Ijumaa, 04 Sha'aban 1447 | 2026/01/23
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hitimisho la Kampeni “Khilafah sio Ndoto… Bali, ni Kilio cha Ulimwengu Unaowaka Moto!”

Leo, kwa Msaada Wake, tunahitimisha kampeni ya kimataifa iliyozinduliwa na Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir, kwa maelekezo ya Amiri wa Hizb ut Tahrir, mwanachuoni mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, katika kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, ambayo iliamshwa na wanaume na wanawake wa Hizb ut Tahrir kote ulimwenguni.

Soma zaidi...

Kongamano la kila Mwaka la Hizb ut Tahrir katika Wilayah Lebanon Kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 105 ya Kuvunjwa kwa Khilafah “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha, au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Uislamu?!”

Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Lebanon ilifanya kongamano lake la kila mwaka la kisiasa kwa kichwa: “Kuhalalisha Mahusiano na Kujisalimisha, au Ahadi ya Mwenyezi Mungu na Dola ya Uislamu?!”, ambapo wazungumzaji kutoka Lebanon, Syria, Uturuki, na Gaza walishiriki.

Soma zaidi...

Mapendekezo ya Kongamano Lililofanywa na Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan Kukumbuka 105 Hijri Tangu Kuvunjwa kwa Khilafah

Mnamo Jumamosi, tarehe 28 Rajab 1447 H, sambamba na tarehe 17 Januari 2026 M, Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan ilifanya kongamano la kumbukumbu ya miaka 105 tangu kuvunjwa kwa dola ya Kiislamu ya Khilafah. Kongamano hilo lilihudhuriwa na watu mashuhuri, wakiwemo wanasiasa, watu mashuhuri wa vyombo vya habari, wasomi, na viongozi wa jamii. Kwa kuzingatia kwamba kumbukumbu hii chungu inakuja huku sisi nchini Sudan tukiteseka kutokana na vita vilivyowashwa na ubeberu wa Marekani, ikiwatumia vibaraka wake wa ndani kusambaratisha kile kilichobaki cha umoja wa nchi yetu chini ya sera yake inayoitwa “Mipaka ya Damu”. Hivyo, kichwa cha kongamano letu kilikuwa: “Sudan Kati ya Sera za Mipaka ya Damu na Kuunganisha Watu Kuwa Umma Mmoja.”

Soma zaidi...

Vyombo vya Usalama jijini Umdurman Vyalikamata Kundi la Wanachama wa Hizb ut Tahrir

Kufuatia utekelezaji wa mashababu wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan wa visimamo vitatu katika maeneo tofauti tofauti katika jiji la Omdurman, asubuhi ya Jumatano iliyopita, 25 Rajab 1447 H, sambamba na 14/1/2026 M, ndani ya muundo wa kukumbusha tukio la kupita kwa miaka 105 tangu kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah mwezi Rajab 1342 H, vyombo vya usalama viliendelea kuwakamata wanachama watano wa Hizb: Al-Radi Muhammad Ibrahim, Fadlallah Ali Suleiman, Omar Al-Bashir, Hassan Fadl, na Mujahid Adam. Kisha waliachiliwa baada ya Magharibi siku ya Jumatano baada ya nambari zao za simu kuchukuliwa na baada ya kunyakua mabango ambayo Mashababu hao wa Hizb ut Tahrir walikuwa wamebeba katika visimamo hivyo vitatu. Kisha waliitwa mnamo alasiri ya Alhamisi, 15/1/2026, na wangali wako kizuizini hadi wakati wa kuandika taarifa hii!!

Soma zaidi...

Mikutano na Matembezi ya Kulaani Yaliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir / Wilayah Bangladesh: Enyi Watu! Pingeni Mpango wa Kupeleka Jeshi Letu Gaza chini ya Kikosi Kilichopendekezwa na Trump, na Takeni Msimamo Wazi kutoka kwa Wagombea katika Uchaguzi Ujao

Hizb ut Tahrir katika Wilayah Bangladesh, iliandaa mikutano na matembezi mengi ya kulaani leo, Ijumaa (16 Januari 2026), baada ya swala ya Ijumaa, katika majengo mbalimbali ya misikiti jijini Dhaka na Chattogram, dhidi ya mpango wa kupeleka vikosi vya nchi hii kwa “Kikosi cha Kuleta Utulivu wa Kimataifa” kilichopendekezwa na Trump huko Gaza. Ili kupinga mpango huu mbaya wa Marekani, na kuwataka wagombea na vyama vya kisiasa katika uchaguzi ujao kuelezea msimamo wao kuhusu suala hili.

Soma zaidi...

Barua ya Wazi kwa Mkurugenzi Mkuu wa ASIO Mike Burgess kutoka Hizb ut Tahrir / Australia

Kuhusu Khilafah, jaribio lako la kutia matope maji lilionekana wazi zaidi ulipopotoka wakati wa majadiliano yako ya baada ya muhadhara. Kwanza, ombi lako la mila za chuki dhidi ya Uislamu linawachora Waislamu kama daraja za tano katika nchi hii, inayothibitishwa kupitia kuwepo kwao tu, inazidi mipaka yote ya usawa na kutokuwa na upendeleo. Muhadhara huu kamwe haukuwa kuhusu kuwasilisha ukweli bali kuhusu kuendeleza ajenda.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Ilifanya Kisimamo na Hotuba ya Hadhara huko Nile Mashariki jijini Khartoum

Mashababu wa Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan huko Nile Mashariki jijini Khartoum walifanya, mnamo Jumamosi, 10/01/2026, kisimamo na hotuba ya hadhara ya kisiasa huko Souq Sitta. Hotuba hiyo ilitolewa na Ustadh Hammad Al-Dayi, mwanachama wa Hizb, ambapo alielezea ubora wa Ummah huu, ambao ulitimiza wajibu wake katika kuwaongoza wanadamu chini ya Dola ya Khilafah, hadi ilipovunjwa na mkoloni kafiri mnamo Rajab 1342 H. Aliukumbusha Ummah kuhusu tukio hili uchungu, na jinsi, kwa kuvunjwa Khilafah, ulivyompoteza Imam ambaye ni ngao, umoja wake na kuchanika vipande vipande, na mkoloni kafiri akapata udhibiti juu yake ili kugawanya ardhi zake.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Kongamano kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Kuvunjwa Khilafah katika Hoteli ya Al-Busayri Plaza

Kwa mnasaba wa tukio la kupita miaka 105 ya hijriya tangu kuvunjwa kwa Dola ya Waislamu, Khilafah mnamo 28 Rajab 1342 H, na kama mwendelezo wa kuwakumbusha Waislamu faradhi ya kufanya kazi ya kuiregesha kama Dola ya Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan yatoa heshima kukualikeni kuhudhuria kongamano lenye kichwa: “Sudan Kati ya Sera ya Mipaka ya Damu na Sera ya Kuwaunda Watu Kuwa Ummah Mmoja”

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan Yafanya Visimamo Kadhaa katika Miji Tofauti Tofauti kote nchini Sudan

Ndani ya muundo wa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah mnamo Rajab 1342 H, na kama ukumbusho kwa Ummah wa tukio hili chungu, si kwa lengo la kulia juu ya historia tukufu iliyopotea, bali ili kuchochea azma ili Ummah uweze kutimiza wajibu wake wa kusimamisha Khilafah ili kuishi chini ya sheria za Mola wa Mlezi Walimwengu na kuondoa dhambi ya kifo cha Jahiliyyah kutoka shingoni mwake, Mashababu wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan walifanya matembezi kadhaa katika miji tofauti kote Sudan, kufuatia swala ya Ijumaa mnamo 20 Rajab 1447 H, sawia na 9 Januari 2026 M

Soma zaidi...

Mkutano na Hotuba katika Mji wa El Obeid

Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 105 ya kuvunjwa kwa Khilafah, wanachama wa Hizb ut Tahrir walifanya mkutano na hotuba ya hadhara katika mji la El Obeid, mji mkuu wa Kordofan Kaskazini, mnamo Jumatano, 18 Rajab 1447 H, sambamba na 7 Januari 2026 M, katika uwanja wa Msikiti wa Soko la Al-Salihin.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu