Jumatatu, 23 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/15
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Majibu ya Aibu ya Tawala katika Nchi za Waislamu kwa Uvamizi wa Umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran!

Yeyote anayetazama miitikio ya tawala zilizopo katika ardhi za Waislamu kwa mashambulizi ya umbile la Kiyahudi dhidi ya Iran atahisi huzuni kubwa na masikitiko kwa hali ya sasa ya Waislamu. Wengine wamelaani na kushutumu pekee; wengine wameonyesha hofu ya machafuko katika eneo hilo kutokana na mashambulizi haya. Baadhi walieleza kuwa ni ongezeko la hatari; wengine walielezea wasiwasi wao juu ya athari zake kwa kadhia ya Palestina. Wengine hata walitangaza kuwa tayari kufanya upatanishi kati ya Iran na umbile la Kiyahudi. Walio bora zaidi walionyesha nia ya kuiunga mkono Iran katika majukwaa ya kimataifa, huku baadhi ya nchi hizo hizo zikifungua anga zao kwa ndege za umbile la Kiyahudi kuruka juu, kuipiga Iran kwa mabomu, kuua na kuharibu, na kisha kuregea bila hata risasi moja kufyatuliwa kwao! Wengine walinasa makombora na droni za Iran zilizolenga kushambulia umbile la Kiyahudi, na hivyo kuwaepusha na kupigwa!

Enyi Waislamu: Adui Yenu Anaujua Uzito Wenu Vizuri Kuliko Mnavyoujua nyinyi, na Anakuogopeni Nyinyi na Anakuchukulieni Kwa Umakini Mara Elfu!

Siku baada ya siku, matukio na misimamo inafichua ushahidi mwingi wa dola za kikoloni za kikafiri kuwaogopa Waislamu, ikiwemo umbile vamizi la Kiyahudi. Pia inaonyesha kwamba wanapoamiliana na Waislamu, wanawachukulia kwa uzito mara elfu moja. Baada ya zaidi ya karne moja, baada ya kuvunjwa kwa Khilafah, kugawanyika kwa Waislamu na kuwa maumbo dhaifu, nyenyekevu, ikifuatwa na udanganyifu na uvamizi wa kifikra, kujitenga kwa Waislamu na imani yao, kuporwa mali ya Waislamu, kupanuka kwa ushawishi wa wakoloni hao makafiri katika ardhi zao, na kudhoofika kwao na kudhalilika, baadhi wanasema: Waislamu kamwe hawatainuka tena, na baada ya haya yote, tunasikia na kuona kauli kutoka kwa viongozi wa Magharibi na viongozi wa umbile vamizi la Kiyahudi, ambazo zinaonyesha hofu yao ya Uislamu na hofu iliyojaa nyoyoni mwao kutoka kwa Waislamu katika hali hii.

Vyombo vya Usalama katika Mji wa Al-Qadarif Vyawakamata Mashababu wa Hizb ut Tahrir vikiliunga mkono umbile la Kiyahudi!

Katika hotuba ya hadhara iliyotolewa na Mashababu wa Hizb ut Tahrir katika mji wa Al-Qadarif, kwenye soko la Al-Qadarif karibu na hospitali ya meno, mnamo siku ya Alhamisi, tarehe 23 Dhul-Hijjah 1446 H, inayolingana na 19/6/2025 M, Ustadh Awad Muhajir, mwanachama wa Hizb ut Tahrir, alizungumza kuhusu uhalisia wa vita na umbile la Kiyahudi, furaha ya Waislamu kwa mashambulizi dhidi ya umbile hili, na kiu ya watu ya ushindi dhidi ya mkaaji huyu wa kimabavu wa ardhi tukufu—Masrah ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw). Alithibitisha faradhi ya kusimamisha Khilafah Rashida kwa njia ya Utume, ambayo itaikomboa Palestina na ardhi nyenginezo za Kiislamu zinazokaliwa kwa mabavu. Hadhira iliitikia vyema hotuba hiyo, na kulikuwa na michangio tofauti tofauti kutoka kwa waliohudhuria.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu