Alhamisi, 19 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/11
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Kauli za Netanyahu kuhusu "Israel Kubwa" ni Tangazo la Vita ambalo linafuta Mikataba, na, kwa sababu hiyo, Majeshi Yanasonge, na Jambo jengine lolote lisokuwa hilo ni Usaliti

Huyu hapa mhalifu wa kivita Netanyahu anatangaza waziwazi na bila kufasiriwa kwa watawala waoga wa Kiarabu na wasemaji wao, akisema katika mahojiano na chaneli ya Kiebrania i24: “Mimi niko kwenye misheni ya vizazi na kwa jukumu la kihistoria na la kiroho, ninaamini kwa dhati ruwaza ya Israel Kubwa, ambayo ni pamoja na Palestina ya kihistoria na sehemu za Jordan na Misri.” Mhalifu Smotrich alikuwa amemtangulia kwa kauli zile zile na kunyakua sehemu za nchi za Kiarabu zinazoizunguka Palestina, ikiwemo Jordan. Katika muktadha huo huo, adui namba moja wa Uislamu na Waislamu, Rais Trump wa Marekani, alimpa idhini ya upanuzi wake akisema, “Israel ni sehemu ndogo sana ikilinganishwa na ukubwa wa ardhi hizo, na najiuliza ikiwa inaweza kupata ardhi zaidi kwa sababu kweli ni ndogo sana.”

Kuundwa kwa cheo cha "Mufti Muongofu" katika Zama za Akili Bandia Kuunda Sheria Inayoafikiana na Magharibi na Watawala wake Vibaraka

Katikati ya mporomoko wa kisiasa na kifikra wa Umma wa Kiislamu, na wakati ambapo njama dhidi ya dini yake na hukmu zake zikiongezeka, serikali tawala na zana zao - taasisi rasmi za kidini - zinazindua makongamano yenye kauli mbiu za kustaajabisha na misamiati ya uchochezi ya kiteknolojia, wakikopesha mradi wao wa kupotosha kuwa dini ni kero kwa “usasa” na “maendeleo”. Hii ni pamoja na kongamano la "Kuunda cheo cha Mufti Sahihi Katika Zama za Akili Bandia,” lililoandaliwa na Dar al-Ifta ya Misri chini ya udhamini wa moja kwa moja wa Rais Abdel Fattah el-Sisi.

Msako Mkali wa Amerika dhidi ya Mashirika ya Kiislamu

Katika mahojiano ya hivi majuzi na mtangazaji wa redio Sid Rosenberg, Katibu wa Waziri wa Mambo ya Nje Marco Rubio alionyesha mchakato unaoendelea wa kuiorodhesha Ikhwan al-Muslimin na CAIR kama mashirika ya kigaidi. Waziri Rubio alisema kwamba uorodheshaji kama huo ulikuwa "katika kazi zao, na ni wazi kuna matawi tofauti tofauti ya Ikhwan al-Muslimin, kwa hivyo itabidi uliorodheshe kila moja yao."

Gaza iko Ukingoni mwa Kuzidishwa Mauaji na Ukandamizaji Mkali ikiwa Umma wa Kiislamu hautasonga mbele Kuinusuru

Gaza Hashim inaingia katika hatua mpya ya mauaji na uharibifu baada ya wizara ya usalama ya umbile halifu kuamua asubuhi ya Ijumaa hii, 08/08/2025, kupanua operesheni zake ili kuweka udhibiti wake juu ya Mji wa Gaza kikamilifu, na uamuzi huu ulikuja kwa siri kutoka kwa Amerika kwa ulimi wa Trump, Rubio, na wengine kutoka kwa wakaazi wa (ikulu ya) Jumba Jeusi.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu