Ulaya Inaendelea Kuunga Mkono Mauaji ya Halaiki mjini Gaza
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Licha ya kauli mbiu tupu kuhusu kuitambua dola ya Palestina, Ulaya inaendelea kusafirisha silaha kwa umbile hilo la Kizayuni. Habari zilizovuja zilizopatikana na gazeti la Denmark zinafichua kuwa hivi majuzi mwezi wa Agosti, serikali ya Denmark ilituma vifaa vya silaha kwa ndege zilizotumiwa kuua watoto mjini Gaza.