Alhamisi, 16 Jumada al-awwal 1447 | 2025/11/06
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Katikati ya Mashambulizi ya Marekani kwa ajili ya Kuhalalisha Mahusiano na Kusalim Amri! Ziara Nyingine ya Mara kwa Mara ya Mjumbe wa Marekani Ortagus nchini Lebanon!

Kwa kuzingatia mashambulizi ya Marekani dhidi ya Lebanon na eneo hili pamoja na mradi wa kuhalalisha mahusiano na kusalim amri, na juhudi za utawala wa Trump na timu yake kuwaleta watawala zaidi wa Waislamu katika Makubaliano ya Abraham, inakuja ziara ya mjumbe wa Marekani Morgan Ortagus nchini Lebanon na umbile nyakuzi la Kizayuni, iliyojaa shinikizo, vitisho, na hali za kisiasa, usalama, na kiuchumi zilizolazimishwa nchini Lebanon. Ziara hii iliambatana na ziara ya Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kiarabu na Mkurugenzi wa Ujasusi wa Misri, ikionekana kutimiza lengo moja!

Soma zaidi...

Himaya Yashambulia Gaza - Sami Hamdi na Kifo cha Upinzani

Baada ya umbile la Kizayuni kuifahamisha Marekani kuhusu uamuzi wake wa kuanza tena operesheni zake za uhalifu mjini Gaza, zaidi ya wakaazi 109 wa Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina - wakiwemo watoto 46 - waliuawa shahidi, na wengine wengi walijeruhiwa tangu Jumanne jioni, 28 Oktoba 2025, katika mashambulizi ya anga yaliyofanywa kote Ukanda wa Gaza. Mabomu hayo yalilenga nyumba za raia na shule inayowahifadhi watu waliokimbia makaazi yao huko Beit Lahia, kaskazini mwa Gaza.

Soma zaidi...

Mtu Anayehusika na Usalama wa Watu Anawezaje Kukimbia Akitafuta Usalama?!

Sudan News ilinukuu Darfur 24 katika ripoti moja yenye kichwa: “Kujiondoa kwa Uratibu au Kuanguka?! Makamanda na Maafisa wa Jeshi na Vikosi vya Pamoja Waondoka Al Fasher Siku Mbili Kabla ya Kuanguka Kwake,” ikisema: “Vyanzo viwili kutoka Darfur Kaskazini viliifichulia Darfur 24 kwamba makamanda wa jeshi, pamoja na wanachama wa vikosi vya pamoja, gavana wa Darfur Kaskazini, Al-Hafiz Bakhit, na wanachama kadhaa wa serikali yake, waliondoka Al Fasher siku mbili kabla ya Vikosi vya Msaada wa Haraka kutangaza udhibiti wao kamili wa makao makuu ya Kikosi cha 6 cha Wanajeshi Wapiganaji.”

Soma zaidi...

Uvamizi wa Waliolaaniwa Haukomi Je, kuna kiongozi anayeongozwa na Mungu ambaye atakomesha

Uvamizi dhidi ya Gaza unajirudia kama kile ambacho afisi ya mhalifu Netanyahu ilikiita “mashambulizi makali katika Ukanda wa Gaza” (Al Jazeera), ikidai kwamba Hamas ilifanya shambulizi dhidi ya wanajeshi wake katika Ukanda wa Gaza na kujibu uvunjaji wa makubaliano ya kuregesha miili - ingawa Hamas ilikana uhusiano wake na tukio la ufyatuaji risasi (Al Jazeera). Umbile hilo liliwaua zaidi ya mashahidi hamsini ndani ya masaa, huku likidai kwamba mashambulizi hayo hayamaanishi kuvunjika kwa makubaliano ya kusitisha mapigano! Na Trump anathibitisha kwamba mashambulizi ya Mayahudi hayatahujumu usitishaji mapigano!

Soma zaidi...

Kupiga Kura Ndani ya Mfumo wa Kisekula Kunapelekea Kuoanishwa

Mara nyingi zaidi, maimamu, mabaraza, na viongozi wa kidini huwataka Waislamu nchini Uholanzi kupiga kura kwa wingi na kushiriki katika mchezo wa kisiasa wa mfumo wa kisekula. Mfumo ambao, kutoka asili na kiini chake, unapinga Uislamu, unautenga, na kujaribu kuudogosha hadi kitu kilichofungwa kwenye msikiti au sebule.

Soma zaidi...

Mwaliko wa Kuhudhuria na Kushiriki katika Kikao cha Masuala ya Ummah

Sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah Sudan, tuna furaha kuwaalika ndugu zetu wanahabari, wanasiasa, na wale wenye hamu na masuala ya umma kuhudhuria na kushiriki katika kikao cha kila mwezi cha masuala ya Umma, ambacho mwezi huu kitakuwa kwa kichwa: El Fasher: Kituo Kilicho na Vurugu Zaidi katika Mzozo wa Kimataifa wa Sudan

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Lebanon Wamemtembelea Mheshimiwa Mbunge Dkt Osama Saad

Kwa kuzingatia shambulizi la Marekani dhidi ya Lebanon na kanda hii kupitia uhalalishaji mahusiano na kujisalimisha, na juhudi za Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Lebanon kuzuia shambulizi hili, ujumbe kutoka hizb, ukiwakilishwa na wanachama wa Kamati Kuu ya Mawasiliano na Kamati ya Amali katika Eneo la Kusini, ulimtembelea Mheshimiwa Mbunge Dkt. Osama Saad afisini kwake Sidon mnamo Jumatatu, 27/10/2025.

Soma zaidi...

Wewe Ndiye Uliyewaletea Waislamu Njaa, Masoud Pezeshkian!

Iran ilitangaza kufilisika kwa benki yake kubwa zaidi ya kibinafsi, Benki ya Ayandeh, ambayo ina matawi 270 nchini Iran, baada ya madeni yake kupanda zaidi ya dolari bilioni tano, na kinachoshangaza ni ukosoaji wa rais wa Iran Masoud Pezeshkian kuhusu kushindwa kwa utawala akisema: “Tuna mafuta na gesi lakini tuna njaa”!

Soma zaidi...

Watawala wa Pakistan, Watu wa Trump, Wawateka nyara Mashababu wa Hizb ut Tahrir ili Kuhakikisha Kujisalimisha kwa Palestina

“Jenerali kipenzi cha Trump,” Asim Munir, amejibu kwa udhalimu kampeni yenye nguvu ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Pakistan, ambayo kwayo inataka uhamasishwaji wa haraka wa Vikosi vya Jeshi la Pakistan ili kuikomboa Palestina. Majambazi wa Asim Munir wamewateka nyara matetezi watano, kutoka Lahore, Karachi na Peshawar, na mahali walipo hapajulikani. Udhalimu wa Asim Munir unatarajiwa. Asim Munir hawezi kutenda, sembuse kufikiria, nje ya maagizo ya Trump katika suala lolote, iwe kuhusu Gaza, Kashmir, Afghanistan au rasilimali kubwa za madini za Pakistan.

Soma zaidi...

Watawala wa Waislamu Hawana Sifa za Kulinda Heshima ya Waislamu!

Vyombo vya habari viliripoti kwamba Rais wa Marekani Donald Trump alicheza densi kwenye zulia jekundu kwenye uwanja wa ndege nchini Malaysia mnamo Jumapili, 26/10/2025, alipopokewa na Waziri Mkuu wa Malaysia. Idadi ya Wamalaysia, wanaume na wanawake, walipunga bendera za Marekani na kucheza muziki wa kienyeji ili kumkaribisha mhalifu huyo muuaji ambaye mikono yake imejaa damu ya Waislamu wa Gaza.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu