Jumatatu, 23 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/15
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Iwe ni Suala la Mafuriko au Kashmir, Suala la Uchumi au Kukaliwa Kimabavu kwa Mito Yetu na Dola ya Kibaniani —Je, Tutaendelea Kungoja ‘Jumuiya ya Kimataifa’ Mpaka Lini Kutatua Matatizo Yetu?

Baada ya mafuriko makubwa katika majimbo ya kaskazini ya Khyber Pakhtunkhwa, hasa katika Buner na maeneo ya karibu, ambapo mamia ya watu walipoteza maisha na nyumba, mifugo, mali na magari kusombwa na maji, mafuriko mapya sasa yanapitia Punjab na baadaye yataelekea Sindh. Hapo awali, Karachi pia ilikumbwa na mvua kubwa. Tunamuombea Mwenyezi Mungu Mtukufu usalama na kheri, kwani pamoja na utabiri zaidi wa mvua, watawala wetu wameinua mikono juu tu na kuliacha suala zima kwa rehema ya jumuiya ya kimataifa. Wanaendelea kuwasilisha suala hili zima kwa namna ambayo ni kana kwamba haya ni mabadiliko ya tabianchi ambayo hayawezi kudhibitiwa kabisa na wao, na ikiwa ‘jumuiya ya kimataifa’ haitaingilia kati, wataachwa bila msaada kabisa – kana kwamba ulinzi wa maisha na mali ya watu wao sio jukumu lao bali ni la mfumo wa kimataifa!

Soma zaidi...

Hali Baada ya Mvua na Mafuriko kwa Mara Nyingine Tena Imeweka Wazi Kuwa Waislamu Wanahitaji Mchungaji Khalifah

Tangu Juni 26, mafuriko katika maeneo mbalimbali ya Khyber Pakhtunkhwa, Punjab, na Karachi yamesababisha vifo vya zaidi ya watu 650 na kujeruhi zaidi ya elfu moja. Maelfu ya nyumba zimesombwa na maji, pamoja na akiba za maisha yote za watu, mali za nyumbani, na magari. Dada na mabinti zetu—ishara za staha na heshima—wamenyimwa nyumba na faragha zao, wakilazimishwa kuishi chini ya anga wazi.

Soma zaidi...

Ukosoaji wa Trump wa India ... Maslahi ya Amerika, Sio Urafiki na Pakistan

Mnamo 30 Julai 2025, Rais wa Marekani, Donald Trump alitangaza msururu wa ushuru wa kulipiza kisasi dhidi ya India, akiikosoa kwa kuwa na “vizuizi vizito na visivyo vumilika vya biashara visivyo vya ushuru” na kutoza ushuru wa forodha wa 25% pamoja na faini. Huku Trump alkikiri “urafiki” na India, aliikosoa vikali kwa kununua vifaa vya kijeshi vya Urusi na mafuta ya bei nafuu wakati Marekani ilikuwa ikiishinikiza Urusi kumaliza vita nchini Ukraine. Katika karipio la hadharani lisilo la kawaida, Trump aliusifu uchumi wa Urusi na India kuwa “umekufa” na akamuonya Rais wa zamani wa Urusi Medvedev “kuchunga mdomo wake.”

Soma zaidi...

“Siku ya Uhuru” ya 78 Pakistan Itakuwa Huru Kupitia Kuanzishwa kwa Khilafah Rashida

Chini ya mfumo wa sasa wa kimataifa, kile kinachoitwa uhuru si kitu zaidi ya usanii wa mchezo wa kuigiza, kwan maana ukombozi wa kweli (tahrir) uko pale tu dola inapoweza kupanga mambo yake ya ndani na mahusiano ya nje kwa mujibu wa itikadi yake. Watu wanaoamini “La ilaha illa Allah Muhammadur RasulAllah” kamwe hawatakombolewa kikweli mpaka watabikishe katika ardhi yao mfumo wa Kiislamu wa utawala, uchumi, jamii, elimu, na mahakama, pamoja na sera ya kigeni yenye msingi wa Da‘wah na Jihad. Hii ndiyo maana halisi ya uhuru, na katika suala hili, Pakistan bado haijakombolewa!

Soma zaidi...

Kashmir Haiwezi Kukombolewa Bila Kubadilisha Uongozi Unaopoteza Fursa ya Dhahabu ya Kuikomboa Kashmir, kwa ajili ya Kumfurahisha Trump

Leo, tarehe 5 Agosti 2025, miaka sita imepita tangu kuunganishwa kwa lazima kwa Kashmir Inayokaliwa kimabavu na Raja Dahir wa zama hizi, Modi. Kulingana na makubaliano yaliyofikiwa nchini Marekani, kuisalimisha Kashmir ilikuwa ni usaliti wa wazi wa uongozi wa kisiasa na kijeshi wa Pakistan wa wakati huo, serikali ya Bajwa-Imran. Miezi michache tu baadaye, Jenerali Bajwa aliendeleza usaliti huu kwa kutia saini makubaliano ya kusitisha mapigano, na Dola ya Kibaniani kuhusiana na Kashmir. Hata hivyo, usaliti huu dhidi ya Waislamu wanaodhulumiwa na wanyonge wa Kashmir uliendelea hata zaidi ya hapo.

Soma zaidi...

Njia ya Kujiondolea Dhambi ya Kuwatelekeza Waislamu wa Palestina, ni Kujitahidi Mchana na Usiku Kusimamisha Khilafah Rashida, na Kukusanya Majeshi

Kwa vile majeshi ya Waislamu hayakusonga kuinusuru Gaza, baba mwengine aliyedhulumiwa, Abu Umar, aliuawa shahidi, alipokuwa akiwatafutia watoto wake chakula. Alipokuwa akingoja kupokea msaada, risasi ya mdunguaji Myahudi muoga ilipenya kichwa chake. Yule rafiki aliyeuleta mwili wake alikuwa na njaa kwa siku tano, na akarudi kutoka kwenye kizingiti cha mlango wa shahada, labda kuuawa shahidi hivi karibuni. Hili sio tukio moja pekee. Makumi ya matukio kama haya yanashuhudiwa moja kwa moja kila siku, na Umma wa bilioni mbili.

Soma zaidi...

Usaliti wa Watawala wa Pakistan na Kukumbatia Kwao Uhalalishaji wa Mahusiano: Utangulizi wa Kujiunga na Mkataba wa Khiyana wa Abraham na Kutumikia Maslahi ya Amerika ya Trump na Umbile la Kiyahudi

Marekani ya Trump sasa inajitahidi kuunda "Mashariki ya Kati Mpya," ambayo inatumikia maslahi ya Marekani katika kanda hiyo, shauku kuu ikiwa ni kuhakikisha amani, usalama, na upanuzi wa kambi ya kijeshi ya Amerika katika Ulimwengu wa Kiislamu, inayojumuishwa ndani umbile la Kiyahudi. Inatafuta kuliweka umbile la Kiyahudi kama mamlaka kuu katika eneo hilo kisiasa, kiuchumi, na kimfumo. Licha ya haya yote, vibaraka wa Amerika ya Trump wamekimbilia kutekeleza mradi huu, na kutumikia maslahi ya bwana wao.

Soma zaidi...

Kati ya Usaliti wa Palestina na Kashmir na Utumwa kwa Amerika Asim Munir Anafanya Nini Mbele ya Firauni Wa Zama Zetu, Trump?

Katika wakati ambapo Amerika inapigana vita dhidi ya jirani Muislamu, Iran, kwa kutumia mkono wake mchafu katika eneo hilo, umbile la Kiyahudi, Rais wa Marekani, Donald Trump, alimkaribisha Mkuu wa Majeshi wa Pakistan mnamo Jumatano, 18 Juni 2025, kwa chakula cha mchana katika mkutano ambao haujawahi kushuhudiwa katika Ikulu ya White House. Kinachotia shaka kuhusu mkutano huu, na muda wake, ni kwamba ni mara ya kwanza kwa rais wa Marekani kumkaribisha mkuu wa jeshi la Pakistan katika Ikulu ya White House, bila ya kuwepo kwa afisa yeyote mkuu wa kiraia wa Pakistan, kuashiria umuhimu wa mkutano huo, na unyeti wa mada yake.

Soma zaidi...

Katikati ya Tabasamu za Idd na Machozi ya Gaza: Wito kwa Maafisa na Wanajeshi

Huku Waislamu wakijiandaa kukaribisha Idd al-Adha na kusherehekea pamoja na watoto wao na wenza wao katika siku hizi za sherehe, tunaelekeza ujumbe huu makhsusi kwa wanajeshi na maafisa wanyoofu wa jeshi la nyuklia la Pakistan, na majeshi mengine ya Ummah kwa jumla. Tunawakumbusha katika siku hizi kwamba wamewatelekeza watu wao wenyewe, wanawake, watoto, wazee, na wanaume katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina na Gaza, na hawakujitokeza kuwanusuru licha ya kuwa na uwezo wa kufanya hivyo.

Soma zaidi...

Farauni wa Washington Afanya Maangamizu Makubwa Gaza, Kwa Usaidizi Kamili wa Viongozi wa Kijeshi na Kisiasa wa Waislamu na Mayahudi. Jibu Pekee la Kisharia ni Uhamasishaji wa Majeshi ya Waislamu. Enyi Waislamu! Songeni kwa ajili ya Faradhi ya Kishar

Bila jeshi hata moja la Waislamu kumzuia, Trump alitimiza ahadi yake ya kufanya maangamizi makubwa Gaza. Kamera zimenasa picha za sehemu za miili ya waumini zikipaa angani, juu ya majengo marefu, kutokana na kukithiri kwa mashambulizi ya makombora. Madaktari wa uokoaji wanafunikwa macho na kupigwa risasi. Watoto, wanawake, wazee na waliojeruhiwa wanauawa shahidi kwa kulipuliwa mahema yao. Sera ya njaa ya Amerika, iliyotekelezwa na wafuasi wake, umbile la Kiyahudi, imeongeza mateso hadi kiwango cha baa la njaa. Sasa imedhihirika kwa kila mtu kwamba Firauni wa Washington anafanya maangamizi makubwa kwa Gaza, kwa usaidizi kamili wa kijeshi na uongozi wa kisiasa wa Waislamu na Mayahudi.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu