. Msimamo huu unahitaji kuzingatiwa kwa makini, kwani unaegemezwa juu makisio ambayo hayaakisi vya kutosha uhalisia wa mfumo wa kisekula.

Soma zaidi...

“Amali” kama Pazia la Ukaliaji wa Kimabavu

Yale yanayoitwa makubaliano kati ya dola vamizi “Israel” na Hamas, yaliyopangwa na Washington, yanawasilishwa katika vyombo vya habari vya Magharibi na kwa masikitiko pia katika sehemu za ulimwengu wa Kiislamu kama hatua kuelekea amani. Kiulisia, si kitu chengine ila ni marudio ya mtindo wa zamani: mradi wa kikoloni “Israel” unaimarishwa na kulindwa zaidi, huku jinai zake zikifinikwa na vazi la “amani.”

Soma zaidi...

Maafa Mawili Yanaukumba Ummah wa Kiislamu – Watawala Wafisadi na Mfumo Fisadi – Yote Lazima Yabadilishwe kwa Wakati Mmoja

Mnamo 26 Julai 2025, jiji la Kuala Lumpur lilishuhudia maandamano ya ajabu ya umma — maandamano makubwa ya kudai kujiuzulu kwa Waziri Mkuu wa Malaysia, Datuk Seri Anwar Ibrahim. Mkutano huu ulionyesha hasira kubwa na kuchanganyikiwa kwa watu kuelekea uongozi ambao haujashindwa tu kutekeleza ahadi zake za mageuzi, lakini pia umezidisha ugumu wa watu kupitia nyongeza za kodi, ongezeko la ushuru wa umeme, na kupanda kwa bei za bidhaa muhimu.

Soma zaidi...

Kumwalika Adui wa Mwenyezi Mungu, Mtume Wake, na Waumini Ni Sawa na Kualika Ghadhabu ya Mwenyezi Mungu na Msiba: Mche Mwenyezi Mungu, Ewe Waziri Mkuu wa Malaysia!

Hizb ut Tahrir / Malaysia inalaani vikali mwaliko uliotolewa na Waziri Mkuu wa Malaysia, Dato’ Seri Anwar Ibrahim, kwa Rais wa Marekani, Donald Trump — ambaye mikono yake imejaa damu ya Waislamu wa Gaza — kuja nchini Malaysia kuhudhuria Mkutano wa 47 wa ASEAN jijini Kuala Lumpur. Mwaliko huu si tu ishara ya aibu ya kidiplomasia isiyo na msimamo wa kimaadili; ni aibu kubwa kwa hadhi ya Ummah huu, usaliti unaojeruhi dhamiri ya kila Muislamu ambaye bado ana heshima karibu na moyo wake, hasa zaidi watu wa Palestina.

Soma zaidi...

Watawala wa Pakistan, Watu wa Trump, Wawateka nyara Mashababu wa Hizb ut Tahrir ili Kuhakikisha Kujisalimisha kwa Palestina

“Jenerali kipenzi cha Trump,” Asim Munir, amejibu kwa udhalimu kampeni yenye nguvu ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Pakistan, ambayo kwayo inataka uhamasishwaji wa haraka wa Vikosi vya Jeshi la Pakistan ili kuikomboa Palestina. Majambazi wa Asim Munir wamewateka nyara matetezi watano, kutoka Lahore, Karachi na Peshawar, na mahali walipo hapajulikani. Udhalimu wa Asim Munir unatarajiwa. Asim Munir hawezi kutenda, sembuse kufikiria, nje ya maagizo ya Trump katika suala lolote, iwe kuhusu Gaza, Kashmir, Afghanistan au rasilimali kubwa za madini za Pakistan.

Soma zaidi...

“Vita vya Burqa” vya Wananchi Ni Mwangwi wa Kisasa wa Ukoloni wa Ulaya, Uliotumika Kupuuza Mauaji ya Halaiki mjini Gaza na Kumvua Mwanamke wa Kiislamu Kitambulisho Chake cha Kiislamu

Vita vya hivi karibuni vya watu wengi kutoka kwa vyama vya kidemokrasia na serikali za mrengo wa kulia vinavyotaka kupigwa marufuku kwa burqa sasa vinajumuisha Australia, Italia na Ureno. Mataifa haya ni sehemu ya kundi kubwa la nchi adui za Ulaya ambazo tayari zimepiga marufuku burqa. Ufaransa, Ubelgiji, Denmark, na Uswizi zinatekeleza marufuku ya kitaifa katika maeneo yote ya umma, huku Uholanzi na Ujerumani, zikiwa na marufuku ya sehemu inayolenga muktadha maalum kama vile shule au afisi za serikali. Nchini Uingereza, mjadala unalenga wafanyikazi, ambapo chama cha mrengo wa kulia cha Mageuzi cha Uingereza kinasema kwamba burqa kama hizo zinazuia uoanishwaji, mawasiliano, na usalama, zikiziita “nembo za mgawanyiko.”

Soma zaidi...

Watawala wa Pakistan wanaogopa mwamko wa Kiislamu unaoongezeka miongoni mwa Waislamu wa Pakistan na, kupitia utekelezaji wa Mpango wa Kitaifa wa Utendakazi, wanajaribu—bila mafanikio—kuusimamisha kwa kuigeuza Pakistan kuwa “dola ngumu zaidi.”

Mwenendo mkali na wa kikatili wa watawala dhidi ya mkutano wa TLP umesababisha mawimbi ya wasiwasi katika duara za kidini za Pakistan na kumshangaza kila Muislamu mwenye ufahamu. Hata hivyo, mbinu hii ya kiimla ya watawala wa Pakistan si kitendo cha pekee au kisicho cha kawaida; bali ni sehemu ya msururu wa hatua mfululizo ambazo watawala wamechukua katika siku za hivi karibuni, hatua zilizozidi wakati watawala wa Pakistan walipokubali kutekeleza mpango wa Trump pamoja na watawala wa nchi za Kiarabu na zengine za Kiislamu, mpango ambao lengo lake ni kulinda uwepo wa Mayahudi kutokana na upinzani wa Waislamu wa Palestina.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Indonesia: Matembezi Makubwa ya Kukumbusha Ulimwengu “Palestina ingali chini ya Uvamizi”

Maelfu ya Waislamu katika miji mbalimbali ya Indonesia walifanya matembezi yanayounga mkono Palestina mnamo Oktoba 18 na 19, 2025, chini ya kauli mbiu “Palestinaingali chini ya Uvamizi.” Huko Bandung, zaidi ya waandamanaji 15,000 walikusanyika mbele ya jengo la Gedung Sati, wakinyanyua bendera za Rayah zenye tamko la Tawhid na mabango yenye kauli mbiu kama vile “Tumeni majeshi ya Kiislamu, yakomboe Palestina!”, na “Suluhisho la mwisho kwa Palestina ni kupitia jihad na Khilafah,” na “Palestina itakombolewa kupitia Khilafah na Jihad.”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu