Jumapili, 26 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Tahadharini kwamba Kuondelewa Vikwazo vya Marekani kunaweza kuwa Utangulizi wa Kupoteza Ubwana na Utangulizi wa Uhalalishaji Mahusiano na Mayahudi

Rais wa Syria Ahmed al-Sharaa alikutana na mwenzake wa Marekani, Donald Trump, katika mji mkuu wa Saudi, Riyadh, mnamo Jumatano, kando ya mkutano wa kilele wa Ghuba na Marekani. Mfalme matarajiwa wa Saudia Mohammed bin Salman alihudhuria mkutano huo, huku Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan akishiriki kwa njia ya video, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Saudia.

Soma zaidi...

Kongamano la Amani ya Kiraia jijini Damascus Utangulizi wa Kuwaondoa Watiifu wa Serikali na Kuhalalisha Nembo za Ukandamizaji na Uhalifu

Mkutano na waandishi wa habari uliofanywa na Kamati ya Amani ya Kiraia katika jengo la Wizara ya Habari jijini Damascus mnamo Jumanne, Juni 10, 2025, chini ya uenyekiti wa mwanakamati Hassan Soufan, ulizua wimbi kubwa la hasira na chuki kubwa miongoni mwa Wasyria, hasa miongoni mwa familia za mashahidi na waliopotea, na watoto wa mapinduzi. Wengi waliona kauli za mkutano huo kama uchochezi kwa familia za wahasiriwa, kupuuza mihanga ya wanamapinduzi, kudharau damu ya mahsahidi, kukana ukweli usiopingika, na uhalalishaji wa wazi wa wahalifu wa kivita. Hafla hiyo ilionekana kama jaribio la kulalalisha mahusiano kwa nembo za utawala ulio ng’atuliwa chini ya mabango ya "amani ya raia," "kujenga taifa," na "kuzuia umwagaji damu."

Soma zaidi...

Aqida ya Kiislamu Pekee ndiyo Msingi wa Dola, Katiba, na Sheria Lengo ni Uislamu Uingie Madarakani na sio Kutosheka na Muislamu Kuingia Madarakani

Uislamu umetuwajibisha kuifanya Aqiyah (itikadi) ya Kiislamu kuwa msingi wa dola, na wakati huo huo, msingi wa katiba na sheria. Yaani, chanzo pekee cha sheria. Haupaswi kuambatanishwa na vyanzo vyengine vya sheria, kama ilivyo katika katiba zilizotungwa na mwanadamu; baadhi yazo zinadai kwamba Uislamu ndio chanzo kikuu au chanzo msingi cha sheria, huku kiuhalisia wanaazima sheria ngeni kwetu kutoka Magharibi.

Soma zaidi...

Pesa Zilizotumika Kutuua, Tunawezaje Kujitolea Kuzilipa?!

Katika mahojiano na gazeti la ‘Financial Times’, waziri wa mambo ya nje wa Syria alifichua ruwaza ya serikali mpya ya Syria baada ya Assad, akisisitiza kwamba nchi hiyo “haitaki kuishi kwa msaada,” na kwamba suluhisho liko katika kupunguza vikwazo vya Amerika na Ulaya. Aliongeza kuwa serikali haina mpango wa kusafirisha mapinduzi hayo ng’ambo au kuingilia masuala ya nchi nyingine. Hivyo, ikionyesha mabadiliko makubwa katika sera ya kigeni. Pia alionyesha katika mahojiano yayo hayo nia ya kubinafsisha bandari na viwanda vinavyomilikiwa na serikali na kuvutia uwekezaji wa kigeni, licha ya changamoto kubwa zinazoikabili Syria, ikiwemo madeni ya dolari bilioni 30 kwa washirika wa zamani wa Assad; Iran na Urusi.

Soma zaidi...

Mfano Hatari Ambao Haupaswi Kupuuzwa

Katika mfano hatari katika historia ya mapinduzi, Huduma Kuu ya Usalama mjini Aleppo iliteka nyara wanawake kumi mnamo siku ya Jumamosi, 21 Disemba 2024. Wanawake hao walikuwa wamejitokeza wakiandamana, wakitaka utawala wa Uislamu na kuachiliwa huru waume zao, vijana wao na watoto wao waliotekwa nyara zaidi ya mwaka mmoja na nusu uliopita. Watu hawa wamefungwa jela na Jolani [al-Julani] mjini Idlib tangu Mei 7, 2023!

Soma zaidi...

Uvamizi wa Umbile la Kiyahudi na Mashambulizi Yake ya Kiadui kwenye Ardhi ya Ash-Sham Jinai zinazoendelea ambazo ni Utawala wa Uislamu na Dola Yake ya Khilafah Pekee ndio Unaoweza Kusitisha na Kuvunja Nguvu yao

Tangu kuanguka kwa dhalimu Assad mnamo tarehe nane mwezi huu, makundi ya umbile la Kiyahudi yamekuwa yakishambulia ardhi ya Ash-Sham, na ndege zake zimekuwa zikivamia anga yake kwa mashambulizi ya angani yenye nia mbaya ambayo yalilenga miji kadhaa, na maeneo ya kijeshi. Mashambulizi haya yamefika katika mji wa Deir ez-Zor mashariki mwa Syria. Mashambulizi hayo ya chuki na kihalifu yamejikita kwenye maghala ya silaha, vikosi vya ulinzi wa anga katika maeneo ya kati na kusini, vituo vya utafiti wa kisayansi wa kijeshi, na viwanja vya ndege vya kijeshi, ikiwa ni pamoja na uwanja wa ndege wa kijeshi wa Al-Mazzeh viungani mwa Damascus.

Soma zaidi...

Mumempindua Dhalimu wa ash-Sham, Basi Msikubali Chochote baada ya Dhalimu huyo Zaidi ya Utawala wa Uislamu na Dola yake, Khilafah

Baada ya miaka kumi na nne ya mihanga mikubwa ya watu wa Syria katika mapinduzi yao yaliyobarikiwa, Damascus ilikuwa kwenye miadi ya ushindi alfajiri ya leo, Jumapili 8 Disemba 2024, kwa Idhini ya Mwenyezi Mungu (swt). Mwenyezi Mungu (swt) alitubariki kwa kupinduliwa kwa dhalimu Assad, baada ya zama za dhulma, uhalifu na udhalimu wa familia ya Assad katika utawala wake wa chuki, wa kimadhehebu kwa muda wa miaka 54. Katika zama zao, walipiga vita Dini, Shariah na waja wa Mwenyezi Mungu (swt). Waliwatia watu kila aina ya mateso. Hakuna ushahidi bora zaidi wa hili kuliko idadi ya kutisha ya wafungwa ambao waliachiliwa huru kutoka kwa magereza yake ya dhulma, maovu.

Soma zaidi...

Uvamizi Mpya wa Hay'at Tahrir al-Sham kwa Wanachama wa Hizb ut Tahrir: Hatua ya Kuelekea Uhalalisha Mahusiano au Kuelekea Kujisalimisha?!

Uvamizi mpya wa Huduma ya Kuu ya Usalama yenye uhusiano na Hay'at Tahrir al-Sham (HTS) kwa wanachama wa Hizb ut Tahrir ulikuja baada ya jina kupendekezwa kwa Ijumaa ya 22/11/2024: “Yeyote Anayelinda Mipaka ya NATO, Kuzuia Ufunguzi wa Vita na Kulinda Mipaka ya Utawala.” Huduma Kuu ya Usalama, baada ya uhamasishaji mkubwa iliyoufanya mnamo Ijumaa usiku, iliteka nyara idadi mpya ya wanachama wa Hizb ut Tahrir, ambao ni wakili Muhammad al-Sharif na Fateh al-Tarmanini kutoka mji wa Tarmanin, pamoja na mwanachama Omar Rahhal kutoka mji wa Kafr Nouran, na ndugu wawili, wanafunzi Bashar Abdul-Hay Samsoum na Ahmad Abdul-Hay Samsoum kutoka mji wa Atarib. Hapo awali, Sheikh Amir Salim, ambaye alihamishwa kutoka Jimbo la Daraa, alitekwa nyara.

Soma zaidi...

Sura Mpya ya Walaji Njama katika Astana 22 Imetanguliwa na Mkutano huko Tarnaba na Majadiliano kuhusu Kufungua Barabara na Vivuko vya Kimataifa

Enyi Wana Mapinduzi: Tusikilizeni, sisi ndugu zenu katika Hizb ut Tahrir Al-Nadheer Al-Aryan (mwonyaji wa wazi), ndugu zenu ambao mumeyaona maneno yao kuwa ya kweli na ambao kuona kwao ni kukubwa. Sisi hatuhitaji fadhila katika jambo hili juu yenu, kwani huu ni wajibu wetu na tutakutana nao kwa Mwenyezi Mungu Siku ya Kiyama. Tunakuombeni nyinyi, watu wetu, mufanyeni haraka kuregesha uamuzi wenu kutoka kwa waliouiba, kwani nchi na zana zao ni mikono yenye nia mbaya inayotaka kukuangamizeni.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu