Jumatatu, 13 Dhu al-Hijjah 1446 | 2025/06/09
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Jibu la Swali: Je, Yajuzu Mtu Kumpa Zaka Dadake au Binti Yake?

Uislamu umewajibisha kushibisha mahitaji haya ya kimsingi na kuwapa wale wasioweza kuyapata. Ikiwa mtu binafsi anajipatia wenyewe, ni vizuri; ikiwa hawawezi kujiruzuku kwa sababu ya ukosefu wa pesa za kutosha au kutokuwa na uwezo wa kupata pesa za kutosha, Shariah inawajibisha wengine kuwasaidia hadi mahitaji haya ya kimsingi yatimizwe.

Soma zaidi...

Jibu la Swali: Biashara ya Mtandaoni (E-Commerce)

Je, biashara ya mtandaoni (e-commerce) na kampuni ya DXN ya Malaysia inaruhusiwa? Kampuni hii inategemea uuzaji wa virutubisho vya lishe, shampoo, krimu za ngozi...nk. Unapo  nununua kutoka kwake kiasi fulani, inatoa punguzo (discount). Pindi pointi zako zikifika 100 inakupa punguzo la asilimia sita. Kadiri unavyopata pointi zaidi, ndivyo inavyokupa punguzo kubwa zaidi, na pointi hizi hubadilishwa kuwa kiasi cha pesa ambacho huhamishiwa kwako ama kwa njia ya bahasha au barua ambayo hutolewa kwako kila mwezi, au kuhamishiwa kwenye salio (balance) lako la benki.

Soma zaidi...

Mahouthi Wanaendelea na Jinai na Uhalifu wao... Kuwakamata Wanachama wa Hizb ut Tahrir

Kuanzia Alhamisi, tarehe 10 Jumada al-Akhir 1446 H sawia na tarehe 12 Disemba 2024 M, wanamgambo wa Houthi walifanya uvamizi kwenye nyumba za wanachama wa Hizb ut Tahrir bila ya kuzingatia vifungu vya sheria ya Kiislamu au hata kanuni na desturi za kikabila! Walivamia nyumba zao katika kurugenzi tatu za Jimbo la Taiz (Taiziyah, Mawiah, na Khadir); na kuwakamata: Suleiman al-Muhajri, Khaled al-Hami (waliyemwekwa kizuizini miezi sita iliyopita kwa tuhuma za kubeba Dawah pamoja na Hizb ut Tahrir), Mhandisi Taqi al-Din al-Zayla'i, Amir al-Sabry, na Muhammad al-Faqih. Wafuasi watatu wa Hizb ut Tahrir pia walikamatwa: Abdul Malik al-Jundi, Abdul Qader al-Sarari, na Adnan al-Zayla'i, ambao wanasalia chini ya ulinzi wa wahalifu hao mpaka kufikia wakati wa kuandika taarifa hii.

Soma zaidi...

Chini ya Urasilimali Utunzaji wa Afya huwa kama Fadhila tu wala Hauchukuliwi kuwa ni Haki Msingi

Serikali imeanzisha Mamlaka ya Afya ya Kijamii (SHA) ili kusimamia bima ya afya ya jamii nchini. SHA ina hazina tatu za kifedha: Hazina ya Huduma ya Afya ya Msingi, Hazina ya Bima ya Afya ya Jamii na ile ya hali ya Dharura na Ugonjwa hatari. Watoa huduma za afya nchini Kenya wanaweza kuingia katika kandarasi na mamlaka ya SHA ili kutoa huduma za afya kwa walengwa.

Soma zaidi...

Wito kwa Waislamu kwa Jumla, na kwa Watu wa Ash-Sham Hasa

Enyi Waislamu kwa jumla, na watu wa Ash-Sham hasa: Kiongozi wa Hizb ut Tahrir, asiyewadanganya watu wake, anakuonyeni juu ya mikono ya mashetani wa wanadamu wanaotaka damu yenu imwagike bure, ili msifikie wema msafi na dhahiri, kuhukumu kwa yale yote aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu, bali hukmu iliyotungwa na mwanadamu lakini yenye jina na maana tofauti. Badala ya kuwa Umma ambao makafiri wanauchukulia kwa uzito, mumerudi kuwa wafuasi wa makafiri wakoloni na vibaraka wao, na huu ni uhalifu, Mwenyezi Mungu aepushie mbali, ambao hatima yake ni udhalilifu duniani na adhabu kali kesho Akhera.

Soma zaidi...

Mfano Hatari Ambao Haupaswi Kupuuzwa

Katika mfano hatari katika historia ya mapinduzi, Huduma Kuu ya Usalama mjini Aleppo iliteka nyara wanawake kumi mnamo siku ya Jumamosi, 21 Disemba 2024. Wanawake hao walikuwa wamejitokeza wakiandamana, wakitaka utawala wa Uislamu na kuachiliwa huru waume zao, vijana wao na watoto wao waliotekwa nyara zaidi ya mwaka mmoja na nusu uliopita. Watu hawa wamefungwa jela na Jolani [al-Julani] mjini Idlib tangu Mei 7, 2023!

Soma zaidi...
Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu