Waziri wa Fedha Hawezi Kurekebisha Uchumi wa Pakistan Unaodhibitiwa na IMF
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
- |
Waziri wa Fedha wa Pakistan, Bw. Ishaq Dar mnamo Jumapili, tarehe 16 Oktoba 2022, aliusihi Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) na wafadhili wa kimataifa kutoa usaidizi mkubwa wa kisera. Aliiomba IMF kuunda muitiko wake kuafikiana na hali ya Pakistan na nchi zilizo na hali kama hiyo kwa kuzingatia changamoto kubwa za kiuchumi, kijamii na kisiasa zinazokabiliana nazo huku kukiwa na majanga yanayosababishwa na tabianchi, kulingana na taarifa moja kwa vyombo vya habari iliyotolewa na wizara ya fedha.