Jumamosi, 14 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/06
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Kinachoitwa “Tamasha za Hisia” (Zambo) jijini Tripoli ni Jaribio la Kulionyesha Jiji lisilo na Hisia zake kwa Ummah Kwa hivyo Zisusieni na Komesheni utoaji Leseni Kwazo!

Kwa ukaidi wa wazi wa hisia za Umma na maumivu yake, na kwa ukaidi wa wazi wa Tripoli, jiji la elimu na wanazuoni, na licha ya kutolewa kwa tamko kutoka kwa Kamati ya Utunzaji wa Familia katika Dar al-Fatwa jijini Tripoli na Kaskazini kuonya juu ya njia hii hatari kwa jamii, ambapo ilikuja katika taarifa: “Kamati pia inatahadharisha juu ya hatari ya tamasha, sherehe, filamu, na mipango ambayo imejitokeza hivi karibuni katika jiji letu na ambayo yanaathiri maadili na akhlaki, na ambayo hutumiwa kupitisha ujumbe potovu chini ya kauli mbiu za kisanii au kithaqafa, katika jiji linalojulikana katika historia yake kama jiji la elimu na wanazuoni, na kama ngome ya maadili ya kweli na kitambulisho kinachounganisha. Kamati inasisitiza kwamba kuilinda jamii kutokana na hatari ni jukumu tunaloshirikiana pamoja: linaanza na familia na jamaa, kwenda hadi kwa walimu, na wanazuoni, na pia linajumuisha asasi za kiraia, manispaa, na wanasiasa, kufikia hadi kwa watoa maamuzi katika ngazi ya serikali…”

Msamaha Mbele ya Mola Wetu, na Pole kwa Waliojeruhiwa Gaza Tripoli ash-Sham Yapaza Sauti Yake Dhidi ya Sherehe za Kucheza juu ya Majeraha ya Umma!

Hizb ut Tahrir katika Wilayah Lebanon imetoa wito kwa Mashababu (wanachama) wake kushiriki katika kikao kilichopangwa kwa uratibu na wanaharakati na watu mashuhuri katika mji wa Tripoli, Jumamosi hii jioni saa sita kamili mbele ya Maonyesho ya Kimataifa ya Tripoli, kwa ajili ya kukemea tamasha la densi (Zambo) na kuimba katika mji wa Tripoli, mji wa elimu na wanazuoni, kama udhuru mbele ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kuhusiana na makosa yanayofanywa mjini Tripoli na ambayo hayaonyeshi kitambulisho chake, katika wakati ambapo umbile halifu la Kiyahudi linaendesha vita vikali dhidi ya Waislamu wa Palestina kwa jumla na hasa Gaza, na uvamizi na jinai zake zimeenea hadi Lebanon na Syria, kwa kukalia kimabavu sehemu ya ardhi ya Kusini na ardhi ya Syria, na ndege zake hazijaondoka anga zake, zikipiga mabomu na kuangamiza bila kuzuiwa au mwenye kuwazuia!

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu