Alhamisi, 19 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/11
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Enyi Watu! Je, bado mungali na matumaini kwa Watawala na Wanasiasa Watepetevu (Ruwaibidha) wa Sasa?!

Baada ya kuanguka kwa dhalimu Hasina, watu walitarajia Profesa Yunus achukue hatua madhubuti za kukabiliana na udhibiti wa Marekani-Uingereza-India kwa kutumia ushawishi wake wa kimataifa. Angeweza kuunda mjadala huo na mazingira ya kisiasa nchini humo ambayo kwayo watu wangeweza kuunda suluhisho jipya la kisiasa ili kulinda maslahi ya Uislamu, maslahi ya watu na ubwana wa nchi katika Bangladesh mpya. Ijapokuwa idadi kubwa ya wakaazi wa nchi hii ni Waislamu, serikali ya mpito, kuuondoa Uislamu katika masuluhisho ya kisiasa, haijaondoa marufuku iliyowekwa na dhalimu Hasina kwa chama cha kisiasa cha Hizb ut Tahrir kwa kujisalimisha kwa Marekani-India. Pamoja na hayo, kupitia makongamano ya mtandaoni Hizb ut Tahrir imewasilisha muundo wa dola ya Kiislamu, njia ya kuasisi uchumi unaojitegemea na kuwa na jeshi thabiti kwa ajili ya kulinda ubwana wa nchi hii kwa kuzingatia katiba ya Kiislamu ili kutekeleza matumaini na matarajio ya wananchi wa Bangladesh mpya.

Hotuba ya Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan katika Mkutano na Waandishi wa Habari mnamo Jumamosi, 22 Safar 1447 H sawia na 16/08/2025 M, yenye kichwa: “Wito kwa Watu wa Sudan... Ikamateni Darfur Ili Isiungane na Kusini”

Mnamo Jumamosi, 26/7/2025, Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) vilitangaza kuundwa kwa serikali sambamba na serikali iliyopo nchini Sudan, katika mji mkuu wa Darfur Kusini (Nyala). Hatua hii ya RSF ni hatua ya juu katika kutenganisha eneo la Darfur, ambalo inalidhibiti, isipokuwa sehemu za mji wa El Fasher, ambao mzingiro wa kukandamiza umewekwa juu yake kwa zaidi ya mwaka mmoja, na kuanzisha mashambulizi mfululizo dhidi yake ili kuuangusha, ili eneo zima la Darfur liwe chini ya udhibiti wake.

Iwapo Kuanguka kwa ‘Jamhuri’ Hakukupelekea Kusimamishwa kwa Khilafah, Ni lazima Kutumike kama Hatua ya Mpito kuelekea Khilafah Rashida

Kuporomoka kwa serikali ya Jamhuri nchini Afghanistan ni moja ya matukio muhimu zaidi kwa watu wa Afghanistan na Umma mpana wa Kiislamu katika karne ya 21. Serikali hii sio tu kwamba haikuwa na mizizi yoyote katika itikadi ya Kiislamu, bali ilikuwa ni zao la muundo wa ukoloni mamboleo - mfumo ulioagizwa kutoka nje uliojengwa ili kurasimisha ufisadi, utegemezi, na dhulma. Kuanguka kwake lilikuwa ni mwisho wa kimaumbile na usioepukika wa mfumo ambao, tangu kuanzishwa kwake, ulikuwa ngeni kwa kitambulisho cha Kiislamu na kupingana na maadili ya Uislamu.

Ayman Safadi: “Yeyote ambaye ana badali ya Suluhisho la dola mbili, basi na aiwasilishe!” Hizb ut Tahrir imewasilisha na inaendelea kuwasilisha suluhisho halali na la kivitendo

Serikali ya Jordan ndio iliyowawekea watu wa Jordan na Umma wa Kiislamu suluhisho linaloendana na kuhifadhi usalama wa umbile katili la Kiyahudi. Hukuwa na maregeleo ya masuluhisho ya kadhia ya Palestina isipokuwa Marekani, rafiki wa serikali hii, mshirika wa umbile la Kiyahudi, mdhamini wake, mlinzi wake, na mshirika wake katika vita vya maangamizi na njaa dhidi ya watu wa Gaza.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu