Jumanne, 10 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/02
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Taqli Watoa Wito Mkali kwa Waislamu Kutibua Mpango wa Marekani wa Kutenganisha Darfur

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/ Wilayah Sudan ya kukwamisha mpango wa kuisambaratisha Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kuzingatia umoja wa Ummah kama suala nyeti, suala la uhai na kifo, wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi' al-Awwal 1447 H sawia na 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Sheikh Yahya kituo cha kuhifadhi Quran. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa matabaka yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, wanazuoni, maafisa na askari na wengineo, wakiwahimiza kutimiza wajibu wao wa kidini ili kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Kinachoitwa “Tamasha za Hisia” (Zambo) jijini Tripoli ni Jaribio la Kulionyesha Jiji lisilo na Hisia zake kwa Ummah Kwa hivyo Zisusieni na Komesheni utoaji Leseni Kwazo!

Kwa ukaidi wa wazi wa hisia za Umma na maumivu yake, na kwa ukaidi wa wazi wa Tripoli, jiji la elimu na wanazuoni, na licha ya kutolewa kwa tamko kutoka kwa Kamati ya Utunzaji wa Familia katika Dar al-Fatwa jijini Tripoli na Kaskazini kuonya juu ya njia hii hatari kwa jamii, ambapo ilikuja katika taarifa: “Kamati pia inatahadharisha juu ya hatari ya tamasha, sherehe, filamu, na mipango ambayo imejitokeza hivi karibuni katika jiji letu na ambayo yanaathiri maadili na akhlaki, na ambayo hutumiwa kupitisha ujumbe potovu chini ya kauli mbiu za kisanii au kithaqafa, katika jiji linalojulikana katika historia yake kama jiji la elimu na wanazuoni, na kama ngome ya maadili ya kweli na kitambulisho kinachounganisha. Kamati inasisitiza kwamba kuilinda jamii kutokana na hatari ni jukumu tunaloshirikiana pamoja: linaanza na familia na jamaa, kwenda hadi kwa walimu, na wanazuoni, na pia linajumuisha asasi za kiraia, manispaa, na wanasiasa, kufikia hadi kwa watoa maamuzi katika ngazi ya serikali…”

Soma zaidi...

Msamaha Mbele ya Mola Wetu, na Pole kwa Waliojeruhiwa Gaza Tripoli ash-Sham Yapaza Sauti Yake Dhidi ya Sherehe za Kucheza juu ya Majeraha ya Umma!

Hizb ut Tahrir katika Wilayah Lebanon imetoa wito kwa Mashababu (wanachama) wake kushiriki katika kikao kilichopangwa kwa uratibu na wanaharakati na watu mashuhuri katika mji wa Tripoli, Jumamosi hii jioni saa sita kamili mbele ya Maonyesho ya Kimataifa ya Tripoli, kwa ajili ya kukemea tamasha la densi (Zambo) na kuimba katika mji wa Tripoli, mji wa elimu na wanazuoni, kama udhuru mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kuhusiana na makosa yanayofanywa mjini Tripoli na ambayo hayaonyeshi kitambulisho chake, katika wakati ambapo umbile halifu la Kiyahudi linaendesha vita vikali dhidi ya Waislamu wa Palestina kwa jumla na hasa Gaza, na uvamizi na jinai zake zimeenea hadi Lebanon na Syria, kwa kukalia kimabavu sehemu ya ardhi ya Kusini na ardhi ya Syria, na ndege zake hazijaondoka anga zake, zikipiga mabomu na kuangamiza bila kuzuiwa au mwenye kuwazuia!

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Wanamtembelea Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist mjini Al-Obeid

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Ustadh Al-Nazir Muhammad Hussein - Mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan - akifuatana na Ustadh Issam al-Din Abdul Qadir, walimtembelea Ustadh Khalid Hussein, Mkuu wa Chama cha Democratic Unionist, katika afisi yake katika mji wa Al-Obeid, mnamo Jumanne 3 Rabi’ al-Awwal sawia na tarehe 26 Agosti 2025 M, kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ili kutibua mpango wa kuitenganisha Darfur.

Soma zaidi...

Kuhuisha Uislamu: Njia Pekee ya Kuepuka Majanga

Mafuriko ya hivi majuzi nchini Pakistan yameharibu Khyber Pakhtunkhwa na Sindh, huku maeneo mengine yakipambana na barabara zilizojaa maji ambayo yamegeuza maisha ya kila siku kuwa hatari. Masaibu ya kupoteza maisha na riziki katika KPK yamewaacha watu na hofu. Kinachosumbua zaidi ni kukosekana kwa vifaa sahihi vya uokoaji – na kufanya wengi kuhoji uwezo wa serikali kujibu. Wafanyikazi wa uokoaji wanaachwa wakifanya kila kitu kwa mikono, na kwa mara nyingine tena, ni watu wa eneo hilo ambao, waliopata ukakamavu kwa miaka ya kupuuzwa, wanajua lazima wajitegemee wenyewe kwa sababu ima utakuja msaada mdogo hautakuja kabisa.

Soma zaidi...

Fahali Wanapopigana, Zinazoumia ni Nyasi “Sudan ni Mfano”

Sijapata katika historia msemo wenye ufasaha zaidi wa uovu wa ukoloni kuliko maneno ya Rabi ibn Amir, Mwenyezi Mungu amuwiye radhi, kwa kamanda wa Kifursi: “Sisi ni watu ambao Mwenyezi Mungu amewatuma kuwatoa wanadamu kutoka katika ibada ya waja wengine hadi kwenye kumwabudu Mola wa waja wote.” Ijapokuwa kauli hii ilitolewa ili kubainisha lengo la ujumbe mtukufu wa Uislamu, unaowakirimu watu kutokana na kumwabudu kwao Mwenyezi Mungu, na kuhifadhi maisha yao, mali zao na heshima zao, hii wakati fulani hujidhihirisha kama kauli iliyo kinyume chake. Rehema ya Uislamu na uhuru unaowadhaminia watu unakinzana na utumwa wa watu na mataifa kwenye ukoloni, ambao unawaona kuwa ni mashini tu za kuzalisha dhahabu na pesa.

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu