Marufuku ya Kyrgyzstan dhidi ya Niqab ni Jaribio la Kutapatapa la Utawala wake wa Kisekula Kukandamiza Kuibuka kwa Kitambulisho cha Kiislamu Miongoni mwa Watu wake
- Imepeperushwa katika Kitengo cha Wanawake Afisi Kuu ya Habari
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Kyrgyzstan imekuwa nchi ya hivi punde zaidi katika Asia ya Kati kupiga marufuku Niqab. Hatua hii ya kisheria ilianza kutekelezwa mnamo tarehe 1 Februari 2025 na ukiukaji huu utatozwa faini ya 20,000 som ($230). Nguo za Kiislamu za wanawake na ndevu za wanaume zimekuwa zikilengwa na serikali za Asia ya Kati kwa muda mrefu, ambapo dola zenye nguvu ya kisekula zinaogopa ushawishi unaoongezeka wa Uislamu. Wabunge wa Kyrgyzstan wametoa kisingizio duni kwamba marufuku hiyo inahitajika kwa sababu za usalama, ili nyuso za watu zionekane na watu binafsi kutambuliwa. Lakini wapinzani wanasema marufuku hiyo inawanyima wanawake uhuru wa kuvaa wanavyotaka.