Jumamosi, 23 Sha'aban 1446 | 2025/02/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Miaka Miwili Iliyopita Baada ya Tetemeko la Ardhi la Februari 6 Bado Mateso Hayana Mwisho

Mnamo Februari 6, 2023, matetemeko makubwa mawili ya ardhi yenye kipimo cha 7.8 na 7.5, yaliyopiga kusini na katikati mwa Uturuki na kaskazini mwa Syria, yaliathiri mikoa 11 na kusababisha uharibifu mkubwa na kupoteza maisha. Takriban watu 54,000 nchini Uturuki na 8,500 nchini Syria walipoteza maisha katika matetemeko haya ya ardhi huku kitovu cha matetemeko hayo kikiwa Kahramanmaraş. Jumla ya waliopoteza maisha ilizidi 62,000, na mamilioni ya watu wakabaki bila makao. Hata hivyo, baadhi ya wataalamu wa huru na rasilimali za ndani zinaonyesha kuwa idadi halisi inaweza kuwa kubwa zaidi.

Soma zaidi...

Watawala wa India Wanatumia Sheria ya (Kuzuia) Shughuli zisizo halali ya 1967 kupiga Vita Uislamu na Waislamu, wakimwemo Mashababu wa Hizb ut Tahrir

Katika kampeni yake inayoendelea dhidi ya Hizb ut Tahrir, Shirika la Kitaifa la Upelelezi la India lilimkamata Bava Bahrudeenand Kabeer Ahmed Aliyar mnamo 3 Februari 2025, baada ya miezi kadhaa ya unyanyasaji. Vyombo vya habari vya India viliripoti kwamba "walikula njama na wengine kueneza fikra ya Hizb ut Tahrir huko Tamil Nadu, ambalo ni shirika lililopigwa marufuku." Kisha mamlaka zikanasibisha kesi yao na kesi inayoendelea ya Dkt. Hameed Hussain chini ya Sheria ya (Kuzuia) Shughuli Zisizo Halali (UAPA) ya 1967!

Soma zaidi...

Marufuku ya Kyrgyzstan dhidi ya Niqab ni Jaribio la Kutapatapa la Utawala wake wa Kisekula Kukandamiza Kuibuka kwa Kitambulisho cha Kiislamu Miongoni mwa Watu wake

Kyrgyzstan imekuwa nchi ya hivi punde zaidi katika Asia ya Kati kupiga marufuku Niqab. Hatua hii ya kisheria ilianza kutekelezwa mnamo tarehe 1 Februari 2025 na ukiukaji huu utatozwa faini ya 20,000 som ($230). Nguo za Kiislamu za wanawake na ndevu za wanaume zimekuwa zikilengwa na serikali za Asia ya Kati kwa muda mrefu, ambapo dola zenye nguvu ya kisekula zinaogopa ushawishi unaoongezeka wa Uislamu. Wabunge wa Kyrgyzstan wametoa kisingizio duni kwamba marufuku hiyo inahitajika kwa sababu za usalama, ili nyuso za watu zionekane na watu binafsi kutambuliwa. Lakini wapinzani wanasema marufuku hiyo inawanyima wanawake uhuru wa kuvaa wanavyotaka.

Soma zaidi...

Enyi Majeshi! Chagueni kati ya Watawala hawa ambao ni Watiifu kwa Trump, na Khalifa Rashid ambaye ataikomboa Gaza na Palestina nzima kupitia Nguvu za Kijeshi!

Mnamo Jumanne 4 Februari 2025, akiwa ameketi ubavuni mwa muuaji wa Gaza, Benjamin Netanyahu, Rais Trump wa Marekani alitangaza, "Marekani itauchukua Ukanda wa Gaza, na tutafanya kazi nayo pia." Tamko la kiburi la Trump kuhusu Gaza ni kofi kwenye uso wa watawala wa Waislamu, ambao wametekeleza kwa utiifu amri ya Marekani, na kuzuia vikosi vya majeshi ya Waislamu kupigana na umbile la Kiyahudi, na hivyo kuruhusu mauaji ya Waislamu nchini Palestina. Watawala wa sasa wa Waislamu, kama wale waliotangulia, wanajifunza kwamba Marekani haiwajali wao, au viti vyao vya khiyana. Marekani itaendelea kuwadhalilisha na kuwashusha hadhi mbele ya dunia na watu wao wenyewe. Kwa hakika, kushiriki katika mfumo wa dunia unaoongozwa na Marekani, na kushikamana na sheria za kimataifa na taasisi za kimataifa, si chochote ila unyenyekevu na utiifu kwa Marekani na rais wake. Hata hivyo watawala hawa hawajali. Hata hivi sasa wanakimbilia kumfurahisha na kumtuliza bwana wao, Amerika, wakijaribu kuwasilisha kwake "mpango wa amani wa Waarabu" wao wenyewe.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu: Msiikubali Marekani kama Mpatanishi, Kwa Maana sio tu kuwa ina Upendeleo; bali, ni Sehemu ya Mzozo!

Mnamo Januari 15, makubaliano yalifikiwa kusitisha vita dhidi ya Gaza kati ya umbile la Kiyahudi na harakati ya Hamas. Makubaliano hayo yalianza kutekelezwa mnamo Januari 19 mwezi huo huo na yalisimamiwa na nchi tatu: Amerika, Misri na Qatar. Tangu wakati huo hadi leo, umbile la Kiyahudi limetekeleza ukiukaji mwingi wa makubaliano haya na limeshindwa kutimiza wajibu wake mwingi, kama ilivyo kawaida kwa Mayahudi katika khiyana na uvunjaji ahadi na makubaliano.

Soma zaidi...

Wanasiasa wa Sudan Wanatekeleza Njama za Amerika Kuichana Nchi!

Mnamo Alhamisi, 13 Februari 2025, Al-Sharq iliripoti kwamba Osama Saeed, kiongozi wa Chama cha Mapinduzi, alisema: “Kundi letu linapanga kutangaza serikali kufikia mwisho wa Februari.” Alikuwa anakusudia serikali sambamba na ile iliyopo Port Sudan kwa sasa. Alifafanua zaidi: “Ngazi za utawala katika serikali ya kiraia ndani ya maeneo yanayodhibitiwa na Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) zitajumuisha rais wa Baraza Kuu, wajumbe, na Baraza la Mawaziri.”

Soma zaidi...

Kushutumu kwa Watawala wa Waislamu Mradi wa Kuwahamisha Watu wa Gaza hakufuti Upeo wa Aibu wa Usaliti wao

Usaliti wa watawala wa Waislamu, na majeshi yao, kwa watu wa Gaza, na Palestina yote, kwa zaidi ya miaka 78 ya kukaliwa kwa mabavu Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, na umbile la Kiyahudi, ni fedheha kubwa. Haiwezi kufutwa kwa shutuma tu za kuhamishwa. Watawala hawa wameficha usaliti wao mkubwa katika kipindi cha miezi kumi na tano iliyopita. Nchi kadhaa zimeelezea kukataa mipango ya kuwahamisha watu wa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina kutoka Ukanda wa Gaza, hivi karibuni Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan, ambaye alisema mnamo Jumatatu, 10 Februari, "Hakuna mtu anayeweza kuwasukuma watu wa Palestina kuelekea Nakba mpya ya uhamisho." Erdogan alisisitiza kwamba "ukaliaji kimabavu wa 'Israel' lazima ubebe gharama ya ujenzi mpya wa Gaza peke yake," akionya dhidi ya "jaribio lolote la kuwalazimisha watu wa Palestina Nakba mpya ya uhamisho."

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir Wakutana na Mkuu wa Harakati ya Wokovu wa Kitaifa

Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia inakutana na Bw. Ahmed Najib Al-Shabi, mkuu wa Harakati ya Wokovu wa Kitaifa, jana, Jumanne 11/02/2025. Mkutano huo ulifanyika katika ukumbi wa mikutano wa Hizb kwenye makao makuu ya Sakra Ariana, na uliongozwa na Bwana Al-Arabi Karbaka, mwanachama wa Hizb ut Tahrir. Mkutano huo pia ulihudhuriwa na Bw. Al-Habib Hajji, Tamim Noura, Dkt. Faisal Darghouth, na Mhandisi Yasser Al-Anwar, wanachama wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir/Wilayah Tunisia.

Soma zaidi...

Kuanguka kwa Khilafah Kunaashiria Wito wa Kuhuishwa Kwake

Mnamo tarehe 3 Machi 1924, sawia na 28 Rajab 1342 H, kikundi kidogo cha wasaliti wa Kituruki, wakiongozwa na Mustafa Kemal, walivunja urithi wa zaidi ya karne 13 za umoja wa Waislamu. Kuanzia wakati huo na kuendelea, Waislamu walipoteza paa lao juu ya vichwa vyao na wakawa mayatima. Leo, miaka 104 ya hijria imepita tangu tukio hili la kusikitisha. Baada ya kuanguka kwa Khilafah, makafiri waligawanya ulimwengu wa Kiislamu katika maeneo madogo yaliyojitenga. Waliweka vikwazo vya usafiri kati ya maeneo haya, yakihitaji pasipoti na visa, na kuharibu majeshi yetu, silaha, rasilimali, ardhi, uwezo wa binadamu, na teknolojia-kila kitu.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu