Ijumaa, 28 Ramadan 1446 | 2025/03/28
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

“Al-Wala wa-l-Bara” ni Hukmu Madhubuti ya Kiislamu na Kanuni Imara ya Kidini, na Haipaswi Kutolewa Kafara kwa ajili ya Maslahi ya Kitaifa

Adam Boehler, mwakilishi wa Kizayuni wa Trump katika masuala ya wafungwa, na Zalmay Khalilzad, mjumbe wa zamani wa Marekani katika masuala ya amani nchini Afghanistan, walikutana na Amir Khan Muttaqi, waziri wa mambo ya nje wa serikali inayotawala jijini Kabul. Kufuatia mkutano huu, serikali ilimwachilia huru mfungwa wa Kimarekani kama ishara ya nia njema. Amir Khan Muttaqi alitoa wito wa "mahusiano chanya ya kisiasa na kiuchumi na Marekani." Boehler alielezea hatua hii kama hatua kuelekea "kujenga uaminifu," na Khalilzad alisema kwamba "kuachiliwa huru kwa George Glezmann ni ishara ya nia njema ya Taliban."

Soma zaidi...

Marekani Yatoa Tahadhari kuhusu Alfajiri ya Khilafah Rashida kwa Njia ya Utume

Kila wakati Umma unapopiga hatua kuelekea ukombozi kutoka kwenye nira ya ukoloni unaolemea sana kifua chake, na kutaka kujikomboa kutoka kwenye himaya ya Magharibi, dola za Magharibi hutoa tahadhari, zikihofia kwamba juhudi za waumini wa kweli wa Ummah zitafikia kilele kwa kuasisiwa Khilafah Rashida, kama ilivyotolewa bishara njema na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw). Kwa hivyo, Amerika na muungano wake wa Makruseda walijipanga, baada ya kukimbia kwa dhalimu wa Syria, Bashar al-Assad, na kuingia kwa wanamapinduzi jijini Damascus. Walituma mjumbe baada ya mjumbe, wakuu pamoja na wa vyeo vya chini, wanaowakilisha serikali zao, ili kudhibiti tukio ambalo Amerika na muungano wake wa Makruseda walikadiria kuwa muhimu. Endapo maji yatazidi unga, matokeo hayatakuwa mazuri kwa makafiri.

Soma zaidi...

Wakati wa Ziara yake nchini India, Tulsi Gabbard katika Taarifa yake Alieleza Kujitolea kwa Ushirikiano wa Marekani na India na Mapambano dhidi ya Uislamu na Waislamu

Ingawa maoni ya chuki yaliyotolewa na Mkuu wa Ujasusi wa Kitaifa wa Kruseda Amerika, Tulsi Gabbard wakati wa ziara yake nchini India juu ya mateso ya watu walio wachache nchini Bangladesh na 'Khilafah ya Kiislamu' hayakuwashtua watu wanaozingatia siasa na wapenda Uislamu wa nchi hii, yaliondoa aibu ya mwisho ya vibaraka wa Amerika nchini Bangladesh. Kwa sababu vibaraka hawa walikuuza kukubalika kusiko epukika kwa Amerika kama rafiki wa Bangladesh ili kukabiliana na India na kuwahakikishia watu wapenda Uislamu wa nchi hii kwamba Amerika ilikuwa imeacha sera ya "vita dhidi ya Uislamu". Ingawa ukweli ni kwamba, hata kama uongozi wa Amerika utabadilika, 'sera yao ya kigeni' haibadilika. Badala yake, Trump shupavu au utawala wake hupenda kuwatusi vibaraka wake na kufichua nia za ‘sera zao za kigeni’. Kwa hili ametaka uwajibikaji wa dolari milioni 29 ambazo zililipwa kwa vibaraka ili kubadilisha mazingira ya kisiasa ya Bangladesh, huku kutumia pesa kama hizo kudhibiti siasa za nchi huru ni uhalifu mkubwa na ni sawa na kuingilia masuala ya ndani ya nchi nyingine.

Soma zaidi...

Marekani Yaanzisha Mashambulizi ya Kikatili kwa Yemen Huku Majeshi Yetu Yakitulia tuli, Yakishindwa Kuinusuru Yemen na Gaza!

Kwa siku nyingi sasa, Amerika imekuwa ikianzisha mashambulizi ya kikatili kwa watu wetu nchini Yemen, kwa kutumia kile Rais wa Marekani Trump alichoeleza kuwa "nguvu kuu mbaya." Alikuwa amewatisha hapo awali, akichapisha, “JAHANAM ITANYESHA JUU YENU KWA NAMNA AMBAYO KWAME HAMJAWAHI KUONA KABLA!!”

Soma zaidi...

Doria ya Pamoja ya 'CORPAT' na Adui India na Zoezi la Pande Mbili 'Bangosagar' Inathibitisha kuwa Vibaraka wa Marekani-India Wanacheza na Ubwana wa Nchi kwa Maslahi ya Mabwana zao Wakoloni

Moja ya sababu zilizomfanya msaliti Hasina kupinduliwa na watu ni kwamba alitekeleza njama ya India kule Pilkhana na mara kwa mara alifanya majaribio mabaya yote ya kuweka udhibiti wa India juu ya jeshi la nchi hiyo. Wakati ambapo wananchi wanapaza sauti kudai haki kwa mkasa wa Pilkhana, doria ya pamoja 'CORPAT' na zoezi la pande mbili 'Bangosagar' lililofanyika katika Ghuba ya Bengal kwa kushirikisha jeshi la wanamaji la Bangladesh na India imewashtua watu. Kwa kweli, vibaraka wa Marekani-India wamedhamiria kulinda maslahi ya kijiografia ya wakoloni wao hata kwa gharama ya ubwana wa nchi. Inafaa kutaja kwamba wakati matabaka ya kisiasa ya kisekula ya nchi hayakupaza sauti yake dhidi ya njama hiyo ya Pilkhana, ni Hizb ut Tahrir pekee ndiyo iliyofichua njama hiyo mbele ya taifa hilo kwa ushujaa na kupinga njama hiyo dhidi ya ubwana wa nchi hii.

Soma zaidi...

Aqida ya Kiislamu Pekee ndiyo Msingi wa Dola, Katiba, na Sheria Lengo ni Uislamu Uingie Madarakani na sio Kutosheka na Muislamu Kuingia Madarakani

Uislamu umetuwajibisha kuifanya Aqiyah (itikadi) ya Kiislamu kuwa msingi wa dola, na wakati huo huo, msingi wa katiba na sheria. Yaani, chanzo pekee cha sheria. Haupaswi kuambatanishwa na vyanzo vyengine vya sheria, kama ilivyo katika katiba zilizotungwa na mwanadamu; baadhi yazo zinadai kwamba Uislamu ndio chanzo kikuu au chanzo msingi cha sheria, huku kiuhalisia wanaazima sheria ngeni kwetu kutoka Magharibi.

Soma zaidi...

Kuanzia Mjumuiko wa “Matembezi kwa ajili ya Khilafah” yalioandaliwa na Hizb ut Tahrir, watu wanaopenda Uislamu wanawaita watoto wao wa kiume katika jeshi kujitokeza ili kusimamisha Khilafah kwa njia ya Utume; Na ili kuiridhisha Marekani na India, vib

Kwa mnasaba wa kumbukumbu ya miaka 101 tarehe 3 Machi, 2025, ya kuondolewa kwa Khilafah tukufu, Hizb ut Tahrir, Wilayah Bangladesh, iliandaa mjumuiko wa “Matembezi kwa ajili ya Khilafah” mnamo siku ya Ijumaa, Machi 7, 2025, baada ya Ijumaa, kutoka kwenye Lango la Kaskazini la Baitul, wakitaka kusimamishwa kwa Khilafah kwa njia ya Utume. Maelfu ya watu wanaopenda Uislamu kutoka matabaka mbalimbali walishiriki kwa hiari katika mjumuiko huu, wakipuuza vitisho vya vibaraka wa Marekani-India. Kutokana na mkusanyiko huu, watu wanaopenda Uislamu waliwaita watoto wao wanaotumikia jeshi kutoa nusrah (msaada wa kimada) kwa uongozi wa dhati wa Hizb ut Tahrir, katika kusimamisha Khilafah kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Amerika Yala Sanamu Lake Yenyewe!

Katika Arabuni ya kabla ya Uislamu, baadhi ya Waarabu walikuwa wakitengeneza masanamu yao kutokana na tende; walipohisi njaa, wangekula miungu yao! Leo, historia inajirudia yenyewe, lakini kwa umbo gumu zaidi. Mfumo wa Kimagharibi ambao hapo awali uliinyanyua fahamu ya uhuru hadi kwenye hadhi takatifu—uhuru wa fikra, dhamiri, na dini; uhuru wa kuzungumza na kujieleza; uhuru wa kukongamana kwa amani; ushiriki wa kisiasa; ulinzi wa haki za walio wachache; na kukataza utesaji na kutendewa kikatili – sasa unasaliti maadili haya haya yanapokinzana na maslahi ya mabepari na kipote cha watawala.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu