Makongamano Yenye Malengo ya Kufuta Kadhia ya Ardhi Iliyobarikiwa Yanafanyika Wakati Damu ya Watu wake Ikimalizwa
- Imepeperushwa katika Palestina
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Milipuko ya mabomu inateketeza miili ya watoto mjini Gaza, njaa inatafuna mabaki yao, mizinga inasaga saga uhai na nyumba za watu walio na msimamo thabiti, na ndege zinanyesheza lava zao kwenye hospitali na hema za waliohamishwa. Kutokana na hali ya uhalifu huu, kongamano lililokongamana jana usiku, 22 Septemba 2025, jijini New York, lililoitishwa na Ufaransa na Saudi Arabia, lilitaka kutambuliwa kwa “Dola ya Palestina”.