Kufuatia utekelezaji wa mashababu wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan wa visimamo vitatu katika maeneo tofauti tofauti katika jiji la Omdurman, asubuhi ya Jumatano iliyopita, 25 Rajab 1447 H, sambamba na 14/1/2026 M, ndani ya muundo wa kukumbusha tukio la kupita kwa miaka 105 tangu kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah mwezi Rajab 1342 H, vyombo vya usalama viliendelea kuwakamata wanachama watano wa Hizb: Al-Radi Muhammad Ibrahim, Fadlallah Ali Suleiman, Omar Al-Bashir, Hassan Fadl, na Mujahid Adam. Kisha waliachiliwa baada ya Magharibi siku ya Jumatano baada ya nambari zao za simu kuchukuliwa na baada ya kunyakua mabango ambayo Mashababu hao wa Hizb ut Tahrir walikuwa wamebeba katika visimamo hivyo vitatu. Kisha waliitwa mnamo alasiri ya Alhamisi, 15/1/2026, na wangali wako kizuizini hadi wakati wa kuandika taarifa hii!!