Jumatano, 04 Rajab 1447 | 2025/12/24
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kifo cha Imam Fouad Saeed Abdulkadir: Pindi Hifadhi Inapogeuka Kuwa Mkasa

Idara ya Uhamiaji na Forodha ya Marekani (ICE) imethibitisha kifo cha Fouad Saeed Abdulkadir, raia wa Eritrea mwenye umri wa miaka 46, ambaye alifariki tarehe 14 Disemba akiwa kizuizini mwa ICE katika Kituo cha Ushughulikiaji cha Moshannon Valley huko Pennsylvania. Kulingana na ICE, Imam Abdulkadir anaripotiwa kupata maumivu ya kifua na kupokea uangalizi kutoka kwa wafanyikazi wa matibabu na huduma za matibabu za dharura. Kifo chake, mojawapo ya vifo kadhaa vilivyoripotiwa katika vituo vya ICE, bado kinachunguzwa na kimeongeza uchunguzi wa hali za uzuizi na upatikanaji wa huduma za afya za kutosha kwa wafungwa.

Soma zaidi...

Kipindi cha Tarique Rahman: Purukushani ya Kisiasa Kutoka kwa Mfumo wa Kisekula Uliovunjika

Huku Bangladesh ikiingia katika awamu muhimu ya kabla ya uchaguzi, kutangazwa kwa kurudi kwa Tarique Rahman, mwana wa Waziri Mkuu wa zamani wa Bangladesh Khaleda Zia na kaimu Mwenyekiti wa Chama cha Kizalendo cha Bangladesh (BNP), kumesababisha wimbi linalotabirika la umaarufu inaozingatia shakhsiya ya mtu. Simulizi hii, iliyokuzwa kwa ukali na chama chake, inamwakilisha kama suluhisho la pekee kwa changamoto za taifa. Lazima tuone hili kwa jinsi lilivyo: udanganyifu mkubwa wa kisiasa ambao unaficha kwa hatari uhalisia msingi wa mamlaka na mfumo wa leo.

Soma zaidi...

Taarifa ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilaya ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari Wenye Kichwa: “Usimamizi wa Amerika wa Mgogoro wa Sudan Unazidisha Majeraha na Kugawanya Nchi”

Katika taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na Naibu Katibu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Balozi Muawiya Othman, kufuatia ziara ya Mwenyekiti wa Baraza la Mpito la Utawala na Kamanda wa Jeshi, Luteni Jenerali Burhan, nchini Saudi Arabia, Muawiya alisema mnamo Jumatatu jioni, 15/12/2025: “Rais alielezea shukrani zake kamili kwa azimio la Rais wa Marekani Donald Trump la kushiriki katika juhudi za kufikia amani na kukomesha vita nchini humo, kwa ushiriki wa Ufalme wa Saudi Arabia. Mheshimiwa alithibitisha nia ya Sudan kufanya kazi na Rais Trump, Waziri wake wa Mambo ya Nje, na Mjumbe wake Maalum wa Amani nchini Sudan, ili kufikia lengo hili zuri bila shaka.”

Soma zaidi...

Unafiki wa Magharibi; Kati ya Kulaani Tukio la Sydney, na Kimya Juu ya Mauaji katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina

Bado hakuna kiongozi hata mmoja wa nchi au kiongozi wa Magharibi au wa Kiarabu ambaye hajashutumu tukio la Sydney, ambapo watu kumi na tano waliuawa kwa kupigwa risasi kufuatia shambulizi lililolenga tamasha la Mayahudi la Hanukkah jijini Sydney. Hata hivyo hatujaona azma mithili ya hiyo katika kulaani jinai za umbile la Kiyahudi katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina katika kipindi cha miaka miwili iliyopita. Kama kawaida, rai jumla ya umma imepotoshwa, na kupuuzwa kabisa nia ya tukio hilo, kwani kila mtu alijikita kukemea kitendo hicho, bila kujali sababu iliyowafanya washambuliaji hao wawili kuwafyatulia risasi washerehekaji.

Soma zaidi...

Vyombo vya Usalama Vyawakamata Mashababu wa Hizb ut Tahrir kwa Kutoa Wito wa Kutibua Mpango wa Amerika wa Kutenganisha Darfur

Kikosi kutoka kwa vyombo vya usalama kiliwakamata Mashababu watano (wanachama) wa Hizb ut Tahrir katika mji wa Al-Shawak, ambao ni: Othman Al-Amin Kanda, Hassan Al-Amin Kanda, Muhammad Thamin Adam, Ahmad Babikr, na Al-Amin Abdullah. Hili lilikuja kufuatia Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan kufanya kisimamo mbele ya Msikiti wa Kale huko Al-Shawak, ambapo Sheikh Othman Al-Amin Kanda, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alihutubia hudhuri ya watu mashuhuri wa eneo hilo na umma kwa jumla. Katika hotuba yake, alielezea hatari ya mpango wa Marekani unaotaka kuigawanya Sudan kwa kuikata Darfur, akiwapa wale waliohudhuria jukumu la Kisharia linalofanya umoja wa Ummah na umoja wa dola kuwa suala nyeti. Baadhi ya watu mashuhuri walishiriki kwa kutoa kauli zinazothibitisha msimamo wao na pamoja na hizb ili kuzuia mpango wa kujitenga.

Soma zaidi...

Watawala wa Waislamu Wameshikana Mkono kwa Mkono na Marekani na Mayahudi Kupitisha Mipango Yao, Na kwa Kauli na Shutma Tupu Pamoja na Waislamu

Umbile la Kiyahudi linaendelea kutekeleza jinai zake dhidi ya Gaza, Ukingo wa Magharibi, Lebanon na Syria; kumuua limtakaye, kupiga mabomu popote lipendapo, kubomoa nyumba na vituo, kujenga makaazi, na kuwaandama watu katika nyumba na ardhi zao, huku watawala wa Waislamu wakiendelea na misimamo yao ya fedheha ya kula njama na kurahisisha mambo kwa ajili yake, wakicheza dori ya mwangalizi na mwandishi wa habari anayeripoti habari na kutoa maoni yake kwa misemo isiyozuia wala kutibua njama.

Soma zaidi...

Wakati Dola ya Kibaniani Inapozivua Niqab Kwenye Nyuso za Mabinti wa Kiislamu, Warithi wa Muhammad Bin Qasim Wako Wapi Ndani ya Jeshi la Pakistan?

Mnamo Jumatatu, 15 Disemba 2025, katika sherehe moja, Waziri Mkuu wa jimbo la India la Bihar, Nitish Kumar, aliichana niqab kutoka kwa daktari mmoja Muislamu, Nusrat Parveen. Baada ya kufanya hivyo, alicheka kana kwamba kuichana niqab hiyo kutoka kwa uso wa mwanamke wa Kiislamu ilikuwa ni mzaha. Ilhali, Mayahudi walipomfunua mwanamke mmoja wa Kiislamu na kumdhihaki hali yake, Swahaba aliyekuwepo alimuua Myahudi huyo; na Mayahudi walipomuua shahidi Swahaba huyo baadaye, Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) alizingira kabila lote, akawakamata na kuwafunga wote, na alikuwa akitoa hukumu juu yao, lakini hatimaye, baada ya maombezi, adhabu ndogo ilitolewa: kabila lote lilifukuzwa Madina. Lakini leo hakuna dola ya kulinda heshima ya Dkt. Nusrat Parveen na kumpa Baniani huyu muovu, Nitish Kumar, funzo.

Soma zaidi...

Kuvunjwa Moyo Kupya: Watu wa Gaza Wanakufa kwa Baridi Baada ya Kuachwa Kuteswa na Mauaji ya Halaiki kwa Miaka Miwili!

Maafa yanayoikumba Palestina inayokaliwa kwa mabavu yanaendelea bila kukoma. Tangu kuanguka kwa Khilafah, ambayo mtawala wake aliwahi kutamka, “Palestina ni ardhi iliyonyweshwa kwa damu ya mababu zangu, na iwapo Khilafah itaanguka, mtaichukua bila malipo,” uvamizi wa Waingereza (ulioitwa Mamlaka) uliibadilisha. Na hadi leo, umbile la Kiyahudi linaloikalia kwa mabavu, lililoundwa na Uingereza na kuungwa mkono na nchi za Magharibi kwa mali yake yote, vifaa, ujuzi na uwezo wake wote, linaendelea kuwaua watu wa ardhi iliyobarikiwa, likiwafanyia ukatili vijana na wazee, na kuwatishia wafungwa kuwaua na kuwanyonga, huku ulimwengu ukitazama. Limeizingira Gaza kwa miaka mingi, likiishambulia bila kuchoka kwa ukatili usiofikirika, na kusababisha mauaji ya zaidi ya watu elfu sabiini. Na ulimwengu wa Kiislamu, pamoja na majeshi yake na wanazuoni, hutazama na kuona kama vipofu wanavyofanya, na husikia vilio vya wanawake waliofiwa kama viziwi wanavyosikia!

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria Mkutano na Waandishi wa Habari

Tunafurahi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, kuwaalika wataalamu wa vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wanaopenda masuala ya umma kuhudhuria mkutano na waandishi wa habari ambapo Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan atazungumza chini ya kichwa: “Usimamizi wa Amerika wa Mgogoro wa Sudan: Kuongeza Majeraha na Kugawanya Nchi”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu