Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Bangladesh

H.  24 Dhu al-Hijjah 1445 Na: H 1445 / 30
M.  Jumapili, 30 Juni 2024

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Utiifu Wakuendelea kwa India unathibitisha kwamba Serikali ya Hasina ni Tishio kwa Ubwana wa Nchi; na Wajibu wa Vikosi vya Jeshi, Mlinzi wa Ubwana huu, ni kuiondoa mara moja Serikali ya Hasina

(Imetafsiriwa)

Ili kuonyesha uaminifu wake usioyumbayumba kwa India, Hasina aliondoka bila kuchelewa hadi New Delhi (Juni 21, 2024) kukutana na Waziri Mkuu mpya aliyechaguliwa wa India. Katika ziara hii, Hasina alitia saini Mikataba 10 ya Maelewano (MoU) kwa ajili ya India. Hasa, India imepewa usafiri wa Reli katikati mwa nchi hii ili kusaidia kuanzisha muunganisho wa kimkakati kati ya eneo la mashariki na eneo la magharibi mwa India, ambayo inasababisha hasira kubwa ya umma. Katika kujibu, Hasina alisema, “Angalia Ulaya, hakuna mipaka” [Prothom Alo, Juni 25, 2024]. Kwa kweli, kauli yake, akitoa mfano wa Ulaya, ilifichua nia yake mbaya ya kuunganisha Bangladesh na India. Hoja hii inawekwa wazi zaidi anaposema, India iliikomboa Bangladesh kwa damu yake [Hindustan Times (Bangla), Juni 25, 2024]. Serikali ya Hasina ni kipofu kwa India kiasi kwamba haijali kuhusu mauaji ya mara kwa mara ya wakulima wetu wasio na hatia, kuwakamata wavuvi wetu, kuwakamata na kuwaua wanachama wetu wa usalama wa mpakani (BGB). [قَاتَلَهُمُ اللّهُ أَنَّى يُؤْفَكُونَ] “Mwenyezi Mungu awaangamize! Wanageuzwa namna gani hawa!” [Surah At-Tawbah: 30].

Enyi Wananchi, katika ziara hiyo pia kulikuwa na utiaji saini Mkataba wa Maelewano kati ya Chuo cha Mafunzo ya Watoaji Huduma za Ulinzi (DSSC), Wellington na Chuo cha Mafunzo ya Watoaji Amri na Huduma za Ulinzi (DSSC), Mirpur kwa ajili ya ushirikiano katika elimu ya kijeshi katika masomo ya kimkakati na operesheni. Lengo kuu lilikuwa ni kuweka udhibiti zaidi juu ya jeshi la Bangladesh. Mnajua jinsi India ilivyotekeleza mchakato wa kudhoofisha jeshi la nchi hii kupitia mauaji ya Pilkhana kwa msaada wa serikali ya Hasina, ambayo ni dhahiri kama mchana katika taarifa ya hivi karibuni ya aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa BGB, msaliti Mkuu (mstaafu) Mainul Islam [Kilichotokea Pilkhana siku hiyo katika taarifa ya DG Mainul, Daily Manab zamin, Februari 26, 2024]. Kwa hakika dola ya Hindutva ya India ni adui wa Waislamu, uvamizi wa India dhidi ya Waislamu wa eneo hilo ni sawa na uvamizi wa dola ya Kiyahudi inayokalia kwa mabavu dhidi ya Waislamu wa Palestina. Na Hasina ni mmoja wa watawala wa Waislamu ambao kupitia kwao India inatawala nchi hii. Mwenyezi Mungu (swt) asema,

[لَتَجِدَنَّ أَشَدَّ النَّاسِ عَدَاوَةً لِّلَّذِينَ آمَنُواْ الْيَهُودَ وَالَّذِينَ أَشْرَكُواْ]

“Hakika utawakuta walio shadidi kuliko watu wote katika uadui kwa walio amini ni Mayahudi na washirikina.” [Surah Al-Ma'idah: 82].

Enyi Maafisa Wanyoofu katika Jeshi, nyinyi ni warithi wa Mohammad Bin Qasim, Ikhtiyar Uddin Mohammad Bin Bakhtiyar Khilji, ambao walikomboa eneo hili kutoka mikononi mwa wafalme wa Hindutva kwa kutoa kafara damu yao. Kwa kutambua damu ya askari wa India, dola ya washirikina iliyoingilia ardhi za Kiislamu kwa jina la vita vya uhuru, kimsingi Hasina anakanusha damu tukufu ya askari mashujaa wa Kiislamu na kuusaliti Umma wa Kiislamu. Na kuitiisha nchi hii kwa Mfalme Dahir wa zama hizi na kuhatarisha ubwana wa nchi. Ni lazima mutambue kuwa mamlaka ya nchi hii yako mikononi mwenu na watu wa nchi hii wanakutakeni muiondoe serikali ya Hasina na mulinde ubwana wa nchi hii. Mtume (saw) amesema,

«إِنَّمَا الْإِمَامُ جُنَّةٌ يُقَاتَلُ مِنْ وَرَائِهِ وَيُتَّقَى بِهِ» “Hakika Imam (Khalifa) ni ngao watu hupigana nyuma yake na hujihami kwaye” (Sahih Muslim). Hivyo basi, Hizb ut Tahrir inakulinganieni mutimize wajibu wenu wa Iman kwa kuipa Nusrah Hizb ut Tahrir katika kusimamisha Khilafah kwa njia ya Utume na muwe waanzilishi katika kulinda ubwana wa Umma wa Kiislamu.

[إِلاَّ تَنفِرُوا يُعَذِّبْكُمْ عَذَابًا أَلِيمًا وَيَسْتَبْدِلْ قَوْمًا غَيْرَكُمْ وَلاَ تَضُرُّوهُ شَيْئًا وَاللَّهُ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ]

“Kama hamwendi atakuadhibuni adhabu chungu, na atawaleta watu wengine, wala nyinyi hamtamdhuru chochote. Na Mwenyezi Mungu ni Muweza wa kila kitu.” [Surah At-Tawbah: 39].

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir
katika Wilayah Bangladesh

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Bangladesh
Address & Website
Tel: ‎+88 01798 367 640‎
www.ht-bangladesh.info
E-Mail: contact@ht-bangladesh.info, htmedia.bd@outlook.com Skype: htmedia.bd

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu