Ijumaa, 12 Dhu al-Hijjah 1447 | 2026/05/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Pongezi kwa Idd ul-Adha Iliyobarikiwa 1447 H

Kutoka kwa Mtume (saw) ambaye amesema: «إِنَّ أَعْظَمَ الْأَيَّامِ عِنْدَ اللهِ يَوْمُ النَّحْرِ» “Hakika siku tukufu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu ni siku ya Arafah”, basi kwa mnasaba huu uliobarikiwa na kwa kutukuza alama za Mwenyezi Mungu Azza wa Jalla: ذَلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّهِ فَإِنَّهَا مِن تَقْوَى الْقُلُوبِ﴿ “Ndio hivyo! Na anayetukuza ibada za Mwenyezi Mungu, basi hayo ni katika unyenyekevu wa nyoyo.” [Al-Hajj: 32], na Licha ya majanga ambayo Umma wa Kiislamu unapitia chini ya watawala waliouangusha na kuusalimisha kwa adui yake, ambayo yamejaza nyoyo zetu maumivu na huzuni, bado tunapaswa kutoa pongezi na baraka zetu za dhati kwa Umma wetu wa Kiislamu, wenye subira, na wenye kutaraji mema katika Idd al-Adha iliyobarikiwa, tukimwomba Mwenyezi Mungu azifanye siku hizi za Idd kuwa za baraka, ushindi, na kuinuliwa.

Soma zaidi...

Salamu za Idd al-Adha Iliyobarikiwa

Tunafurahi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, kuupongeza Ummah mzima wa Kiislamu, na haswa watu wa Sudan, kwa kuwasili kwa Idd al-Adha iliyobarikiwa, tukimwomba Mwenyezi Mungu, Mtukufu, Mwenye Nguvu Zote, kuirudisha tena huku Ummah ukiwa umeungana chini ya umbo lake linalounganisha; Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, na umeachwa huru kutokana na minyororo ya utumwa kwa wakoloni makafiri wa Magharibi, ukiwa umebeba bendera ya mabadiliko, ili wanadamu waweze kujitolea katika ibada kwa Mola Mlezi wa walimwengu.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Ulikutana na Kiongozi (Amir) wa Makabila ya Hausa Mjini Port Sudan

Mnamo Alhamisi, 21/5/ 2026, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, Ustadh Nasser Ridha, akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail, Mratibu wa Kamati ya Mawasiliano, walikutana na Amiri wa makabila ya Hausa katika Wilayah ya Port Sudan, Ustadh Salih Abdul Rahman, nyumbani kwake.

Soma zaidi...

Umaskini Ulioenea na wa Kimuundo Nchini Afghanistan: Matokeo ya Kufeli Kutabikisha Mfumo wa Kiuchumi wa Uislamu—Na Uendelevu wa Fikra ya Kiuchumi ya Enzi ya Jamhuri

Ripoti za hivi karibuni—ikiwa ni pamoja na ripoti ya kushtua ya BBC kutoka mkoa wa Ghor, kujichoma moto kwa mhandisi jijini Kabul, na simulizi zinazorudiwa rudiwa za watu wanaouza figo—zimefichua janga la kibinadamu linaloumiza moyo wa kila Muislamu. Katika baadhi ya miji, foleni ndefu za watu wanaotafuta kazi, njaa, na umaskini zimekuwa uhalisia unaoonekana. Wengine, wakiwa wamekandamizwa na umaskini na madeni, wamelazimika kuwauza binti zao wadogo ili kuokoa maisha ya wanafamilia wengine. Ripoti za UNDP zinaonyesha kwamba watu watatu kati ya kila wanne nchini Afghanistan hawawezi kukidhi mahitaji yao ya msingi ya maisha, na zaidi ya asilimia kumi ya idadi ya watu wako ukingoni mwa njaa.

Soma zaidi...

Kama Hujui, Hilo Ni Janga; Lakini Kama Unajua, Basi Janga Ni Kubwa Zaidi!

Wakati wanasiasa wa Iraq na kambi zao wakigombea nyadhifa, matukio yanajitokeza ambayo yanathibitisha tena kwamba nchi hii si tu kwamba haina ubwana, bali pia kwamba maamuzi yake, ardhi, na anga zake vinakiukwa waziwazi na mtu yeyote na kila mtu. Amri za Marekani zinatolewa waziwazi na bila kuficha kuhusu uundaji wa serikali. Uingiliaji kati wa Iran kupitia kamanda wa Kikosi cha Quds cha Iran na ziara zake za mara kwa mara pia ni uko hadharani na haujafichika. Suala jengine lilikuwa ni ufichuzi wa ‘New York Times’ wa kuwepo kwa kambi mbili za kijeshi za umbile la Kiyahudi wakati wa vita vya Marekani dhidi ya Iran: moja katika Jangwa la Al-Nukhaib na nyingine katika jangwa la magharibi.

Soma zaidi...

Msamaha Jumla; Uadilifu Nusu ni Dhulma, na Hakuwezi Kuwa na Msamaha Jumla wa Kibaguzi!

Mnamo Mei 19, 2026, tovuti ya Lebanon Debate ilichapisha kile ilichokiita toleo la mwisho lililorekebishwa la sheria ya msamaha wa jumla. Ilionekana wazi kwamba sheria hii haikuwa ya jumla, ikiwajumuisha raia wote, bali iliundwa kwa vipimo vya kimadhehebu, ubaguzi, na hesabu finyu, zisizo na uwazi. Inaonyesha mwendelezo wa enzi ya dhulma iliyowekwa na utawala wa Assad mhalifu na wafuasi wake nchini Lebanon, na mtazamo unaokataa kuhama kutoka wazo la udhalimu hadi wazo la haki na usawa. Zaidi ya hayo, ukiukwaji wa kisheria uliibuka katika kuingiliwa kwa kimabavu wakati wa uandishi wa sheria ya msamaha wa jumla! Ni chini ya kanuni gani za kisheria au mifumo ya kimataifa ambapo kitu kama hicho kipo?! Ni katika chombo hiki dhaifu tu, ambacho kinathibitisha kila siku kwamba ni mkusanyiko tu wa madhehebu ambayo nchi imeundwa, si nchi ya kawaida ambapo madhehebu huishi pamoja kama mataifa mengine, mradi tu yachague mfumo wa utawala unaoegemea msingi wa utunzaji wa haki wa raia wake, usio na ukandamizaji na unyanyasaji wa kiholela!

Soma zaidi...

Hakuna Mwisho wa Mauwaji kwa Watoto wa Palestina na Lebanon Bila Kuondolewa kwa Umbile la Kiyahudi

Mnamo tarehe 13 Mei, UNICEF iliripoti kwamba angalau watoto 59 waliuawa au kujeruhiwa nchini Lebanon katika wiki iliyopita kutokana na shambulizi la umbile la Kiyahudi nchini humo. Tangu kuanza kwa usitishaji mapigano mnamo tarehe 17 Aprili 2026, angalau watoto 23 wameuawa na 93 kujeruhiwa, na kufikisha jumla ya watoto 200 waliouawa na 806 waliojeruhiwa nchini Lebanon tangu tarehe 2 Machi. Mapema mwezi huu, iliripotiwa kwamba msichana wa miaka 12 na baba yake waliuawa huko Nabatieh baada ya Jeshi la Ulinzi la ‘Israel’ kumlenga kupitia droni kwa mashambulizi matatu ili kuhakikisha kwamba haishi.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan ina furaha kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wote walio nah amu na masuala ya umma kuhudhuria kikao kipya cha kisiasa, kinachomkaribisha Ustadh Ibrahim Mushrif, mwanachama wa Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan, chenye kichwa: “Dori Iliyopewa Nchi Jirani katika Vita vya Sudan”

Soma zaidi...

ACSA na GSOMIA: Watu Wenye Ufahamu na Wanasiasa Wenye Ikhlasi Wanapaswa Kujitokeza Kuilinda Nchi Isije Kuwa Nchi ya Kitumwa

Inatisha sana kwa watu wa Bangladesh, wakati vyanzo mbalimbali vinathibitisha kwamba Marekani na Bangladesh zinaendelea na mfululizo wa mikataba ya ulinzi na biashara chini ya ‘Mkataba wa Biashara wa Pamoja (ART)’ wa kikoloni. Kampeni ya Marekani ya GSOMIA ilihama kutoka fahamu dhahania hadi ramani halisi mnamo Machi 2022, wakati Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani wa wakati huo Victoria Nuland alipowasilisha rasimu ya Mkataba Mkuu wa Usalama wa Taarifa za Kijeshi (GSOMIA) ndani ya mfumo wa Mkakati wa Marekani wa Indo-Pacifiki (IPS) ulitarajiwa mnamo 2017 na kuandikwa mnamo 2019. Ingawa ziara ya Nuland ilikuwa alama muhimu kwa GSOMIA, Mkataba wa Upataji na Huduma Mtambuka (ACSA) uliinuliwa rasmi mnamo Aprili 2019 na kuitekelezwa wakati wa Mazungumzo ya 7 ya Usalama jijini Dhaka.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu