Usekula Unapanda Uovu Wake kwa Dini Kuu
- Imepeperushwa katika Kenya
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Tunakemea vikali sheria hizi ambazo kwa uhalisia ni dhihirisho la uchafu na ufisadi wa fikra ya kisekula ambayo imewapa wanadamu uhuru wa kutunga sheria na kukiuka utukufu wa kidini. Tunaeleza kinaga ubaga kuwa sheria hizi zilizopendekezwa ni kinyume na ile inayodaiwa kuwa ni haki ya kikatiba ya uhuru wa kuabudu na kwamba dola haipaswi kuingilia dini!