Marekani Yatoa Tahadhari kuhusu Alfajiri ya Khilafah Rashida kwa Njia ya Utume
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kila wakati Umma unapopiga hatua kuelekea ukombozi kutoka kwenye nira ya ukoloni unaolemea sana kifua chake, na kutaka kujikomboa kutoka kwenye himaya ya Magharibi, dola za Magharibi hutoa tahadhari, zikihofia kwamba juhudi za waumini wa kweli wa Ummah zitafikia kilele kwa kuasisiwa Khilafah Rashida, kama ilivyotolewa bishara njema na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw). Kwa hivyo, Amerika na muungano wake wa Makruseda walijipanga, baada ya kukimbia kwa dhalimu wa Syria, Bashar al-Assad, na kuingia kwa wanamapinduzi jijini Damascus. Walituma mjumbe baada ya mjumbe, wakuu pamoja na wa vyeo vya chini, wanaowakilisha serikali zao, ili kudhibiti tukio ambalo Amerika na muungano wake wa Makruseda walikadiria kuwa muhimu. Endapo maji yatazidi unga, matokeo hayatakuwa mazuri kwa makafiri.