Gazeti la Al-Raya: Vichwa Vikuu vya Toleo 601
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Katika Idd hii iliyobarikiwa, Hizb ut Tahrir / Amerika inatoa salamu zake za dhati kwenu na wapendwa wenu. Mwenyezi Mungu akubali amali zenu njema, atupe rehema zake, na atulinde kutokana na adhabu yake. Idd hii iwe ya mwisho bila Khilafah.
Kutoka kwa Mtume (saw) ambaye amesema: «إِنَّ أَعْظَمَ الْأَيَّامِ عِنْدَ اللهِ يَوْمُ النَّحْرِ» “Hakika siku tukufu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu ni siku ya Arafah”, basi kwa mnasaba huu uliobarikiwa na kwa kutukuza alama za Mwenyezi Mungu Azza wa Jalla: ذَلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّهِ فَإِنَّهَا مِن تَقْوَى﴾ الْقُلُوبِ﴿ “Ndio hivyo! Na anayetukuza ibada za Mwenyezi Mungu, basi hayo ni katika unyenyekevu wa nyoyo.” [Al-Hajj: 32], na Licha ya majanga ambayo Umma wa Kiislamu unapitia chini ya watawala waliouangusha na kuusalimisha kwa adui yake, ambayo yamejaza nyoyo zetu maumivu na huzuni, bado tunapaswa kutoa pongezi na baraka zetu za dhati kwa Umma wetu wa Kiislamu, wenye subira, na wenye kutaraji mema katika Idd al-Adha iliyobarikiwa, tukimwomba Mwenyezi Mungu azifanye siku hizi za Idd kuwa za baraka, ushindi, na kuinuliwa.
Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir: Pongezi za Kitengo cha Wanawake kwa Mnasaba wa Ujio wa Idd ul-Adha Iliyobarikiwa 1447 H
Pongezi kutoka Kote Ulimwenguni kwa Mnasaba wa Idd ul-Adha Iliyobarikiwa 1447 H
Baada ya swala ya Ijumaa mnamo tarehe 5 Dhul-Hijjah 1447 H, matembezi ya Takbira (Allahu Akbar) yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Tunisia yalianza kutoka Msikiti wa Al-Fath katika mji mkuu, Tunis. Umati mkubwa wa Watunisia ulishiriki, wakipiga Takbir na Tahleel (Allahu Akbar na La Ilaha illa Allah), na kuandamana kupitia barabara kuu za mji mkuu zinazoelekea Barabara ya Al-Thawra (Mapinduzi). Mabango yaliinuliwa, ikiwa ni pamoja na moja lililoandikwa, “Allahu Akbar, na sheria ni ya Mwenyezi Mungu pekee,” jengine liliandikwa, “Allahu Akbar: Uislamu ndio kitambulisho chetu na Khilafah ndio Dola yetu,” na la tatu liliandikwa, “Allahu Akbar, Uislamu ni dini yetu na njia yetu ya maisha, Khilafah ni dola yetu, na Jihad ni njia yetu.”
Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Kipindi cha Mpito!
Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan ilizindua kampeni ya mitandao ya kijamii, haswa kwenye mtandao wa X (zamani ikijulikana kama Twitter), yenye kichwa “Katika Kumbukumbu ya Miaka 14 ya Kutekwa Nyara Kwake... Mwachilieni Huru Naveed Butt!” Kampeni hii inalenga kuishinikiza serikali dhalimu ya Pakistan, ambayo huduma zao za siri zilimteka nyara Mhandisi Naveed Butt, msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir nchini Pakistan, miaka 14 iliyopita mbele ya familia yake na majirani zake.
Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Dua kwa Naveed Butt – Mwenyezi Mungu Amfungue Kifungo Mwake