Jumamosi, 14 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/06
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Huku Amerika Ikiunga Mkono Mauaji ya Halaiki mjini Gaza, Inaingia Uzbekistan Kama Mshirika wa Usalama!

Mnamo tarehe 28/8/2025, Rais Shavkat Mirziyoyev alimpokea Mjumbe Maalum wa Rais wa Marekani wa Ushirikiano wa Kimataifa, Paolo Zampoli. Kulingana na taarifa kwa vyombo vya habari kutoka Huduma ya Habari ya Rais, “Mkutano huo ulijadili ushirikiano wa kimkakati kati ya Uzbekistan na Marekani na upanuzi wa ushirikiano wa pande nyingi.”

Watu wa Al-Fashir Baina ya Nyundo ya Vita na Kinoo cha Njaa, na Hawana Wokovu isipokuwa kwa Dola ya Khilafah

Mji wa Al-Fashir, mji mkuu wa Jimbo la Darfur Kaskazini, unashuhudia janga halisi la kibinadamu, huku kukiwa na vita kati ya pande zinazopigana, ambapo makumi ya raia waliuawa katika siku chache zilizopita, huku wakaazi wakiteseka kutokana na kuzingirwa kwa zaidi ya mwaka mmoja, na njaa ya makusudi, katika kivuli cha kimya cha kituliwa shaka cha kimataifa, huku Umoja wa Mataifa ukithibitisha mauaji ya angalau watu 89 katika mapigano ya siku zilizopita.

Mvua ni Baraka na Rehema, lakini bila Uchungaji imekuwa ni Laana!

Ni huzuni na pia inasikitisha kwamba msimu wa mvua hauji kwa ghafla, bali ni kipindi cha taarifa ambacho hurudiwa kila mwaka. Kinachoshangaza zaidi ni kwamba vituo vingi vya uchunguzi wa hali ya hewa vilionya kuhusu mvua kubwa, lakini asasi za serikali hazikuchukua hatua yoyote kuzuia madhara yake, ambayo yalikuwa mabaya zaidi kwa vijiji vya Jimbo la Mto Nile, mashariki mwa Sudan na hata Kordofan, miongoni mwa kwengine.

Wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya Taqli Watoa Wito Mkali kwa Waislamu Kutibua Mpango wa Marekani wa Kutenganisha Darfur

Kama sehemu ya kampeni iliyoandaliwa na Hizb ut Tahrir/ Wilayah Sudan ya kukwamisha mpango wa kuisambaratisha Sudan kwa kutenganisha eneo la Darfur, na kuzingatia umoja wa Ummah kama suala nyeti, suala la uhai na kifo, wanachama wa Hizb ut Tahrir huko Abbasiya walifanya mkutano mnamo Ijumaa, 6 Rabi' al-Awwal 1447 H sawia na 29 Agosti 2025 M, baada ya swala ya Ijumaa katika Msikiti wa Sheikh Yahya kituo cha kuhifadhi Quran. Walitoa wito wa dhati kwa Waislamu wa matabaka yote, wakiwemo wanasiasa, wanahabari, wanazuoni, maafisa na askari na wengineo, wakiwahimiza kutimiza wajibu wao wa kidini ili kuzuia kujitenga kwa Darfur.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu