Jumapili, 26 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/22
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kati ya Usaliti wa Palestina na Kashmir na Utumwa kwa Amerika Asim Munir Anafanya Nini Mbele ya Firauni Wa Zama Zetu, Trump?

Katika wakati ambapo Amerika inapigana vita dhidi ya jirani Muislamu, Iran, kwa kutumia mkono wake mchafu katika eneo hilo, umbile la Kiyahudi, Rais wa Marekani, Donald Trump, alimkaribisha Mkuu wa Majeshi wa Pakistan mnamo Jumatano, 18 Juni 2025, kwa chakula cha mchana katika mkutano ambao haujawahi kushuhudiwa katika Ikulu ya White House. Kinachotia shaka kuhusu mkutano huu, na muda wake, ni kwamba ni mara ya kwanza kwa rais wa Marekani kumkaribisha mkuu wa jeshi la Pakistan katika Ikulu ya White House, bila ya kuwepo kwa afisa yeyote mkuu wa kiraia wa Pakistan, kuashiria umuhimu wa mkutano huo, na unyeti wa mada yake.

Soma zaidi...

Kuharibu Masoko kama vile Soko la Dokhinat ni Vita dhidi ya Watu katika Riziki zao na ni Matokeo ya Kukosekana kwa Dola ya Kiislamu ya Khalifah

Katika kitendo cha kikatili na vurugu, mamlaka za eneo la Jabal Awlia, Jimbo la Khartoum, kwa kutumia askari waliokuwa na silaha nyingi, walibomoa Soko la Tumbaku lililoko kwenye Barabara ya Jabal Awlia kwa tingatinga mnamo siku ya Alhamisi asubuhi, 12 Juni 2025, na kuvunja meza za maonyesho. Hata wale waliotoroka soko hilo na bidhaa zao hawakusazwa!

Soma zaidi...

Tahadharini kwamba Kuondelewa Vikwazo vya Marekani kunaweza kuwa Utangulizi wa Kupoteza Ubwana na Utangulizi wa Uhalalishaji Mahusiano na Mayahudi

Rais wa Syria Ahmed al-Sharaa alikutana na mwenzake wa Marekani, Donald Trump, katika mji mkuu wa Saudi, Riyadh, mnamo Jumatano, kando ya mkutano wa kilele wa Ghuba na Marekani. Mfalme matarajiwa wa Saudia Mohammed bin Salman alihudhuria mkutano huo, huku Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdoğan akishiriki kwa njia ya video, kwa mujibu wa vyombo vya habari vya Saudia.

Soma zaidi...

Enyi Waislamu! Msidharau Matendo Yenu Wenyewe kwa Kuangalia Matendo ya Watu! Kwa sababu Nyinyi Ni “Mashahidi” Juu ya Wanadamu!

Meli ya misaada ya "kwenda Gaza" ya Madleen na matendo ya wanaharakati wake maarufu wasio Waislamu yamekuwa na athari kubwa kwenye vyombo vya habari vya kawaida na mitandao ya kijamii. Nchi nyingi, ikiwemo Uturuki, zilitoa "msaada wa ushauri" kwa raia wao wenyewe kwenye meli hiyo, ambayo ilikamatwa na umbile vamizi la kigaidi la kizayuni.

Soma zaidi...

Utawala wa Jordan Unalilinda Umbile Adui la Kiyahudi kwa Kuyapangua Makombora na Droni Zinazoelekezwa kwake

Mnamo siku ya Ijumaa, tarehe 13/6/2025, alfajiri, umbile la Kiyahudi lilianzisha mashambulizi dhidi ya Iran, yakilenga vituo vyake vya nyuklia, viwanda vyake vya makombora ya balestiki, na viongozi wa kijeshi, na kusababisha uharibifu mkubwa kwa maisha na mitambo ya kijeshi na ya kiraia, kwa msaada na ushirikiano wa Marekani. Iran, kama kawaida, iliapa kutoa jibu kali na baya kwa umbile la Kiyahudi kupitia mashambulizi ya droni na makombora. Ilitekeleza mawimbi ya mashambulizi haya asubuhi na jioni ya siku hiyo hiyo, yakivuka anga ya Iraq, Syria, na Jordan. Baadhi ya mashambulizi haya yalisababisha uharibifu kwa baadhi ya vifaa katika miji ya umbile hilo, kabla ya baadhi yake kupanguliwa katika anga ya jirani kabla na baada ya kufika kwenye umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Utelekezaji wa Serikali ya Misri wa Gaza: Kuanzia Kuzuia Nusra, Hata wa Maneno, hadi Kushiriki kwa Kizuizi!

Katika mandhari inayojirudia rudia, kwa kila maafa yanayowakumba watu waliozingirwa wa Gaza, tawala za Kiarabu - zinazoongozwa na utawala wa Misri - zinathibitisha kwamba sio tu hazipo katika wajibu wao wa kunusuru, lakini pia ziko katika nafasi ya ulaji njama na usaliti, na hata kushiriki kikamilifu katika mzingiro, kulinda vivuko na kuzuia mradi wowote wakilishi au maarufu kwa lengo la kukandamiza Waislamu.

Soma zaidi...

Afisi ya NATO nchini Jordan: Kujisalimisha kwa Nchi na Kuahidi Kutumikia Maslahi ya Kikoloni ya Maadui wa Ummah

Mnamo siku ya Alhamisi, 12 Juni 2025, Jordan na Shirika la Mkataba wa Atlantiki ya Kaskazini (NATO) walitia saini makubaliano jijini Brussels ili kuwa mwenyeji wa afisi ya mawasiliano ya kidiplomasia ya muungano huo katika mji mkuu, Amman. Makubaliano hayo yalitiwa saini kwa niaba ya Jordan na Balozi Yusuf Bataineh, balozi aliyeidhinishwa katika NATO, na kwa niaba ya muungano huo na Javier Colomina, Mwakilishi Maalum wa NATO kwa jirani wa Kusini, ambaye alisifu uhusiano uliotukuka na Jordan na kuthamini ukaribishaji wa afisi ya Jordan na dori yake kuu katika kanda, akiizingatia kuwa mshirika wa kutegemewa kwa muungano huo katika nyanja tofauti tofauti.

Soma zaidi...

Kongamano la Amani ya Kiraia jijini Damascus Utangulizi wa Kuwaondoa Watiifu wa Serikali na Kuhalalisha Nembo za Ukandamizaji na Uhalifu

Mkutano na waandishi wa habari uliofanywa na Kamati ya Amani ya Kiraia katika jengo la Wizara ya Habari jijini Damascus mnamo Jumanne, Juni 10, 2025, chini ya uenyekiti wa mwanakamati Hassan Soufan, ulizua wimbi kubwa la hasira na chuki kubwa miongoni mwa Wasyria, hasa miongoni mwa familia za mashahidi na waliopotea, na watoto wa mapinduzi. Wengi waliona kauli za mkutano huo kama uchochezi kwa familia za wahasiriwa, kupuuza mihanga ya wanamapinduzi, kudharau damu ya mahsahidi, kukana ukweli usiopingika, na uhalalishaji wa wazi wa wahalifu wa kivita. Hafla hiyo ilionekana kama jaribio la kulalalisha mahusiano kwa nembo za utawala ulio ng’atuliwa chini ya mabango ya "amani ya raia," "kujenga taifa," na "kuzuia umwagaji damu."

Soma zaidi...

Pongeza kutoka kwa Hizb ut Tahrir / Wilayah Iraq kwa Sikukuu ya Idd al-Adha 1446 H

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir / Wilayah Iraq inatoa pongezi na baraka zake nyingi kwa Umma wa Kiislamu kwa mnasaba wa Idd al-Adha iliyobarikiwa. Hasa tunatoa salamu hizi kwa wabebaji da’wah, na kwa mwanachuoni mkubwa, Amiri wa Hizb utTahrir, Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah Mwenyezi Mungu amlinde na amhifadhi na ampe ushindi na tamkini kupitia mikono yake.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen Inawapongeza Watu wa Imani na Hekima na Umma wa Kiislamu kwa Sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa

Hizb ut Tahrir / Wilayah Yemen inatoa pongezi zake za dhati na baraka zenye thamani kubwa zaidi kwa watu wa imani na hekima, na kwa Amiri wa Hizb, mwanachuoni mkubwa Ata Bin Khalil Abu Al-Rashtah, na kwa wanachama wote wa Hizb, na kwa Ummah mzima wa Kiislamu kwa sikukuu ya Idd al-Adha iliyobarikiwa mwaka huu wa 1446 H. Mwenyezi Mungu airudishe kwao, juu yetu, na juu ya ulimwengu wote kwa kheri, baraka, na furaha.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu