“Al-Wala wa-l-Bara” ni Hukmu Madhubuti ya Kiislamu na Kanuni Imara ya Kidini, na Haipaswi Kutolewa Kafara kwa ajili ya Maslahi ya Kitaifa
- Imepeperushwa katika Afghanistan
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Adam Boehler, mwakilishi wa Kizayuni wa Trump katika masuala ya wafungwa, na Zalmay Khalilzad, mjumbe wa zamani wa Marekani katika masuala ya amani nchini Afghanistan, walikutana na Amir Khan Muttaqi, waziri wa mambo ya nje wa serikali inayotawala jijini Kabul. Kufuatia mkutano huu, serikali ilimwachilia huru mfungwa wa Kimarekani kama ishara ya nia njema. Amir Khan Muttaqi alitoa wito wa "mahusiano chanya ya kisiasa na kiuchumi na Marekani." Boehler alielezea hatua hii kama hatua kuelekea "kujenga uaminifu," na Khalilzad alisema kwamba "kuachiliwa huru kwa George Glezmann ni ishara ya nia njema ya Taliban."