Hakuna Suluhisho kwa Suala la Sudan Isipokuwa Kutawalisha Uislamu
- Imepeperushwa katika Uchambuzi
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Tangu uhuru wake mnamo tarehe 1/1/1956, Sudan imeshuhudia mfululizo wa mapinduzi ya kijeshi. Ya kwanza ilikuwa jaribio lililofeli lililoongozwa na Ismail Kabida, ambaye alijaribu kupindua serikali ya kwanza ya kitaifa iliyoongozwa na Ismail al-Azhari. Hii ilifuatiwa na mapinduzi ya kwanza yaliyofaulu yaliyoongozwa na Luteni Jenerali Ibrahim Abboud mnamo Novemba 1958 dhidi ya serikali iliyochaguliwa ya al-Azhari.