Jumanne, 18 Ramadan 1446 | 2025/03/18
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Sudan imekua Jeraha jengine Chungu kwa Umma wa Kiislamu

Mnamo tarehe 18 Februari 2025, kikosi cha Rapid Support cha Sudan kilifanya mkutano katika jumba la mikutano ya kimataifa la Kenyatta (KICC) jijini Nairobi kuzungumza uundaji wa serikali ya umoja ya majimbo yanayodhibitiwa na kikosi hicho nchini Sudan. Utawala nchini Kenya unashikilia kudai kwamba kujihusisha kwake kwenye mazungumzo hayo ni kuimarisha “juhudi za amani nchini Sudan”. Nairobi imetetea uamuzi wake wa kuwa mwenyeji wa kufanya mazungumzo na kikosi cha wapiganaji yanayolenga kusainiwa kwa mkataba wa kisiasa. Maafisa wa Kiutawala wa Sudan wameiona hatua hii kama jaribio la kuanzisha utawala mwengine sambamba na ule wa Khartoum, hatua hii ya Kenya imepelekea kulaumiwa kwake kwa kukiuka ubwana wa Sudan na kujihusisha na matendo ya kiuhasama.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Kenya Iliandaa Msururu wa Amali katika Kumbukumbu ya Miaka 104 ya Kuvunjwa kwa Dola ya Khilafah

Kama sehemu ya kumbukumbu ya miaka 104 ya kuondolewa kwa Khilafah, Hizb ut Tahrir/Kenya ilifanya kampeni nchi nzima katika mwezi mtukufu wa Rajab 1446 H. Kampeni hii iliyoanza mwanzoni mwa mwezi mtukufu wa Rajab ilihusisha shughuli mbali mbali; Darsa, Semina na Visimamo. Hii ilikuwa ni kuukumbusha Ummah kuhusu hali yake ya kusikitisha ambayo umekuwa ukikabiliana nayo tangu kuondolewa kwa Khilafah mnamo tarehe 28 Rajab 1342 H sawia na tarehe 3 Machi 1924 M.

Soma zaidi...

Chini ya Urasilimali Utunzaji wa Afya huwa kama Fadhila tu wala Hauchukuliwi kuwa ni Haki Msingi

Serikali imeanzisha Mamlaka ya Afya ya Kijamii (SHA) ili kusimamia bima ya afya ya jamii nchini. SHA ina hazina tatu za kifedha: Hazina ya Huduma ya Afya ya Msingi, Hazina ya Bima ya Afya ya Jamii na ile ya hali ya Dharura na Ugonjwa hatari. Watoa huduma za afya nchini Kenya wanaweza kuingia katika kandarasi na mamlaka ya SHA ili kutoa huduma za afya kwa walengwa.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu