Jumatano, 25 Rabi' al-awwal 1447 | 2025/09/17
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu
kesho kutwa

kesho kutwa

Hizb ut Tahrir / Wilayah Tunisia ni mwenyeji wa Kongamano la Kimataifa la Wanawake “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu” Lililoandaliwa na Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya

Mnamo Jumamosi 27 Oktoba 2018, Hizb ut Tahrir Wilayah ya Tunisia itakuwa mwenyeji wa kongamano muhimu la kimataifa la wanawake lililoandaliwa na Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kwa kichwa, “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu” ili kutatua janga linaloathiri uwiano na umoja wa ndoa na familia katika jamii ulimwenguni, ikijumuisha ardhi za Waislamu. Tukio hili adhimu litawakusanya wanawake waliopendekezwa kutoka Tunisia na nchi nyinginezo, ambao ni viongozi mashuhuri katika jamii zao au walio na ujuzi kuhusiana na mada hii.

Kampeni ya Kimataifa: “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu” iliyo Zinduliwa na Kitengo cha Wanawake Katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir

Mnamo 3 Oktoba, Kitengo cha Wanawake katika Afisi Kuu ya Habari ya Hizb ut Tahrir kilizindua kampeni muhimu ya kiulimwengu kwa anwani, “Familia: Changamoto na Suluhisho la Kiislamu” ambayo itamalizikia katika kongamano la kimataifa la wanawake mwishoni mwa Oktoba litakalo hudhuriwa na wazungumzaji kutoka pembe zote za dunia.

Faini ya Kwanza ya Denmark kwa Wanawake Wanaovaa Niqab Itawasukuma Waislamu Kushikamana na Maadili ya Kiislamu Hata Zaidi!

Mnamo Agosti 4, 2018, shirika la habari la BBC liliripoti juu ya mwanamke wa kwanza wa Kiislamu kulipishwa faini nchini Denmark kwa ajili ya kuvaa niqab hadharani. “Bunge la Denmark liliidhinisha mswada mnamo Mei 2018 wa kumwadhibu yeyote anayevaa niqab kwa faini” (BBC, 31 Mei 2018). Kwa sasa sheria hiyo haitaji burka na niqab kwa majina, bali inaeleza, “Yeyote anayevaa nguo inayofinika uso hadharani ataadhibiwa kwa faini”. Marufuku hiyo ilipangwa kuanza utekelezwaji wake mnamo Agosti 2018. Mnamo Ijumaa 3 Agosti 2018 mwanamke wa Kiislamu mwenye umri wa miaka 28 aliyekuwa amevaa niqab katika soko kuu la hadhara mjini Horshom, km 25 (maili 15) kaskazini mwa Copenhagen, alishambuliwa kwa nguvu na mwanamke mwengine aliyepinga vazi lake na kuchukua hatua mikononi mwake kumvua kwa lazima vazi hilo la Kiislamu. Polisi waliitwa katika eneo hilo la “vita” na baada ya kuangalia kanda ya CCTV walimweleza mwanamke huyo wa Kiislamu kuwa angelipishwa faini ya kroner 1,000 ($155; £120) baada ya kukataa kuvua niqab hiyo kwa agizo la polisi. Kwa sasa faini hiyo imeongezeka mara kumi zaidi hadi kroner 10,000 ($1,500; £1,200) kwa wahalifu wanaorudia kosa.

Jiunge kwa hii RSS feed

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu