“Imekwisha fichuka chuki yao katika midomo yao. Na yanayo ficha vifua vyao ni makubwa zaidi.” [Aal-i-Imran: 118]
- Imepeperushwa katika Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Chansela wa Ujerumani Friedrich Merz alitangaza mnamo Ijumaa kupinga kwake Muungano wa Ulaya kuweka vikwazo kwa umbile la Kiyahudi, huku Ufaransa ikitangaza kwamba haitakubali kuondoa vikwazo vilivyowekwa na Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu Iran isipokuwa makubaliano yoyote ya mwisho kuhusu mpango wake wa nyuklia yajumuishe kushughulikia mpango wake wa makombora ya masafa marefu na uungaji mkono wake kwa makundi yenye silaha katika eneo hilo.



