Jumanne, 10 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/02
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Msamaha Mbele ya Mola Wetu, na Pole kwa Waliojeruhiwa Gaza Tripoli ash-Sham Yapaza Sauti Yake Dhidi ya Sherehe za Kucheza juu ya Majeraha ya Umma!

Hizb ut Tahrir katika Wilayah Lebanon imetoa wito kwa Mashababu (wanachama) wake kushiriki katika kikao kilichopangwa kwa uratibu na wanaharakati na watu mashuhuri katika mji wa Tripoli, Jumamosi hii jioni saa sita kamili mbele ya Maonyesho ya Kimataifa ya Tripoli, kwa ajili ya kukemea tamasha la densi (Zambo) na kuimba katika mji wa Tripoli, mji wa elimu na wanazuoni, kama udhuru mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kuhusiana na makosa yanayofanywa mjini Tripoli na ambayo hayaonyeshi kitambulisho chake, katika wakati ambapo umbile halifu la Kiyahudi linaendesha vita vikali dhidi ya Waislamu wa Palestina kwa jumla na hasa Gaza, na uvamizi na jinai zake zimeenea hadi Lebanon na Syria, kwa kukalia kimabavu sehemu ya ardhi ya Kusini na ardhi ya Syria, na ndege zake hazijaondoka anga zake, zikipiga mabomu na kuangamiza bila kuzuiwa au mwenye kuwazuia!

Soma zaidi...

Kinachoitwa “Tamasha za Hisia” (Zambo) jijini Tripoli ni Jaribio la Kulionyesha Jiji lisilo na Hisia zake kwa Ummah Kwa hivyo Zisusieni na Komesheni utoaji Leseni Kwazo!

Kwa ukaidi wa wazi wa hisia za Umma na maumivu yake, na kwa ukaidi wa wazi wa Tripoli, jiji la elimu na wanazuoni, na licha ya kutolewa kwa tamko kutoka kwa Kamati ya Utunzaji wa Familia katika Dar al-Fatwa jijini Tripoli na Kaskazini kuonya juu ya njia hii hatari kwa jamii, ambapo ilikuja katika taarifa: “Kamati pia inatahadharisha juu ya hatari ya tamasha, sherehe, filamu, na mipango ambayo imejitokeza hivi karibuni katika jiji letu na ambayo yanaathiri maadili na akhlaki, na ambayo hutumiwa kupitisha ujumbe potovu chini ya kauli mbiu za kisanii au kithaqafa, katika jiji linalojulikana katika historia yake kama jiji la elimu na wanazuoni, na kama ngome ya maadili ya kweli na kitambulisho kinachounganisha. Kamati inasisitiza kwamba kuilinda jamii kutokana na hatari ni jukumu tunaloshirikiana pamoja: linaanza na familia na jamaa, kwenda hadi kwa walimu, na wanazuoni, na pia linajumuisha asasi za kiraia, manispaa, na wanasiasa, kufikia hadi kwa watoa maamuzi katika ngazi ya serikali…”

Soma zaidi...

Usaliti Mpya: Mamlaka ya Lebanon Yamwachilia Huru Mmoja wa Wafungwa Wanaohusishwa na umbile la Kiyahudi!

Leo, Alhamisi, tarehe 21/8/2025, mamlaka ya Lebanon ilimwachia huru ghafla Saleh Abu Hussein, ambaye ni mmoja wa washirika wa umbile la Kiyahudi, bila kubadilishana na yeyote! Na wakamkabidhi kwa umbile hilo kililokuwa mstari wa mbele wa ukaliaji kimabavu wa Palestina mjini Naqoura!

Soma zaidi...

Kudumu kwa Mashirika ya Kifeministi na Mashoga hadi kufikia Hatua ya Kueneza Uchafu miongoni mwa Waumini ni Shambulizi la Dhahiri kwa Heshima ya Waislamu

Baada ya wasagaji wawili wanachama wa chama chenye uhusiano na Chuo Kikuu cha Marekani cha Beirut (AUBMC), chini ya kivuli na jina "Programu Oanishi ya Afya ya Jimai ya Wanawake (WISH) katika AUBMC," kutembelea shule ya upili ya wasichana jijini Tripoli, kwa uratibu wa Wizara ya Elimu; kisha kwa mbwembwe na bila aibu kuendekeza mambo machafu na kuonyesha picha na maudhui machafu kwa wanafunzi, wazazi wakasukumwa kuripoti tukio hilo kwa uongozi wa shule, ambao nao ulieleza kuwa wawili hao walikuja shuleni kwa amri ya Wizara ya Elimu na Elimu ya Juu!

Soma zaidi...

Kisimamo cha Kulaani cha Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Lebanon jijini Beirut “Kutoka Beirut hadi Gaza, Kuweni Answari wa Mwenyezi Mungu, Enyi Majeshi ya Ummah”

Mamia ya Mashababu (wanachama) na wafuasi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Lebanon walishiriki katika kisimamo cha kulaani kilichoitishwa na Hizb, baada ya swala ya Ijumaa mnamo tarehe 25/4/2025, jijini Beirut, mbele ya Msikiti wa Mohammad Al-Amin. Kisimamo hicho kilikuwa na kichwa “Kutoka Beirut hadi Gaza, Kuweni Answari wa Mwenyezi Mungu, Enyi Majeshi ya Umma,” ambapo mabango yalinyanyuliwa yakitaka kuhamasishwa kwa majeshi, kupinduliwa kwa viti vya utawala vya madhalimu, na kunusuriwa kwa Gaza kupitia jihad na silaha.

Soma zaidi...

Ujumbe kutoka Hizb ut Taharir / Wilayah Lebanon Wamzuru Mbunge Osama Saad

Ujumbe kutoka Hizb ut Tahrir / Wilayah Lebanon katika mji wa Sidon, ukiwakilishwa na Mjumbe wa Kamati Kuu ya Mawasiliano, Mhandisi Bilal Zaidan na Mjumbe wa Kamati ya Amali katika mji wa Sidon, Hajj Hassan Nahhas, walimtembelea Mwakilishi Osama Saad leo, Jumatano, Disemba 11, 2024. Ujumbe huo uliwasilisha msimamo wa Hizb kuhusu matukio mbalimbali hasa yanayojiri katika eneo hali ya Syria, Lebanon na kanda kwa jumla.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu