Jumapili, 27 Safar 1446 | 2024/09/01
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Pongezi za Idd Al-Adha Iliyobarikiwa 1445 H

Hizb ut Tahrir inatoa pongezi na baraka zake za dhati kwa Umma wa Kiislamu, wenye kulemewa na majeraha na kustahamili shinikizo la moja kwa moja na lisilo la moja kwa moja la kikoloni. Kwa mnasaba huu, tunawataja makhsusi watu wetu wenye subira mjini Gaza Hashim na kwa jumla katika Ardhi Iliyobarikiwa ya Palestina, tukimuomba Mwenyezi Mungu azifanye siku za Idd hii kuwa chanzo cha utulivu wa nyoyo zao.

Soma zaidi...

Hizb ut Tahrir / Wilayah Pakistan: Kutaka Kuhamasishwa Majeshi ili Kuinisuru Gaza Kutaendelea licha ya Ukamataji Mashababu wa Hizb ut Tahrir!

Watawala wa Pakistan wanawatia mbaroni miongoni mwa safu za Hizb ut Tahrir/Wilayah Pakistan ili kuizuia Hizb kutaka kuhamasishwa jeshi la Pakistan kuinusuru Gaza. Lakini Umma mzima unatoa wito kwa majeshi yake kupigana jihad ili kufikia moja kati ya mema mawili ili kuukomboa Msikiti uliobarikiwa wa Al-Aqsa, basi ukamataji huo utawazuia vipi watu wake?!

Soma zaidi...

Baraza la Usalama liko “Mfukoni mwa Marekani” Likiendeshwa na Maslahi yake na Maslahi ya Mayahudi na Wakoloni wa Makafiri

Mnamo tarehe 11/6/2024, Baraza la Usalama lilitoa azimio la kuunga mkono mradi wa Biden kwa ajili uvamizi wa kikatili wa Kiyahudi dhidi ya Gaza, bali Palestina yote! Maandishi ya azimio hilo, kama yalivyochapishwa na CNN, mnamo tarehe 11 Juni 2024, yalisema yafuatayo: (Baraza la Usalama “linakaribisha pendekezo jipya la kusitisha mapigano lililotangazwa mnamo Mei 31, ambalo lilikubaliwa na ‘Israel,’ na kutoa wito kwa Hamas pia kulikubali, na kuzitaka pande husika zikubali kutekeleza masharti yake kikamilifu bila kuchelewa na bila masharti.”

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu