Jumamosi, 15 Dhu al-Qi'dah 1444 | 2023/06/03
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Njama Mpya Inatayarishwa Dhidi ya Mapinduzi Yanayohitaji Kuingiliwa Upya na Ujasusi wa Hay'at Tahrir al-Sham

Mnamo Jumapili tarehe 7/5/2023, Hay'at Tahrir al-Sham (HTS) alikamata idadi ya wanachama wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Syria, akiwemo Mkuu wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Syria, Ahmed Abdul Wahhab, Mjumbe wa Afisi ya Habari, Nasser Sheikh Abdul Hai, na baadhi ya wabebaji wa Dawah katika maeneo ya Idlib.

Soma zaidi...

Tetemeko la Ardhi Limefichua Sura Halisi ya Jumuiya ya Kimataifa na Mashirika Yake ya Kimataifa

Watu wa Ash-Sham waliamka alfajiri siku ya Jumatatu, 6/2/2023 na tetemeko la ardhi lenye ukubwa wa nyuzi 7.8 kwenye kipimo cha Richter, ambalo lilidumu kwa karibu dakika mbili, na kuacha uharibifu wa kutisha katika maeneo mengi ya miji ya Syria, kwani idadi ya waliokufa katika tetemeko hilo ilifikia 3,581, na zaidi ya majeruhi 12,400.

Soma zaidi...

Mkakati wa Kutambaa kwa Mchwa Unasalia Kuthibitishwa hadi Uavyaji wa Mapinduzi ya Ash-Sham... Jihadharini!

Duru rasmi za Kituruki ziliiambia Al-Jazeera kwamba Uturuki iliweka masharti ya kujiondoa kwa kile kinachojulikana kama Vikosi vya Kidemokrasia vya Syria – ambavyo kimsingi vinajumuisha Vikosi vya Ulinzi vya Watu wa Kikurdi (YPG) - kutoka Manbij, Ayn al-Arab Kobani na Tal Rifaat kaskazini mwa Syria.

Soma zaidi...

Daraa kwa Mara Nyengine Tena iko katikati ya Chuma cha Utawala wa Kihalifu na Nyundo ya Makundi ya Maridhiano

Mji wa Jasim ulizingirwa mwezi Agosti mwaka wa 2022. Kisingizio cha hilo kilikuwa uwepo wa chembechembe za ISIS katika mji huo. Mji huo baadaye ulivamiwa mnamo Oktoba; wengi waliuawa wakati wa uvamizi huo. Kabla ya hapo, mji wa Tafas ulishuhudia mandhari hiyo hiyo, na utawala wa kihalifu ulijaribu kuuvamia na kuzua mifarakano miongoni mwa wakaazi wake.

Soma zaidi...

Mapigano Mapya ya Kimakundi kati ya Vipengee vya Mfumo na Makundi Yanayohusishwa ni Jinai dhidi ya Mapinduzi ya Ash-Sham na Kupuuza Hatima yake

Maeneo ya Ngao ya Furat na Operesheni Tawi la Mzaituni, kaskazini na kaskazini-magharibi mwa Aleppo, yameshuhudia mapigano makali kwa siku kadhaa kati ya vipengee vya mfumo wa makundi yanayohusishwa na utawala wa Uturuki, kutokana na kuhusika kwa wapiganaji wa Kitengo cha Hamza katika mauaji ya mwanaharakati wa vyombo vya habari Muhammad Abu Ghannoum na mkewe, ambaye alitumiwa kama kisingizio cha kutatua hesabu na kupanua ushawishi na udhibiti.

Soma zaidi...

Kundi la Tahrir Al-Sham Limemteka Nyara Mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Syria Nasser Sheikh Abdul Hai

Mnamo Alhamisi, tarehe 1/9/2022, Vikosi vya Usalama vya Hay'at Tahrir Al-Sham vilimteka nyara mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir/Wilaya ya Syria, Ustadh Nasser Sheikh Abdul Hai, mbele ya nyumba yake katika mjini wa Atarib; hii ilikuwa ni baada ya kauli zake dhidi ya wito wa Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki, anayeutaka upinzani, kufanya maridhiano na dhalimu wa Al-Sham, na msimamo wa serikali ya Uturuki kuhusu utawala wa Bashar Al-Assad.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu