Jumanne, 05 Sha'aban 1446 | 2025/02/04
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Hizb ut Tahrir / Ardhi Iliyobarikiwa: Kitengo cha Wanawake “Kalima kwa Mnasaba wa Kumbukumbu ya Miaka 104 ya Kuvunjwa Khilafah!”

Kwa mnasaba wa ujio wa kumbukumbu ya miaka 104 ya kuvunjwa kwa dola ya Kiislamu na makhaini wa Kiarabu na Kituruki iliyoasisiwa na Bwana wa Mitume Muhammad (saw) na maswahaba zake watukufu na waliobarikiwa, Mwenyezi Mungu awawie radhi, na kukomeshwa kwa mfumo wa utawala wa Kiislamu (Khilafah) mnamo tarehe 28 Rajab al-Muharram katika mwaka wa 1342 H sawia na 03/03/1924 M, Kitengo cha Wanawake cha Hizb ut Tahrir katika The Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina) kinawasilisha mkusanyiko wa kalima hizo.

Soma zaidi...

Ujasiri Wenu Kwa Mwenyezi Mungu, Enyi Madhalimu, Unatangaza Kukaribia Mwisho Wenu

Wakati Mayahudi walipokuwa wakiizingira Hospitali ya Kamal Adwan mjini Gaza, kisha kuivamia, kisha kuichoma moto, na kuwapeleka wagonjwa, majeruhi, na wafanyikazi wa matibabu kwenye hatima isiyojulikana hadi wakati wa kuandika taarifa hii, badala ya mamlaka hiyo kulaani uhalifu wao, badala ya kuuchochea ulimwengu dhidi ya vitendo vyao viovu na vya kikatili, badala ya kuuhamasisha Umma wa Kiislamu kuwanusuru watu wa Gaza, badala ya kuona haya kwa heshima ya majeraha ya Gaza na Ukingo wa Magharibi, walikataa kufanya chochote isipokuwa kuwa Jenin, wakifanya matendo ya Mayahudi na kuwanyanyasa watu wa Palestina mithili Mayahudi wanavyowanyanyasa.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina): Watu wa Palestina Wanauita Umma na Majeshi yake Kuinusuru Gaza na Jenin!

Chini ya anwani, “Enyi Majeshi ya Waislamu ... Ni Nani Atakayenusuru Rafah, Jenin, na Palestina yote ikiwa Nyinyi Hamtazinusuru?!”, umati mkubwa wa watu wa Palestina ulishiriki katika mji wa Al-Bireh matembezi yaliyoitishwa na Hizb ut Tahrir katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina mnamo siku ya Ijumaa, 16 Dhu al-Qa'dah 1445 H sawia na 24 Mei 2024 M, wakiyataka majeshi ya Waislamu na vikosi vya silaha kuisuluhisha Palestina na watu wake kutokana na uhalifu wanaotendewa na umbile la Kiyahudi.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina): Qalqilya... Mkutano mkubwa wa Hadhara wa Kuinusuru Gaza na Rafah!

Alasiri ya leo Jumamosi tarehe 18/05/2024, umati mkubwa wa watu kutoka eneo la mkoa huu na maeneo ya jirani walikusanyika katikati ya mji wa Qalqilya, kuitikia wito wa Hizb ut Tahrir katika Ardhi Iliyobarikiwa (Palestina), ambao iliuelekeza kwa watu kuinusuru Gaza na Rafah, kukusanyika katika kisimamo cha halaiki chini ya kichwa, “Enyi Waislamu: Rafah baada ya Gaza Inalilia msaada, basi ifikieni,”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu