Je! Uongozi wa Pakistan Ulipotezaje Hadhi Yake Mbele ya India na Trump?!
- Imepeperushwa katika Al-Rayah
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Uongozi wa kisiasa na kijeshi wa Pakistan ulipoteza ushindi uliopatikana na mwewe wa Jeshi lake la Anga, na simba wa jeshi lake la nchi kavu, juu ya India mnamo Mei, ikitoa funzo ambalo India haitalisahau kamwe, kwa kukubali kusitishwa kwa mapigano kati ya nchi hizo mbili. Hii ni licha ya msisitizo wa India kusitisha Mkataba wa Maji wa Indus, na kuinyima Pakistan karibu 80% ya maji ambayo hutiririka kutoka kwa Mto Indus, ambao unatoka China, unapitia India, na kisha kuingia Pakistan. Hii pia ni licha ya kwamba India bado inaendelea kuikalia kimabavu Kashmir... Kisha, baada ya upatanishi wa Rais wa Marekani, Donald Trump kuweka usitishaji vita kati ya pande hizo mbili, na kuiokoa India kutokana na mtego iliyokuwa imejiwekea, kutokana na hesabu potofu ya mienendo ya madaraka, serikali ya Pakistan ilitangaza, mnamo tarehe 21 Juni 2025, uteuzi wake wa Rais wa Marekani Donald Trump kwa ajili ya Tuzo ya Amani ya 2026, ikidai ni kutokana na “kuhusika kwake pamoja na Islamabad na New Delhi ambako kulipunguza hali iliyokuwa ikizorota kwa kasi” kati ya Pakistan na India mwezi Mei.