Jumatatu, 16 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/08
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Umuhimu wa Kimkakati wa Siasa za Kijiografia za Sudan

Sudan ni nchi yenye umuhimu mkubwa wa kisiasa za kijiografia, unaotokana na ardhi yake kubwa, maliasili nyingi, na eneo ambalo linaiweka kitovu cha baadhi ya njia muhimu zaidi za kibiashara na kisiasa duniani. Licha ya kukabiliwa na miongo kadhaa ya ukosefu wa utulivu wa kisiasa, Sudan inasalia kuwa kitovu cha maslahi kwa dola zenye nguvu za kieneo na kimataifa kutokana na nafasi yake ya kimkakati na uwezo wake ambao haujatumiwa. Umuhimu wake sio wa kisasa tu bali pia wa kihistoria, haswa katika zama ambazo ilikuwa sehemu ya Khilafah kubwa zaidi ya Kiislamu, ambapo ilichukua nafasi muhimu katika kuunganisha na kuimarisha ulimwengu mpana wa Kiislamu. Na umuhimu wake utabaki mbeleni, Khilafah itakaporegea.

Mwaliko wa Kuhudhuria Kikao cha Kisiasa

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Sudan inafuraha kuwaalika ndugu katika vyombo vya habari, wanasiasa, na wale wote wanaopenda masuala ya umma, kuhudhuria na kushiriki katika kikao kipya cha Kisiasa, ambapo Ustadh Hatim Jaafar, mwanasheria - mjumbe wa Baraza la Hizb ut Tahrir katika Wilayah ya Sudan.

Jibu la Swali: Matukio nchini Armenia na Azerbaijan

Uwepo wa Urusi katika Caucasus Kusini umetikiswa “kufuatia Armenia na Azerbaijan kutia saini tamko la pamoja na Marekani juu ya suluhisho la amani na makubaliano katika maeneo ya biashara na usalama baada ya mzozo uliodumu kwa zaidi ya miaka 35 kati ya nchi hizo mbili jirani...” (Al Jazeera, 15/8/2025). Azerbaijan na Armenia zilitoa taarifa ya pamoja mnamo tarehe 11/8/2025, kufuatia makubaliano yaliyotiwa saini kati yao jijini Washington mnamo tarehe 8/8/2025, yakizitaka pande nyingine kufunga Kundi la Minsk lililoundwa mwaka 1992 ili kutatua masuala kati ya nchi hizo mbili.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu