Ziara ya Usaliti
- Imepeperushwa katika Habari na Maoni
- Kuwa wa kwanza kutoa maoni!
Katika wakati ambapo ulimwengu wa Kiislamu unavuja damu—kuanzia Gaza hadi Kashmir, hadi barabara za Tehran—ziara ya Jenerali Asim Munir kwa Rais wa Marekani Donald Trump si tu kwamba ni uziwi bali ni usaliti wa kiasi kikubwa. Mkutano huo, uliofanyika katika Ikulu ya White House na uliandaliwa na Trump kama ishara ya kushukuru dori ya Munir katika kutuliza hali iliyokaribia vita na India, inasifiwa na sehemu za utawala wa Pakistan kama hatua ya kimkakati ya kidiplomasia.