Jumatatu, 29 Dhu al-Hijjah 1447 | 2026/06/15
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Kadhia za Umma

Tunafuraha, kama Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, kuwaalika wanahabari, wanasiasa, na wote walio na hamu na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika Kikao cha kila mwezi cha Kadhia za Umma, ambacho mwezi huu kitafanyika katika afisi ya Hizb jijini Khartoum baada ya kukatizwa kwa muda mrefu kwa zaidi ya miaka mitatu kutokana na vita.

Soma zaidi...

Vikosi vya Msaada wa Haraka Vinafanya Mauaji Dhidi ya Watu Wasio na Silaha, na Serikali Haiwezi Kuwalinda!

Mnamo Alhamisi na Ijumaa, Mei 28 na 29, 2026, Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vilizindua mashambulizi kwenye vijiji vilivyo magharibi mwa mji wa Bara katika Jimbo la Kordofan Kaskazini, na kusababisha vifo vya raia kadhaa wasio na silaha. Mtandao wa Madaktari wa Sudan ulithibitisha katika taarifa mnamo Ijumaa, Mei 29, 2026, kwamba RSF ilifanya mauaji makubwa katika mji wa Al-Marra na vijiji vinavyozunguka, na kuwaua raia 27. Katika ripoti yake ya hivi karibuni mnamo Jumamosi, Mei 30, 2026, Al-Arabiya TV ilisema: “Idadi ya vifo kutokana na mauaji ya Vikosi vya Msaada wa Haraka katika eneo la Al-Marra huko Kordofan Kaskazini imeongezeka hadi 58.” Wakati Vikosi vya Msaada wa Haraka vinafanya mauaji haya katika vijiji vya Kordofan, serikali inalaani tu na kuhesabu waliokufa, bila kuchukua hatua zozote kali kuzuia mauaji haya kutokea.

Soma zaidi...

Ulaya Yahangaika Siku Chache Tu Bila Mafuta na Gesi ya Waislamu: Vipi Basi Ikiwa Ummah Ungeamka?!

Waziri wa Fedha wa Ufaransa Roland Lescure alisema kwamba serikali haziwezi kuamua kama zitoe akiba ya ziada ya mafuta ya kimkakati ili kupunguza usumbufu unaosababishwa na vita vya Iran hadi muda unaowezekana wa mzozo huo utakapokuwa wazi. Katika muktadha huo huo, mashambulizi ya awali ya makombora ya Iran kwenye kituo cha gesi cha Ras Laffan nchini Qatar, mojawapo ya vituo vikubwa zaidi vya gesi asilia vilivyoyeyushwa duniani, yalisababisha kupungua kwa kasi kwa akiba ya gesi ya Uingereza. Akiba ya gesi asilia nchini Uingereza ilishuka hadi viwango vya kutosha kukidhi matumizi ya ndani kwa muda usio zidi  masaa 48.

Soma zaidi...

Ufisadi wa Mfumo Huzalisha Ufisadi katika Masuluhisho Sera ya Ufukarishaji: Zawadi ya Idd al-Adha kutoka kwa Watawala kwa Watu wa Yemen

Serikali ya Shaea Al-Zandani mnamo Jumanne, 19/05/2026, ilianzisha hatua mpya ya kiuchumi ambapo ilipandisha bei ya dolari ya ushuru wa forodha kwa zaidi ya 100%, kutoka riyali 750 hadi riyali 1,550, na kuongeza bei ya chombo cha dizeli cha lita 20 kwa 24.5%, ikiruka kutoka riyali 29,500 hadi 36,000. Kisha ilijaribu kuwaziba macho watu wa Yemen kwa kuidhinisha posho ya gharama ya maisha ya 20% kwa wafanyikazi wa sekta ya umma, pamoja na kuwapa nyongeza yao ya kila mwaka inayostahili kwa miaka ya 2021-2024, na kufanya marekebisho ya viwango vya kazi ambayo yalikuwa yamesimamishwa kwa zaidi ya miaka 13.

Soma zaidi...

Salamu za Idd Idd ni Wakati Ambapo Furaha na Huzuni Zinaunganishwa!

Siku hizi Idd al-Adha inafika, ambapo furaha na huzuni zimechanganyika. Furaha katika mwitikio wa waumini kwa wito wa Mwenyezi Mungu wa Hijja, wakiitikia wito wake katika mkusanyiko unaowaunganisha kutoka pembe zote za dunia, pamoja na makabila na rangi zao mbalimbali, kwa kutii amri ya Mwenyezi Mungu na kupata radhi Zake. Na huzuni kubwa inawakumba nyoyo zao kwa masaibu yao tangu kupoteza nguvu yao na kuvunjwa kwa dola yao mikononi mwa mhalifu Mustafa Kemal. Ni Idd ya aina gani huku Gaza ikiendelea kutokwa na damu?! Idd ya aina gani huku kambi na meli za kivita za maadui wa Umma zikiwa katikati ya ardhi zake?! Idd ya aina gani huku wanawake huru wa Waislamu wakidhalilishwa huko Palestina, Turkestan Mashariki, Myanmar, na India?!

Soma zaidi...

Pongezi kwa Idd ul-Adha Iliyobarikiwa 1447 H

Kutoka kwa Mtume (saw) ambaye amesema: «إِنَّ أَعْظَمَ الْأَيَّامِ عِنْدَ اللهِ يَوْمُ النَّحْرِ» “Hakika siku tukufu zaidi mbele ya Mwenyezi Mungu ni siku ya Arafah”, basi kwa mnasaba huu uliobarikiwa na kwa kutukuza alama za Mwenyezi Mungu Azza wa Jalla: ذَلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّهِ فَإِنَّهَا مِن تَقْوَى الْقُلُوبِ﴿ “Ndio hivyo! Na anayetukuza ibada za Mwenyezi Mungu, basi hayo ni katika unyenyekevu wa nyoyo.” [Al-Hajj: 32], na Licha ya majanga ambayo Umma wa Kiislamu unapitia chini ya watawala waliouangusha na kuusalimisha kwa adui yake, ambayo yamejaza nyoyo zetu maumivu na huzuni, bado tunapaswa kutoa pongezi na baraka zetu za dhati kwa Umma wetu wa Kiislamu, wenye subira, na wenye kutaraji mema katika Idd al-Adha iliyobarikiwa, tukimwomba Mwenyezi Mungu azifanye siku hizi za Idd kuwa za baraka, ushindi, na kuinuliwa.

Soma zaidi...

Salamu za Idd al-Adha Iliyobarikiwa

Tunafurahi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, kuupongeza Ummah mzima wa Kiislamu, na haswa watu wa Sudan, kwa kuwasili kwa Idd al-Adha iliyobarikiwa, tukimwomba Mwenyezi Mungu, Mtukufu, Mwenye Nguvu Zote, kuirudisha tena huku Ummah ukiwa umeungana chini ya umbo lake linalounganisha; Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, na umeachwa huru kutokana na minyororo ya utumwa kwa wakoloni makafiri wa Magharibi, ukiwa umebeba bendera ya mabadiliko, ili wanadamu waweze kujitolea katika ibada kwa Mola Mlezi wa walimwengu.

Soma zaidi...

Je, Sio Wakati wa Ummah Kuwekeza Utajiri Wake Katika Kujenga Maslahi na Nguvu Zake Wenyewe?

Utajiri na rasilimali za Ummah zinaendelea kufujwa ili kutajirisha Magharibi, huku ndani ya nchi, zikitumika kwa anasa zinazowaweka Waislamu mbali na mfumo wa maisha wa Kiislamu. Mnamo Alhamisi, 21/5/2026, Mamlaka Kuu ya Burudani ya Saudi Arabia ilitangaza muungano mpya wa Saudi Arabia na Misri unaolenga kujenga mfumo jumuishi wa matukio makubwa katika eneo hilo, unaounganisha nchi hizo mbili kwenye njia moja ya kuvutia wasanii na nyota wa kimataifa! Wakati huo huo, mnamo Jumatano, 20/5/2026, nchi za Baraza la Ushirikiano la Ghuba (GCC) na Uingereza zilitangaza makubaliano ya kihistoria na makubwa ya biashara huria yenye thamani ya takriban dolari bilioni 5, na kuifanya Uingereza kuwa taifa la kwanza la G7 kusaini makubaliano kama hayo na kambi ya Ghuba.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Ulikutana na Kiongozi (Amir) wa Makabila ya Hausa Mjini Port Sudan

Mnamo Alhamisi, 21/5/ 2026, ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, ukiongozwa na Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir/ Wilayah ya Sudan, Ustadh Nasser Ridha, akifuatana na Ustadh Abdullah Ismail, Mratibu wa Kamati ya Mawasiliano, walikutana na Amiri wa makabila ya Hausa katika Wilayah ya Port Sudan, Ustadh Salih Abdul Rahman, nyumbani kwake.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu