Uhamisho au Ukombozi, enyi Umma wa Kiislamu?
- Imepeperushwa katika Palestina
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Dhalimu wa Marekani, Trump, alisema katika mkutano na waandishi wa habari pamoja na mhalifu Netanyahu jioni ya Jumanne, 4 Februari 2025: "Marekani itachukua Ukanda wa Gaza, na tutafanya kazi nayo pia" Aliongeza, "Tutageuza Ukanda wa Gaza ulioharibiwa kuwa Riviera ya Mashariki ya Kati." Alizungumzia juu ya umiliki wake wa muda mrefu wa Gaza na alisisitiza taarifa yake ya awali kuhusu kuwahamisha watu wa Gaza, ambapo alisisitiza kutiishwa kwa watawala wa Misri na Jordan na wasaidizi wao, akisema: "Misri na Jordan zilisema hazitapokea wakaazi kutoka Gaza, na mimi nasema lazima watapokea." Hapo ndio watawala watiifu, wasaliti.