Hatua Mpya za UN na za Kanda za Kuoanisha Serikali Tawala ya Afghanistan ndani ya Mfumo wa Kisekula wa Dunia
- Imepeperushwa katika Afghanistan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Katika siku za hivi karibuni, Umoja wa Mataifa umekuwa ukifuatilia shughuli zake nchini Afghanistan kwa kasi zaidi kuliko hapo awali. Ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Masuala ya Kibinadamu jijini Kabul na Kandahar, pamoja na mwaliko wa Amir Khan Muttaqi-Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali tawala nchini Qatar, inaashiria juhudi mpya za kuendeleza mipango ya kimataifa na kushawishi serikali ya Afghanistan.