Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Kenya Yafanya Visimamo vya Kushutumu Kitendo cha Kikatili cha Umbile la Mauaji la Kiyahudi cha Kulipua Mabomu Rafah

Kufuatia kitendo cha kinyama na cha kusikitisha cha umbile la Kiyahudi cha kulipua mabomu katika Kambi za Wakimbizi huko Rafah, usiku wa tarehe 26 Mei 2024, Hizb ut Tahrir / Kenya ilifanya visimamo vya kulaani baada ya swala za Ijumaa katika maeneo mbalimbali jijini Nairobi, Mombasa, Malindi, Kilifi na Kwale.

Soma zaidi...

Je, Ramadhan itaweka Taqwa katika Nyoyo zenu Kusimama kwa ajili ya Ukombozi wa Palestina?

Hizb ut Tahrir / Kenya kwa furaha, inawapongeza Waislamu nchini na kote duniani kwa ujumla kwa kuwasili kwa mwezi mtukufu wa Ramadhan.

Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Je, Ramadhan itaweka Taqwa katika Nyoyo zenu Kusimama kwa ajili ya Ukombozi wa Palestina?

(Imetafsiriwa)

Hizb ut Tahrir / Kenya kwa furaha, inawapongeza Waislamu nchini na kote duniani kwa ujumla kwa kuwasili kwa mwezi mtukufu wa Ramadhan. Tunapoingia katika mwezi huu wa rehema, msamaha na kukombolewa na Moto wa Jahannam, tunamuomba Mwenyezi Mungu (swt) atujaalie nguvu na afya ya kutekeleza amali adhimu ya saumu ambayo si wajibu tu bali ni moja ya nguzo tano za Uislamu.

Ramadhan hii inakuja huku ulimwengu ukishuhudia mgongano kati ya matakwa ya Umma wa Kiislamu ya kushikamana na Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina na matakwa ya ukafiri wa Magharibi. Umma umeonyesha uaminifu wake kwa Uislamu na unatamani kwa dhati ushindi wa Mwenyezi Mungu. Ulimwengu unashuhudia kufilisika kiakhlaqi kwa maadili ya Magharibi huku wakiunga mkono mashambulizi ya kikatili ya ‘Israel’ huko Gaza. Dola na vyombo vya habari vya Magharibi vinaonyesha rangi zao halisi za unafiki na ubaguzi wa rangi.

Cha kusikitisha ni kwamba, unyama unaofanywa na majeshi ya Kiyahudi dhidi ya ndugu zetu wa Gaza bado haujachemsha nyoyo wala mishipa ya viongozi wa Kiislamu na majeshi yao! Enyi viongozi! Je, saumu yenu itaweka taqwa katika nyoyo zenu na kukata mahusiano na umbile la Kiyahudi? Enyi majeshi, je Ramadhan itawapeni taqwa ya kuwapuuza watawala wenu waliomfanyia khiyana Mwenyezi Mungu, Mtume wake na waumini ili muanze kuandamana kwenda Palestina na kupigana na jeshi la Mayahudi?

Katika historia yote, Ramadhan imekuwa ni mwezi wa ukombozi na ushindi. Historia hii angavu kwa hakika itahuisha ushindi katika Vita vya Badr, Qadisiyyah na Ein Jalut. Tunamuomba Mwenyezi Mungu (swt) atukubalie amali zetu na aujaalie Ummah huu mlinzi na ngao Khilafah kwa njia ya Utume. Khilafah ambayo itakusanya majeshi ya Waislamu ili kuling'oa umbile uaji la Kiyahudi na kukomboa sio tu Palestina inayokaliwa kwa mabavu bali ardhi zote za Waislamu.

Shabani Mwalimu
Mwakilishi kwa Vyombo vya Habari wa Hizb ut Tahrir
Kenya

Soma zaidi...

Sera ya Afya bila Afya

Wizara ya Afya imefichua kuwa Ksh.20 bilioni zimepotea kupitia mpango wa Hazina ya Kitaifa ya Bima ya Afya (NHIF) kupitia madai fidia za kirongo na upasuaji ghushi, miongoni mwa shughuli nyingine za ulaghai zinazofanywa na vituo vya afya.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu