Jumatano, 11 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Ufuatiliaji Mkubwa wa Mkoloni Amerika juu ya kile kinachoitwa “Mageuzi” sio Chengine ila ni Jaribio la kupanua Udhibiti wake nchini Bangladesh

Balozi Mdogo wa Marekani jijini Dhaka, Tracy Ann Jacobson, alifanya mkutano na Profesa Ali Riaz, Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Kitaifa ya Maridhiano wiki iliyopita ili kuuliza kuhusu mipango ya mageuzi inayoendelea na maendeleo yake. Jacobson na manaibu wake wamekuwa wakifanya mfululizo wa mikutano na wawakilishi wa vyama vikuu vya kisiasa. Kama sehemu ya ushirikiano wa Marekani ‘kukuza demokrasia’ nchini Bangladesh, tunaona mikutano na taarifa za mara kwa mara kutoka kwa Ubalozi wa Marekani nchini Bangladesh na Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani zinazohimiza marekebisho katika utawala. Kusiwe na shaka kwamba msukumo wa Marekani wa kuleta mageuzi na kile kinachoitwa ‘uwajibikaji wa kidemokrasia’ haukusudiwi kheri ya watu wetu. Katika historia, mbeberu mamboleo Marekani imekuwa ikiunga mkono madikteta kwa maslahi yake huku ikitetea ‘demokrasia’ na ‘haki za binadamu’.

Soma zaidi...

Mbele ya Serikali za Khiyana, Msikiti wa Al-Aqsa Unabadilishwa Kuwa Mahali Patakatifu kwa Mayahudi!!

Mbele ya macho ya watawala wa Waislamu, Mayahudi wamekuwa wakivamia eneo la Msikiti wa Al-Aqsa, uvamizi baada ya uvamizi, ambao wa hivi karibuni ulikuwa wa jana, Jumapili, ukiongozwa na adui wa Mwenyezi Mungu, Ben-Gvir na idadi kadhaa ya Mayahudi wenye itikadi kali, katika uvamizi mkubwa zaidi kuwahi kutokea katika msikiti huo.

Soma zaidi...

Ni Wakati sasa wa Kugeuza Ukurasa wa Giza wa Oslo

Smotrich alitangaza kuangamia kwa mradi wa Dola ya Palestina kwa kuzinduliwa kwa mradi wa E1 au East One, ambao unachukuliwa kuwa utekelezaji wa kinachojulikana kama Mpango wa Jerusalem Kuu. Mpango huu unatenganisha Ukingo wa Magharibi wa Kaskazini kutoka Ukingo wa Magharibi wa Kusini, na, sambamba na hatua zilizochukuliwa na umbile la Kiyahudi uwanjani, unaunda viunga vilivyotengwa ndani yake ambavyo vinawazingira watu wa Ukingo wa Magharibi. Hili lilitanguliwa na kubomolewa kwa kambi kaskazini mwa Ukingo wa Magharibi na kuorodheshwa kwa UNRWA kama shirika lisilo halali, ili suala la wakimbizi libaki kuwa lisilo na umuhimu wowote.

Soma zaidi...

Amerika inaharakisha Mpango wake wa Kulitenganisha Eneo la Darfur Hakuna Suluhisho Isipokuwa kwa Kuufanya Umoja wa Dola kuwa Suala Nyeti

Tangu utawala wa Trump kuchukua faili ya Sudan baada ya kuchukua uongozi mnamo Januari 2025, imekuwa ikiongoza harakati za kijeshi na kisiasa nchini Sudan, ikishinikiza kujitenga kwa eneo la Darfur. Mnamo Jumatano, 26/3/2025, jeshi liliteka tena Khartoum. Al-Burhan alitangaza kutoka Kasri la Republican, “Khartoum iko huru na suala limekwisha.” Hatua za kijeshi ziliharakisha, na kuondoa Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) kutoka Sudan ya kati, ikijumuisha majimbo ya Al-Jazirah, Sennar, White Nile na Blue Nile.

Soma zaidi...

Umuhimu wa Kimkakati wa Eneo la Sudan

Aprili 15, 2025 ilitimiza miaka miwili tangu Sudan kukumbwa na vita vya maangamivu vya wenyewe kwa wenyewe, na kusababisha moja ya majanga makubwa zaidi ya kibinadamu duniani leo. Miaka miwili iliyopita mwezi Aprili, mapigano yalizuka kati ya Vikosi vya Wanajeshi wa Sudan (SAF) na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF), na kuwahamisha mamilioni ya watu, na kuiingiza nchi katika uhaba mkubwa wa chakula, na kuharibu huduma muhimu za afya na elimu. Licha ya maafa ya kibinadamu ambayo yametokea, vita vya Sudan kwa kiasi kikubwa vimeepukana na muanga wa kimataifa. Sudan ni vita iliyosahauliwa, haswa kwa ulimwengu wa Magharibi ambao unaweza kuzingatia Ukraine pekee. Je, ni mambo gani ya siasa za kijiografia ambayo yanaifanya Sudan kushawishika kuyapigania?

Soma zaidi...

Enyi Watu! Je, bado mungali na matumaini kwa Watawala na Wanasiasa Watepetevu (Ruwaibidha) wa Sasa?!

Baada ya kuanguka kwa dhalimu Hasina, watu walitarajia Profesa Yunus achukue hatua madhubuti za kukabiliana na udhibiti wa Marekani-Uingereza-India kwa kutumia ushawishi wake wa kimataifa. Angeweza kuunda mjadala huo na mazingira ya kisiasa nchini humo ambayo kwayo watu wangeweza kuunda suluhisho jipya la kisiasa ili kulinda maslahi ya Uislamu, maslahi ya watu na ubwana wa nchi katika Bangladesh mpya. Ijapokuwa idadi kubwa ya wakaazi wa nchi hii ni Waislamu, serikali ya mpito, kuuondoa Uislamu katika masuluhisho ya kisiasa, haijaondoa marufuku iliyowekwa na dhalimu Hasina kwa chama cha kisiasa cha Hizb ut Tahrir kwa kujisalimisha kwa Marekani-India. Pamoja na hayo, kupitia makongamano ya mtandaoni Hizb ut Tahrir imewasilisha muundo wa dola ya Kiislamu, njia ya kuasisi uchumi unaojitegemea na kuwa na jeshi thabiti kwa ajili ya kulinda ubwana wa nchi hii kwa kuzingatia katiba ya Kiislamu ili kutekeleza matumaini na matarajio ya wananchi wa Bangladesh mpya.

Soma zaidi...

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari mnamo Jumamosi, 22 Safar 1447 H sawia na 16/08/2025 M, yenye kichwa: “Wito kwa Watu wa Sudan... Ikamateni Darfur Ili Isiungane na Kusini”

Mnamo Jumamosi, 26/7/2025, Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vilitangaza kuundwa kwa serikali sambamba na serikali iliyopo nchini Sudan, katika mji mkuu wa Darfur Kusini (Nyala). Hatua hii ya RSF ni hatua ya juu katika kutenganisha eneo la Darfur, ambalo inalidhibiti, isipokuwa sehemu za mji wa El Fasher, ambao mzingiro wa kukandamiza umewekwa juu yake kwa zaidi ya mwaka mmoja, na kuanzisha mashambulizi mfululizo dhidi yake ili kuuangusha, ili eneo zima la Darfur liwe chini ya udhibiti wake.

Soma zaidi...

Iwapo Kuanguka kwa ‘Jamhuri’ Hakukupelekea Kusimamishwa kwa Khilafah, Ni lazima Kutumike kama Hatua ya Mpito kuelekea Khilafah Rashida

Kuporomoka kwa serikali ya Jamhuri nchini Afghanistan ni moja ya matukio muhimu zaidi kwa watu wa Afghanistan na Umma mpana wa Kiislamu katika karne ya 21. Serikali hii sio tu kwamba haikuwa na mizizi yoyote katika itikadi ya Kiislamu, bali ilikuwa ni zao la muundo wa ukoloni mamboleo - mfumo ulioagizwa kutoka nje uliojengwa ili kurasimisha ufisadi, utegemezi, na dhulma. Kuanguka kwake lilikuwa ni mwisho wa kimaumbile na usioepukika wa mfumo ambao, tangu kuanzishwa kwake, ulikuwa ngeni kwa kitambulisho cha Kiislamu na kupingana na maadili ya Uislamu.

Soma zaidi...

Ayman Safadi: “Yeyote ambaye ana badali ya Suluhisho la dola mbili, basi na aiwasilishe!” Hizb ut Tahrir imewasilisha na inaendelea kuwasilisha suluhisho halali na la kivitendo

Serikali ya Jordan ndio iliyowawekea watu wa Jordan na Umma wa Kiislamu suluhisho linaloendana na kuhifadhi usalama wa umbile katili la Kiyahudi. Hukuwa na maregeleo ya masuluhisho ya kadhia ya Palestina isipokuwa Marekani, rafiki wa serikali hii, mshirika wa umbile la Kiyahudi, mdhamini wake, mlinzi wake, na mshirika wake katika vita vya maangamizi na njaa dhidi ya watu wa Gaza.

Soma zaidi...

Kauli za Netanyahu kuhusu "Israel Kubwa" ni Tangazo la Vita ambalo linafuta Mikataba, na, kwa sababu hiyo, Majeshi Yanasonge, na Jambo jengine lolote lisokuwa hilo ni Usaliti

Huyu hapa mhalifu wa kivita Netanyahu anatangaza waziwazi na bila kufasiriwa kwa watawala waoga wa Kiarabu na wasemaji wao, akisema katika mahojiano na chaneli ya Kiebrania i24: “Mimi niko kwenye misheni ya vizazi na kwa jukumu la kihistoria na la kiroho, ninaamini kwa dhati ruwaza ya Israel Kubwa, ambayo ni pamoja na Palestina ya kihistoria na sehemu za Jordan na Misri.” Mhalifu Smotrich alikuwa amemtangulia kwa kauli zile zile na kunyakua sehemu za nchi za Kiarabu zinazoizunguka Palestina, ikiwemo Jordan. Katika muktadha huo huo, adui namba moja wa Uislamu na Waislamu, Rais Trump wa Marekani, alimpa idhini ya upanuzi wake akisema, “Israel ni sehemu ndogo sana ikilinganishwa na ukubwa wa ardhi hizo, na najiuliza ikiwa inaweza kupata ardhi zaidi kwa sababu kweli ni ndogo sana.”

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu