Ijumaa, 11 Dhu al-Qi'dah 1446 | 2025/05/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hatua Mpya za UN na za Kanda za Kuoanisha Serikali Tawala ya Afghanistan ndani ya Mfumo wa Kisekula wa Dunia

Katika siku za hivi karibuni, Umoja wa Mataifa umekuwa ukifuatilia shughuli zake nchini Afghanistan kwa kasi zaidi kuliko hapo awali. Ziara ya Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Masuala ya Kibinadamu jijini Kabul na Kandahar, pamoja na mwaliko wa Amir Khan Muttaqi-Waziri wa Mambo ya Nje wa serikali tawala nchini Qatar, inaashiria juhudi mpya za kuendeleza mipango ya kimataifa na kushawishi serikali ya Afghanistan.

Soma zaidi...

Mkondo wa Bahari wa Suez: Mtazamo kwa Kauli za Trump na Msimamo wa Utawala wa Misri

Katika onyesho jengine la kiburi, Rais wa Marekani Donald Trump alitangaza kwenye jukwaa la "Ukweli wa Kijamii" kwamba meli za Kimarekani zinapaswa kupita kwenye Mikondo ya Suez na Panama bila malipo, akidai kwamba Marekani "iliunda mikondo yote miwili." Alimteua Waziri wake wa Mambo ya Nje kufuatilia makubaliano ambayo yataasisisha matakwa haya ya kikoloni.

Soma zaidi...

Kisimamo cha Kulaani cha Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Lebanon jijini Beirut “Kutoka Beirut hadi Gaza, Kuweni Answari wa Mwenyezi Mungu, Enyi Majeshi ya Ummah”

Mamia ya Mashababu (wanachama) na wafuasi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Lebanon walishiriki katika kisimamo cha kulaani kilichoitishwa na Hizb, baada ya swala ya Ijumaa mnamo tarehe 25/4/2025, jijini Beirut, mbele ya Msikiti wa Mohammad Al-Amin. Kisimamo hicho kilikuwa na kichwa “Kutoka Beirut hadi Gaza, Kuweni Answari wa Mwenyezi Mungu, Enyi Majeshi ya Umma,” ambapo mabango yalinyanyuliwa yakitaka kuhamasishwa kwa majeshi, kupinduliwa kwa viti vya utawala vya madhalimu, na kunusuriwa kwa Gaza kupitia jihad na silaha.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Kenya Yafanya Kisimamo cha kutoa Wito wa Amali ya Kijeshi dhidi ya Umbile la Mauaji ya Halaiki la Kiyahudi

Kufuatia mauaji ya halaiki yanayoendelea kufanywa na umbile la Kiyahudi dhidi ya watu wa Gaza, Hizb ut Tahrir/Kenya mnamo siku ya Ijumaa tarehe 18 Aprili, ilifanya ilifanya kisimamo baada ya Swala ya Jumaa jijini Mombasa na Nairobi. Katika Jiji la Pwani, kisimamo kilifanyika nje ya Masjid Nur huku Nairobi kikifanyika katika Masjid Hidaya mtaa wa Eastleagh. Mada kuu ya Kisimamo ilikuwa ni kuibua wito wa dhati kwa Majeshi katika nchi za Kiislamu kuvunja minyororo ambayo watawala wao wamewaweka katika kambi zao ili wasonge mara moja kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa kutoka katika makucha ya Mayahudi wanaoukalia kwa mabavu.

Soma zaidi...

Farauni wa Washington Afanya Maangamizu Makubwa Gaza, Kwa Usaidizi Kamili wa Viongozi wa Kijeshi na Kisiasa wa Waislamu na Mayahudi. Jibu Pekee la Kisharia ni Uhamasishaji wa Majeshi ya Waislamu. Enyi Waislamu! Songeni kwa ajili ya Faradhi ya Kishar

Bila jeshi hata moja la Waislamu kumzuia, Trump alitimiza ahadi yake ya kufanya maangamizi makubwa Gaza. Kamera zimenasa picha za sehemu za miili ya waumini zikipaa angani, juu ya majengo marefu, kutokana na kukithiri kwa mashambulizi ya makombora. Madaktari wa uokoaji wanafunikwa macho na kupigwa risasi. Watoto, wanawake, wazee na waliojeruhiwa wanauawa shahidi kwa kulipuliwa mahema yao. Sera ya njaa ya Amerika, iliyotekelezwa na wafuasi wake, umbile la Kiyahudi, imeongeza mateso hadi kiwango cha baa la njaa. Sasa imedhihirika kwa kila mtu kwamba Firauni wa Washington anafanya maangamizi makubwa kwa Gaza, kwa usaidizi kamili wa kijeshi na uongozi wa kisiasa wa Waislamu na Mayahudi.

Soma zaidi...

Tangazo la Matokeo ya Kuutafuta Mwezi Muandamo wa Shawwal 1446 H Pongezi kwa Idd Al-Fitr Iliyobarikiwa

Ummah umepitia mateso ya kubaki chini ya nira ya tawala za vibaraka. Umeshuhudia kwa macho yake wenyewe watawala wakifuja mali zake kwa makafiri, wakoloni wa Magharibi, kuzitelekeza kwao na sababu zake, kuzuia kwao majeshi kusonga ili kuinusuru Palestina kutoka kwenye makucha ya Mayahudi wahalifu, uingiliaji wa wazi wa Magharibi katika dini yake na uadilifu wake, na jaribio la kuulazimisha kulishuhudia  umbile la Kiyahudi, na kuuacha na chaguo kati ya uhalalalishaji mahusiano au kifo. Mandhari na matukio haya yote yameufanya utambue kwamba bila ya utawala wa Uislamu, utabakia kukoloniwa, kulengwa, na kudhalilishwa. Kukinaika kwake kwa haja ya dola ya Khilafah kumeimarishwa, na kwa hakika, Khilafah imekuwa ni kiu yake.

Soma zaidi...

Umbile la Kiyahudi Linatekeleza Mauaji ya Halaiki na Unyanyasaji wa Kijinsia mjini Gaza. Je, Kuna Njia ya Kuamsha Uzembe Huu?

Tangu kutekelezwa Operesheni ya Kimbunga cha Al-Aqsa mnamo 7 Oktoba 2023, umbile la Kiyahudi limewatenga watu walio na msimamo thabiti wa Gaza na kumwaga chuki yake juu yao. Limefanya mauaji ya mfululizo ambayo yamesababisha makumi ya maelfu kuuawa shahidi, huku Umma wa Kiislamu ukiwa bado umefungwa pingu na majeshi yake yamenyamaza kimya kama watu wa makaburini! Lilianza tena mauaji yake baada ya kukiuka usitishaji vita, kwa uungaji mkono wa wazi wa Magharibi na ushirikiano wa wazi na wa aibu wa tawala angamivu katika nchi za Waislamu.

Soma zaidi...

Leo Gaza na Yemen, na Kesho nchi zengine za Waislamu, Isipokuwa Majeshi yao Yatangaze Kusonga

Kamandi Kuu ya Ulinzi ya Marekani (CENTCOM) ilitangaza kwamba jioni ya Jumamosi, 15 Machi 2025, ilianzisha msururu wa mashambulizi ya anga dhidi ya maeneo lengwa ya Mahouthi nchini Yemen. Ilidai kuwa ilifanya mashambulizi sahihi dhidi ya maeneo lengwa ya kundi hilo kote Yemen, ikihalalisha mashambulizi hayo kama utetezi wa maslahi ya Marekani, kuzuia dhidi ya maadui, na kuregesha uhuru wa bahari, kulingana na taarifa yake. Kufikia Alhamisi jioni, Machi 20, makumi ya mashambulizi ya anga ya Marekani dhidi ya Yemen yalikuwa yameripotiwa, na kusababisha vifo vya watu 53 na wengine zaidi ya 100 kujeruhiwa, wengi wao wakiwa wanawake na watoto. Kuna matarajio kwamba operesheni zitaendelea kwa wiki kadhaa. Haya ni mashambulizi ya kwanza dhidi ya Yemen tangu makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya umbile la Kiyahudi na Hamas mjini Gaza Januari iliyopita, kufuatia kiapo cha Trump cha "kuwamaliza kabisa."

Soma zaidi...

“Al-Wala wa-l-Bara” ni Hukmu Madhubuti ya Kiislamu na Kanuni Imara ya Kidini, na Haipaswi Kutolewa Kafara kwa ajili ya Maslahi ya Kitaifa

Adam Boehler, mwakilishi wa Kizayuni wa Trump katika masuala ya wafungwa, na Zalmay Khalilzad, mjumbe wa zamani wa Marekani katika masuala ya amani nchini Afghanistan, walikutana na Amir Khan Muttaqi, waziri wa mambo ya nje wa serikali inayotawala jijini Kabul. Kufuatia mkutano huu, serikali ilimwachilia huru mfungwa wa Kimarekani kama ishara ya nia njema. Amir Khan Muttaqi alitoa wito wa "mahusiano chanya ya kisiasa na kiuchumi na Marekani." Boehler alielezea hatua hii kama hatua kuelekea "kujenga uaminifu," na Khalilzad alisema kwamba "kuachiliwa huru kwa George Glezmann ni ishara ya nia njema ya Taliban."

Soma zaidi...

Marekani Yatoa Tahadhari kuhusu Alfajiri ya Khilafah Rashida kwa Njia ya Utume

Kila wakati Umma unapopiga hatua kuelekea ukombozi kutoka kwenye nira ya ukoloni unaolemea sana kifua chake, na kutaka kujikomboa kutoka kwenye himaya ya Magharibi, dola za Magharibi hutoa tahadhari, zikihofia kwamba juhudi za waumini wa kweli wa Ummah zitafikia kilele kwa kuasisiwa Khilafah Rashida, kama ilivyotolewa bishara njema na Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw). Kwa hivyo, Amerika na muungano wake wa Makruseda walijipanga, baada ya kukimbia kwa dhalimu wa Syria, Bashar al-Assad, na kuingia kwa wanamapinduzi jijini Damascus. Walituma mjumbe baada ya mjumbe, wakuu pamoja na wa vyeo vya chini, wanaowakilisha serikali zao, ili kudhibiti tukio ambalo Amerika na muungano wake wa Makruseda walikadiria kuwa muhimu. Endapo maji yatazidi unga, matokeo hayatakuwa mazuri kwa makafiri.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu