Jumapili, 22 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/14
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Chuki na Uhalifu wa umbile la Kiyahudi mjini Gaza na Yemen Haitakomeshwa isipokuwa kwa Khilafah Rashida ya Pili kwa Njia ya Utume, Mlinzi wa Matukufu ya Waislamu

Kulengwa kwa Yemen na umbile la Kiyahudi kusingetokea isipokuwa kwa kukosekana utawala wa Uislamu, na kutabanniwa kwa sheria ya kimataifa inayowakilishwa na Umoja wa Mataifa na wale walio nyuma yake kama kibla chao, na malipo kama hayo ya kuacha kutawala na Uislamu ni matokeo ya kutarajiwa tu – hadi wanasiasa wa Yemen waregee kwenye fahamu zao na kuuweka Uislamu katika utabikishaji ndani ya Khalifah ya pili kwa njia ya Utume.

Soma zaidi...

Enyi Watu wa Sudan, Mnaweza Kutibua Mpango wa Kuitenga Darfur, Basi Inukeni Kumtii Mwenyezi Mungu!

Katika hatua inayotarajiwa, kamanda wa Vikosi vya Msaada wa Haraka, Mohamed Hamdan Dagalo, alikula kiapo cha kikatiba kama mkuu wa Baraza la Rais la kile kinachoitwa serikali sambamba huko Nyala, mji mkuu wa Darfur Kusini, mnamo Jumamosi, 30/8/2025. Makamu wa Rais, wajumbe wa Baraza la Rais, na Waziri Mkuu pia walikula kiapo.

Soma zaidi...

Mwisho wa Uvamizi wa Kijeshi wa Marekani na NATO: Fursa ya Kukabiliana na Ukoloni Laini na Hatua ya Kuelekea Khilafah kwa Njia ya Utume!

Miaka minne iliyopita, mnamo 31 Agosti 2021, uvamizi wa kijeshi wa miongo miwili wa Afghanistan na vikosi vya Amerika na NATO ulimalizika, kwani mwanajeshi wa mwisho wa Amerika aliondoka nchi humu usiku wa manane. Hii ilikuwa hasa kwa sababu ya mhimili wa Wamarekani kuelekea Indo-pacifiki, kupunguza kasi ya maendeleo ya China. Nchi za Kiislamu, hususan Mujahidina wa Afghanistan walikuwa wamewaumiza kichwa Wamarekani na kukengeushwa na mkakati huu mpya. Tunatoa pongezi zetu kwa mafanikio haya ya kihistoria na siku kuu kwa Waislamu wote, hasa kwa watu wa Afghanistan, wabebaji Dawah, na Mujahidina.

Soma zaidi...

Miradi ya Wamarekani – Mayahudi ni Miradi ya Jinai na Uhaini, Iwe Inatekelezwa na PLO au Wengine

Chaneli 5 ya Kiebrania, kama ilivyoripotiwa na Al Jazeera, ilitangaza ripoti iliyosema kwamba Netanyahu anafanya mkutano kujadili kuchukua nafasi ya Mamlaka ya Palestina pamoja na viongozi wa kikabila huko Al-Khalil (Hebron). Taarifa ilitolewa baadaye na Gavana wa Al-Khalil (katika kujibu mashauri yanayoendelea ya serikali ya uvamizi kuhusu kuitenganisha Al-Khalil kutoka kwa jiografia ya kitaifa na kuikabidhi kwa utawala wa kikabila).

Soma zaidi...

Watu wa Al-Fashir Baina ya Nyundo ya Vita na Kinoo cha Njaa, na Hawana Wokovu isipokuwa kwa Dola ya Khilafah

Mji wa Al-Fashir, mji mkuu wa Jimbo la Darfur Kaskazini, unashuhudia janga halisi la kibinadamu, huku kukiwa na vita kati ya pande zinazopigana, ambapo makumi ya raia waliuawa katika siku chache zilizopita, huku wakaazi wakiteseka kutokana na kuzingirwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, na njaa ya makusudi, katika kivuli cha kimya cha kituliwa shaka cha kimataifa, huku Umoja wa Mataifa ukithibitisha mauaji ya angalau watu 89 katika mapigano ya siku zilizopita.

Soma zaidi...

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Taqli Watoa Wito Mkali kwa Waislamu Kutibua Mpango wa Marekani wa Kutenganisha Darfur

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/ Wilayah Sudan ya kukwamisha mpango wa kuisambaratisha Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kuzingatia umoja wa Ummah kama suala nyeti, suala la uhai na kifo, wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi' al-Awwal 1447 H sawia na 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Sheikh Yahya kituo cha kuhifadhi Quran. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa matabaka yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, wanazuoni, maafisa na askari na wengineo, wakiwahimiza kutimiza wajibu wao wa kidini ili kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Soma zaidi...

Msamaha Mbele ya Mola Wetu, na Pole kwa Waliojeruhiwa Gaza Tripoli ash-Sham Yapaza Sauti Yake Dhidi ya Sherehe za Kucheza juu ya Majeraha ya Umma!

Hizb ut Tahrir katika Wilayah Lebanon imetoa wito kwa Mashababu (wanachama) wake kushiriki katika kikao kilichopangwa kwa uratibu na wanaharakati na watu mashuhuri katika mji wa Tripoli, Jumamosi hii jioni saa sita kamili mbele ya Maonyesho ya Kimataifa ya Tripoli, kwa ajili ya kukemea tamasha la densi (Zambo) na kuimba katika mji wa Tripoli, mji wa elimu na wanazuoni, kama udhuru mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kuhusiana na makosa yanayofanywa mjini Tripoli na ambayo hayaonyeshi kitambulisho chake, katika wakati ambapo umbile halifu la Kiyahudi linaendesha vita vikali dhidi ya Waislamu wa Palestina kwa jumla na hasa Gaza, na uvamizi na jinai zake zimeenea hadi Lebanon na Syria, kwa kukalia kimabavu sehemu ya ardhi ya Kusini na ardhi ya Syria, na ndege zake hazijaondoka anga zake, zikipiga mabomu na kuangamiza bila kuzuiwa au mwenye kuwazuia!

Soma zaidi...

Na anaye fedheheshwa na Mwenyezi Mungu hana wa kumhishimu. [Al-Hajj: 18]

Baada ya maafikiano yote yaliyofanywa na PLO, ambayo yalifikia uhaini mkubwa kwa kuitoa sehemu kubwa ya Palestina. Na baada ya kukubalika kwake kuwa chombo cha usalama (katika muundo wa mamlaka) kinachowapiga vita watu wa Palestina, kupokonya silaha kambi za ndani ya Palestina kwa kuua, kuzingira na kukamata, na nje ya Palestina kwa uratibu na serikali za Syria na Lebanon, ili kuzuia tishio lolote, kubwa au dogo, kwa usalama wa Mayahudi ndani au karibu na Palestina.

Soma zaidi...

Huku Amerika Ikiunga Mkono Mauaji ya Halaiki mjini Gaza, Inaingia Uzbekistan Kama Mshirika wa Usalama!

Mnamo tarehe 28/8/2025, Rais Shavkat Mirziyoyev alimpokea Mjumbe Maalum wa Rais wa Marekani wa Ushirikiano wa Kimataifa, Paolo Zampoli. Kulingana na taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Huduma ya Habari ya Rais, “Mkutano huo ulijadili ushirikiano wa kimkakati kati ya Uzbekistan na Marekani na upanuzi wa ushirikiano wa pande nyingi.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu