Katikati ya Mashambulizi ya Marekani kwa ajili ya Kuhalalisha Mahusiano na Kusalim Amri! Ziara Nyingine ya Mara kwa Mara ya Mjumbe wa Marekani Ortagus nchini Lebanon!
- Imepeperushwa katika Lebanon
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kwa kuzingatia mashambulizi ya Marekani dhidi ya Lebanon na eneo hili pamoja na mradi wa kuhalalisha mahusiano na kusalim amri, na juhudi za utawala wa Trump na timu yake kuwaleta watawala zaidi wa Waislamu katika Makubaliano ya Abraham, inakuja ziara ya mjumbe wa Marekani Morgan Ortagus nchini Lebanon na umbile nyakuzi la Kizayuni, iliyojaa shinikizo, vitisho, na hali za kisiasa, usalama, na kiuchumi zilizolazimishwa nchini Lebanon. Ziara hii iliambatana na ziara ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kiarabu na Mkurugenzi wa Ujasusi wa Misri, ikionekana kutimiza lengo moja!



