Afisi ya Habari
Wilayah Sudan
H. 17 Rabi' II 1447 | Na: HTS 1447 / 42 |
M. Alhamisi, 09 Oktoba 2025 |
Taarifa kwa Vyombo vya Habari
Ni lini Tutakomesha Uingiliaji wa Kafiri Magharibi na Mashirika yake ya Kikoloni katika Maisha Yetu, na Kuelekeza Nyuso Zetu Kwa Al-Waahid, Al-Haakim?
(Imetafsiriwa)
Chini ya ufadhili wa shirika la Ufaransa la Promediation, vyama vya kisiasa vya Sudan vilifanya warsha jijini Port Sudan, kama ilivyoripotiwa kwenye tovuti ya Sudan Tribune mnamo tarehe 5 Oktoba 2025: “Warsha inalenga kufafanua vigezo vya mazungumzo ya mustakbali yatakayoongozwa na Sudan, ikiwemo washiriki wake, eneo, na dori ya upatanishi wa kimataifa, kulingana na msemaji wa kambi hiyo Mohammed Zakaria. Viongozi wa muungano huo walisisitiza haja ya muungano wa ndani ulioshikamana. Minni Arko Minnawi, mkuu wa kamati ya kisiasa ya umoja huo, alisema hatua ya pamoja kati ya viongozi wa kiraia na kijeshi ni muhimu kwa ajili ya utulivu.
Kwa kuzingatia uhalisia huu, sisi, katika Hizb ut Tahrir / Wilayah ya Sudan, tunafafanua mambo yafuatayo:
Kwanza: Uislamu umesuluhisha kwa uthabiti suala la chanzo cha utatuzi wa matatizo ya maisha, ukiipa ubwana kwa Shariah pekee. Muislamu haruhusiwi kutafuta ufumbuzi wa matatizo yoyote ya kimaisha isipokuwa kutoka kwa Shariah. Hakika imelinganisha hili na imani. Mwenyezi Mungu (swt) asema:
[فَلَا وَرَبِّكَ لَا يُؤْمِنُونَ حَتَّىٰ يُحَكِّمُوكَ فِيمَا شَجَرَ بَيْنَهُمْ ثُمَّ لَا يَجِدُوا فِي أَنفُسِهِمْ حَرَجاً مِّمَّا قَضَيْتَ وَيُسَلِّمُوا تَسْلِيماً]
“La! Naapa kwa Mola wako Mlezi! Hawataamini mpaka wakufanye wewe ndiye muamuzi katika yale wanayo khitalifiana, kisha wasione uzito katika nyoyo zao juu ya hukumu utayo toa, na wanyenykee kabisa.” [An-Nisa: 65].
Kwa hivyo, chimbuko la suluhisho liko katika Uislamu pekee, na sio matamanio ya wanasiasa wanaogombania madaraka.
Pili: Uislamu unafaradhisha Waislamu, pindi unapotokea mzozo juu ya jambo lolote, wauregeshe kwenye Kitabu cha Mwenyezi Mungu (swt) na Sunnah za Mtume Wake (saw) sio kwa wakoloni au mashirika yao ya uhalifu. Kuyaregesha mambo kwenye Uislamu ni mojawapo ya kanuni msingi za imani. Mwenyezi Mungu (swt) asema:
[فَإِن تَنَازَعْتُمْ فِي شَيْءٍ فَرُدُّوهُ إِلَى اللَّهِ وَالرَّسُولِ إِن كُنتُمْ تُؤْمِنُونَ بِاللَّهِ وَالْيَوْمِ الْآخِرِ ذَلِكَ خَيْرٌ وَأَحْسَنُ تَأْوِيلاً]
“Enyi mlio amini! Mt'iini Mwenyezi Mungu, na mt'iini Mtume na wenye madaraka katika nyinyi. Na mkizozana katika jambo basi lirudisheni kwa Mwenyezi Mungu na Mtume, ikiwa mnamuamini Mwenyezi Mungu na Siku ya Mwisho. Hayo ndiyo bora zaidi na ndiyo yenye mwisho mwema.” [An-Nisa: 59]
Tatu: Mtu kujiweka rehani kwa dola za kikoloni za kikafiri ambazo zina chuki dhidi ya Uislamu na Waislamu, kama vile Ufaransa, Amerika, Uingereza na Urusi, na kutegemea uingiliaji kati wa mashirika yao ya uhalifu, kama vile Promediation, Taasisi ya Amani ya Marekani, Chatham House, na wengineo, ni kujiua kisiasa na kusaliti Ummah. Mwenyezi Mungu (swt) asema:
[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تَتَّخِذُوا بِطَانَةً مِّن دُونِكُمْ لَا يَأْلُونَكُمْ خَبَالاً وَدُّوا مَا عَنِتُّمْ قَدْ بَدَتِ الْبَغْضَاءُ مِنْ أَفْوَاهِهِمْ وَمَا تُخْفِي صُدُورُهُمْ أَكْبَرُ قَدْ بَيَّنَّا لَكُمُ الْآيَاتِ إِن كُنتُمْ تَعْقِلُونَ]
“Enyi mlio amini! Msiwafanye wasiri wenu watu wasio kuwa katika nyinyi. Hawataacha kukufanyieni ubaya. Wanayapenda yanayo kudhuruni. Imekwisha fichuka chuki yao katika midomo yao. Na yanayo ficha vifua vyao ni makubwa zaidi. Tumekwisha kubainishieni Ishara ikiwa nyinyi mtayatia akilini.” [Aal-i-Imran: 118].
Nne: Sheria ya Kiislamu imeweka mipaka ya uhusiano na nchi za kigeni na asasi zake kwa dola, na imeharamisha mtu au kikundi chochote kuwa na uhusiano wowote na nchi ya kigeni au asasi yoyote ya kigeni, kwani jambo hilo linaleta hatari kubwa kwa chombo cha dola na Ummah.
Tano: Uislamu ni tajiri katika hukmu zake na utatuzi wa matatizo yote ya maisha, kwani siasa katika Uislamu ni kushughulikia mambo ya watu, ndani na nje, na inatekelezwa kivitendo na dola. Ni amali tukufu kabisa, hakika ni kazi ya Mitume kama alivyoieleza Mtume (saw) pale aliposema: «كَانَتْ بَنُو إسْرَائِيلَ تَسُوسُهُمُ الأنْبِيَاءُ، كُلَّما هَلَكَ نَبِيٌّ خَلَفَهُ نَبِيٌّ، وإنَّه لا نَبِيَّ بَعْدِي، وَسَتَكُونُ خُلَفَاءُ فَتَكْثُرُ»، قالوا فَما تَأْمُرُنَا؟ قالَ: «فُوا ببَيْعَةِ الأوَّلِ، فَالأوَّلِ، وَأَعْطُوهُمْ حَقَّهُمْ، فإنَّ اللَّهَ سَائِلُهُمْ عَمَّا اسْتَرْعَاهُمْ» Abu Huraira ameripoti kuwa Mtume amesema, “Banu Israil walikuwa wakitawaliwa na manabii, kila mara mmoja anapokufa mtu mwengine anachukua nafasi yake. Hakutakuwa na Nabii baada yangu, lakini kutakuwa na makhalifa wengi.” Akaulizwa unatuamrisha nini? Akajibu, “Timizeni kiapo cha utii kwa kila mmoja na mpeni haki yake kwani Mwenyezi Mungu atawauliza juu ya yale aliyowataka kuyachunga” [Imepokewa na Muslim].
Kwa kumalizia: Umma leo unahitaji mfumo wa Uislamu; Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, inayosimamisha Dini, kutabikisha Shariah, kung'oa ushawishi wa Mkoloni Kafiri Magharibi kutoka katika ardhi zetu, kuwaandama watu wenye kutia shaka wanaowasiliana na balozi na mashirika ya Magharibi, na kuishi maisha kwa ikhlasi kwa Mungu Mmoja, Hakimu. Na kwa ajili hiyo watu wanapaswa kufanya kazi, kama Mwenyezi Mungu (swt) anavyosema:
[يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اسْتَجِيبُوا لِلَّهِ وَلِلرَّسُولِ إِذَا دَعَاكُمْ لِمَا يُحْيِيكُمْ]
“Enyi mlio amini! Muitikieni Mwenyezi Mungu na Mtume anapo kuitieni jambo la kukupeni uzima wa milele.” [Al-Anfal: 24].
Ibrahim Othman (Abu Khalil)
Msemaji Rasmi wa Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Sudan
Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari Wilayah Sudan |
Address & Website Tel: 0912240143- 0912377707 http://www.hizb-sudan.org/ |
E-Mail: Spokman_sd@dbzmail.com |