Ijumaa, 11 Muharram 1448 | 2026/06/26
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

“Imekwisha fichuka chuki yao katika midomo yao. Na yanayo ficha vifua vyao ni makubwa zaidi.” [Aal-i-Imran: 118]

Chansela wa Ujerumani Friedrich Merz alitangaza mnamo Ijumaa kupinga kwake Muungano wa Ulaya kuweka vikwazo kwa umbile la Kiyahudi, huku Ufaransa ikitangaza kwamba haitakubali kuondoa vikwazo vilivyowekwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu Iran isipokuwa makubaliano yoyote ya mwisho kuhusu mpango wake wa nyuklia yajumuishe kushughulikia mpango wake wa makombora ya masafa marefu na uungaji mkono wake kwa makundi yenye silaha katika eneo hilo.

Soma zaidi...

Ardhi Zetu Zitabaki Kukiukwa na Damu Yetu Itaendelea Kumwagika Hadi Tutakaposimamisha Khilafah Rashida Yetu

Mnamo Jumapili, tarehe 14 Juni 2026, jeshi la Kiyahudi lilifanya shambulizi la anga likilenga vitongoji vya kusini mwa Beirut, saa chache tu baada ya kuwaonya wakaazi wa takriban miji 30 kusini mwa Lebanon na kuwaamuru waondoke. Tovuti ya habari ya Axios iliripoti kwamba “jeshi la ‘Israel’ liliiarifu CENTCOM muda mfupi kabla ya shambulizi jijini Beirut kutokea.” Trump aliandika kwenye jukwaa lake la ‘Truth Social’ mnamo Jumapili: “Shambulizi la asubuhi ya leo dhidi ya Beirut halikupaswa kutokea, haswa katika siku maalum ambapo tuko karibu sana na Mkataba wa Amani na Iran.”

Soma zaidi...

Mwaka Mpya wa Hijri Sio Maadhimisho ya Kihistoria, Bali Mwanzo wa Kusimamishwa kwa Dola ya Kiislamu Na Khilafah Rashida ya Pili kwa Njia ya Utume Itarudi Tena

Mwaka Mpya wa Hijri unatujia tarehe 1 Muharram 1448 H, sawia na 16/06/2026 M. Hii ndiyo tarehe iliyochaguliwa na Al-Faruq Umar ibn Al-Khattab na Maswahaba watukufu (ra) kama kalenda ya Waislamu. Alichagua tarehe hii kwa sababu iliashiria kuzaliwa kwa Dola ya kwanza ya Kiislamu iliyosimamishwa na Mtume wetu (saw) mjini Al-Madinah Al-Munawwarah.

Soma zaidi...

Matendo ya Watu wa Ash-Sham Yanathibitisha Kwamba Wao Ndio Wamiliki wa Halisi wa Nguvu na Wanapaswa Kuwa Nusra ya Kimaumbile Baada ya Utabikishaji wa Uislamu

Harakati maarufu katika majiji na miji kadhaa ya Syria, zinazojirudia kwa zaidi ya mnasaba mmoja baada ya kuanguka kwa utawala wa kihalifu uliokufa, hivi karibuni zaidi vuguvugu maarufu dhidi ya wale wanaoitwa Shabiha (majambazi), zinathibitisha ukweli kadhaa ambao haupaswi kusahaulika na watu wetu nchini Syria

Soma zaidi...

Serikali ya Tunisia Itaendelea na Uzembe Wake Hadi Lini na Kuruhusu Malori Haya ya Kifo Kuchukua Maisha ya Wafanyikazi wa Kike wa Mashamba?

Ghadhabu na hasira ziliongezeka nchini Tunisia wiki iliyopita kufuatia ajali nyingine mbaya, wakati huu katika wilaya ya Mazouna katika jimbo la Sidi Bouzid. Ajali hiyo iliwaacha wafanyikazi kadhaa wa kike wa shambani wakiwa wamejeruhiwa na wawili wakiwa wamekufa katika eneo la tukio. Tunisia inashuhudia kujirudia kwa matukio kama hayo kutokana na serikali kushindwa kukomesha usafiri usiodhibitiwa na kuboresha hali mbaya ya wafanyikazi wa kike wa mashamba! Bila shaka, serikali hii inakwepa kutoa tarakimu na takwimu sahihi zinazoonyesha ukubwa wa janga hilo!

Soma zaidi...

Moto Mijini: Jinsi Ubepari Unavyowasha Moto katika Miji ya Waislamu yenye Wakaazi Wengi

Mnamo Jumatatu, tarehe 1 Juni 2026, vyombo vya habari viliripoti kuhusu moto mkubwa ulioharibu eneo la makaazi lenye watu wengi huko Kebon Kosong, Kemayoran, Jakarta ya Kati, Indonesia. Takwimu rasmi kutoka kwa Wakala wa Kupunguza Maafa wa DKI Jakarta (BPBD) na uthibitishaji wa uwanjani zinaonyesha takriban familia 354—takriban watu 620—waliachwa bila makao. Takriban watoto 160 wenye umri wa kwenda shule waliathiriwa moja kwa moja.

Soma zaidi...

Je, Erdogan Anasubiri Mayahudi Waipige Mabomu Ankara Kabla ya Kuhamasisha Jeshi Lake?!

Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan, katika hotuba aliyotoa wakati wa mkutano wa kundi la wabunge wa Chama cha Haki na Maendeleo katika Bunge la Uturuki, alisema: "Tunafahamu vyema lengo kuu la udanganyifu wa 'Ardhi iliyo Ahidiwa', na Mungu akipenda, hatutaruhusu kamwe." Alifafanua kwamba usalama wa Uturuki hauanzii katika mkoa wa Hatay kusini mwa Uturuki, bali Aleppo, Damascus, na Beirut. Aliendelea: "Ikiwa uonevu wa Israel hautasimamishwa, gharama haitalipwa na eneo hilo pekee, bali na wanadamu wote." Erdoğan alizisihi dola kuu duniani kuchukua msimamo wazi dhidi ya umbile hilo la Kizayuni, akisema: "Kuirudisha Israel katika kufuata sheria sio tena jukumu la baadhi ya nchi tu, bali ni jukumu la pamoja linalowaangukia wanadamu wote."

Soma zaidi...

Mtoto Aliyeuawa Shahidi, Kuhesabiwa kwa Waathiriwa Kutaisha Lini? Watu wa Damu hiyo Watainuka Lini Kuwalipiza Kisasi?

Wizara ya Afya ya Palestina ilisema kwamba vikosi vya uvamizi vilifyatua risasi kwenye gari moja lililokuwa limebeba raia wa Palestina katika mji wa Hebron katika Ukingo wa Magharibi wa kusini unaokaliwa kimabavu, na kusababisha kifo cha kishahidi cha mtoto mchanga wa miezi saba Sam Abu Hikal huku akiwa mikononi mwa mamake. Mamake na babake pia walijeruhiwa.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Kadhia za Umma

Tunafuraha, kama Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wote walio na hamu na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika Kikao cha kila mwezi cha Kadhia za Umma, ambacho mwezi huu kitafanyika katika afisi ya Hizb jijini Khartoum baada ya kukatizwa kwa muda mrefu kwa zaidi ya miaka mitatu kutokana na vita.

Soma zaidi...

Jibu kwa Mwandishi wa Makala (Usekula na Ugumu wa Historia ya Uislamu Iliyoghushiwa)

Uislamu ni itikadi ya kiroho na kisiasa ambayo ilikuja kushughulikia matatizo ya wanadamu, kwa kutambua kwamba wanadamu wana silika (ghariza) na mahitaji ya kimwili ambayo yanahitaji kushibishwa. Uislamu umebainisha jinsi mahitaji haya yanavyopaswa kukidhiwa bila ya ziada au upungufu, kupitia hukmu kutoka kwa Mwenye hekima, Mjuzi wa yote. Yeye aliyewaumba wanadamu anajua kipi kuna manufaa na kipi kina madhara kwao! Ukosefu wa elimu wa mwandishi juu ya hukmu hizi haumwondolei jukumu; badala yake, unasisitiza kutoujua kwake Uislamu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu