Jumamosi, 23 Sha'aban 1446 | 2025/02/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Watawala wa India Wanatumia Sheria ya (Kuzuia) Shughuli zisizo halali ya 1967 kupiga Vita Uislamu na Waislamu, wakimwemo Mashababu wa Hizb ut Tahrir

Katika kampeni yake inayoendelea dhidi ya Hizb ut Tahrir, Shirika la Kitaifa la Upelelezi la India lilimkamata Bava Bahrudeenand Kabeer Ahmed Aliyar mnamo 3 Februari 2025, baada ya miezi kadhaa ya unyanyasaji. Vyombo vya habari vya India viliripoti kwamba "walikula njama na wengine kueneza fikra ya Hizb ut Tahrir huko Tamil Nadu, ambalo ni shirika lililopigwa marufuku." Kisha mamlaka zikanasibisha kesi yao na kesi inayoendelea ya Dkt. Hameed Hussain chini ya Sheria ya (Kuzuia) Shughuli Zisizo Halali (UAPA) ya 1967!

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Msiikubali Marekani kama Mpatanishi, Kwa Maana sio tu kuwa ina Upendeleo; bali, ni Sehemu ya Mzozo!

Mnamo Januari 15, makubaliano yalifikiwa kusitisha vita dhidi ya Gaza kati ya umbile la Kiyahudi na harakati ya Hamas. Makubaliano hayo yalianza kutekelezwa mnamo Januari 19 mwezi huo huo na yalisimamiwa na nchi tatu: Amerika, Misri na Qatar. Tangu wakati huo hadi leo, umbile la Kiyahudi limetekeleza ukiukaji mwingi wa makubaliano haya na limeshindwa kutimiza wajibu wake mwingi, kama ilivyo kawaida kwa Mayahudi katika khiyana na uvunjaji ahadi na makubaliano.

Soma zaidi...

Kushutumu kwa Watawala wa Waislamu Mradi wa Kuwahamisha Watu wa Gaza hakufuti Upeo wa Aibu wa Usaliti wao

Usaliti wa watawala wa Waislamu, na majeshi yao, kwa watu wa Gaza, na Palestina yote, kwa zaidi ya miaka 78 ya kukaliwa kwa mabavu Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, na umbile la Kiyahudi, ni fedheha kubwa. Haiwezi kufutwa kwa shutuma tu za kuhamishwa. Watawala hawa wameficha usaliti wao mkubwa katika kipindi cha miezi kumi na tano iliyopita. Nchi kadhaa zimeelezea kukataa mipango ya kuwahamisha watu wa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina kutoka Ukanda wa Gaza, hivi karibuni Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan, ambaye alisema mnamo Jumatatu, 10 Februari, "Hakuna mtu anayeweza kuwasukuma watu wa Palestina kuelekea Nakba mpya ya uhamisho." Erdogan alisisitiza kwamba "ukaliaji kimabavu wa 'Israel' lazima ubebe gharama ya ujenzi mpya wa Gaza peke yake," akionya dhidi ya "jaribio lolote la kuwalazimisha watu wa Palestina Nakba mpya ya uhamisho."

Soma zaidi...

Urusi Yajaribu Kubandika Shtaka la Ugaidi kwa Chama Kinachoheshimika zaidi cha Kisiasa ili Kuhalalisha Ukandamizaji na Kufilisika kwake!

Chini ya kichwa cha habari: "Huduma ya Usalama ya Urusi yakamata seli ya kigaidi yenye uhusiano na Hizb ut Tahrir," Russia Today ilichapisha ripoti mnamo 5 Februari 2025, ikisema kwamba "Huduma ya Usalama ya Shirikisho la Urusi ilisambaratisha seli ya kigaidi yenye uhusiano na Hizb ut Tahrir huko Crimea na kuwakamata watu watano ambao walikuwa wakisajili wafuasi wa chama hicho, ambacho kimepigwa marufuku nchini Urusi." Video ilionyeshwa inayoonyesha operesheni ya ukamataji na uvamizi wa nyumba.

Soma zaidi...

Enyi Majeshi ya Waislamu: Nani Atawakomesha Wapumbavu Hawa Wawili?!

Jana usiku, chaneli za satelaiti zilitangaza sherehe za mapokezi ya Rais wa Marekani Donald Trump kwa Waziri Mkuu wa umbile la Kiyahudi, pamoja na mkutano wa waandishi wa habari uliotangulia mazungumzo yao. Trump alionekana kama mcheshi akilenga kufurahisha watazamaji wanaomtazama, kwa kauli zake za kizembe kuhusu Ukanda wa Gaza, na nia yake ya kuwaondoa watu wake na kuweka udhibiti wa Amerika juu yake.

Soma zaidi...

Trump Aitishia Gaza kwa Uvamizi wa Moja kwa Moja na Kuwafukuza Watu Wake

Jioni ya Jumanne, 4 Februari 2025, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza katika mkutano wake na Waziri Mkuu wa Kiyahudi kwamba "Wapalestina hawana chaguo zaidi ya kuondoka Ukanda wa Gaza. Nataka kuona Jordan na Misri zikipokea Wapalestina kutoka Gaza. Hakuna badali kwa wakaazi wa Gaza isipokuwa kuondoka." Aliongeza, "Jordan na Misri tayari zimekataa kuwapokea wakaazi kutoka Gaza, lakini baadhi ya watu wanakataa mambo isipokuwa hatimaye kukubaliana nayo."

Soma zaidi...

Maamuzi ya Mikutano ya Mawaziri wa Kiarabu ni Matupu na Hayatapita zaidi ya Maandishi kwenye Karatasi

Mkutano wa Mawaziri wa Pande Sita wa Kiarabu jijini Cairo mnamo Jumamosi, 1 Februari 2025, kuhusu Gaza na Kadhia ya Palestina ambayo ni pamoja na Jordan, Imarati, Saudi Arabia, Qatar, na Misri, pamoja na Katibu wa Kamati ya Utendaji ya Jumuiya ya Ukombozi wa Palestina na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiarabu - walithibitisha katika taarifa yao kile walichokiita "uungaji mkono wao kamili wa watu wa Palestina juu ya ardhi yao na kuzingatia haki zao halali kwa mujibu wa sheria ya kimataifa."

Soma zaidi...

Katika Kumbukumbu ya Kila Mwaka ya Kuvunjwa Khilafah na ukingoni mwa kuregea kwake, Tunaulingania Umma wa Kiislamu Uharakishe Kuisimamisha

Tangu Khilafah ilipovunjwa mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H, sawia na 3 Machi 1924 M, Ummah umekuwa ukipitia majanga na kushindwa mfululizo; kuanzia mgawanyiko wa ardhi yake, mpaka kunyang'anywa mali yake, na kuwaua wanawe, na kudhihakiwa matukufu yake na mashambulizi dhidi ya Sharia yake. Hata hivyo, leo Khilafah iko karibu zaidi kuliko wakati mwingine wowote kurudi, Rayah (bendera) yake iko tayari kupeperushwa kwa mara nyengine tena juu ya ardhi za Waislamu. Kwa hakika, tunaishi katika wakati unaokumbusha usiku ule watu wa Madina walipokuwa wakishauriana, wakikubaliana kwamba wakati umefika wa kumpa Bay'ah bwana wetu Muhammad (saw) kama kiongozi wao wa kisiasa na mkuu wa dola.

Soma zaidi...

Watawala Vibaraka Wana Hofu juu ya Tishio kwa Viti vyao vya Utawala lakini Hawana Wasiwasi juu ya Vita vya Mauaji ya Halaiki!

Mnamo Jumanne na Jumatano, wizara za mambo ya nje za Jordan, Saudia, Imarati, Mamlaka ya Palestina na Jumuiya ya Nchi za Kiarabu zililaani uchapishaji wa akaunti rasmi unaohusiana na umbile la Kiyahudi wa ramani za kanda hiyo ambazo ni pamoja na maeneo ya ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu, Jordan, Lebanon na Syria, wakidai kwamba hayo ni ramani ya kihistoria ya umbile la Kiyahudi. Walionyesha wasiwasi wao kuhusu masuala mawili.

Soma zaidi...

“Mayahudi Hawawi Radhi Nawe, Wala Wakristo, Mpaka Ufuate Mila Yao” [Al-Baqarah: 120]

Utawala mpya nchini Syria umetoa taarifa mtawalia kuhusu mfumo wa serikali ambayo wananuia kutekeleza baada ya dhalimu kutoroka. Ni wazi kuwa si mfumo aliouweka Mwenyezi Mungu (swt) bali ni mfumo wa kisekula unaotenganisha dini na maisha kwa kisingizio cha kuwapa watu uhuru wa kuchagua mfumo wa utawala. Wanawaruhusu waandamanaji wa kike wanaodai uhuru na kuvua hijab, huku wakiwateka nyara waandamanaji wasafi wanaodai kuachiliwa kwa jamaa zao wanaotaka kutabikishwa kwa Shariah ya Mwenyezi Mungu (swt)!

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu