Ijumaa, 19 Ramadan 1445 | 2024/03/29
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

بسم الله الرحمن الرحيم

 Kenya: Kampeni na Amali za Kutaka Kuachiliwa Huru kwa Naveed Butt!

Zaidi ya miaka tisa imepita tangu serikali nchini Pakistan imteke nyara mhandisi Naveed Butt, msemaji rasmi wa Hizb ut Tahrir katika Wilayah Pakistan, na tangu alipotekwa nyara haijulikani alipo!

Katika suala hili, mnamo Jumanne 29 Juni 2021, Hizb ut Tahrir / Kenya ilituma ujumbe kwa Ubalozi wa Pakistan jijini Nairobi na ujumbe huo ulioongozwa na mwakilishi kwa vyombo vya habari wa Hizb ut Tahrir nchini Kenya Shabani Mwalimu aliandamana na Ustadh Yassin Kiwayo, Mkuu wa Kamati Kuu ya Mawasiliano ya Hizb ut Tahrir / Kenya na Bwana Yusuf Gasana mwanachama wa Hizb ut-Tahrir nchini Kenya. Ujumbe ulikutana na kuzungumza na Bwana Charles, mmoja wa wafanyikazi wa ubalozi huo, ambaye aliahidi kuziwasilisha nakala tatu za taarifa kwa vyombo vya habari kwa lugha tatu; Kiurdu, Kiarabu na Kiingereza, kwa Balozi.

Baada ya swala ya Ijumaa mnamo 02 Julai 2021, Hizb ut Tahrir nchini Kenya aliandaa msururu wa amali za kuonyesha kadhia ya Ndugu Naveed Butt kwa kumnusuru na kumuombea nusra, ikitaka aachiliwe mara moja, na imam wa Msikiti wa Taqwa, Sheikh Muhammad Ali, alisoma taarifa iliyotolewa na Afisi Kuu ya Habari kwa anwani "Wito wa Kutaka Kumalizwa kwa Kupotezwa kwa Nguvu kwa Naveed Butt Nchini Pakistan" kwa walio swali baada ya swala ya Ijumaa. Mwenyezi Mungu (swt) anawatunza waja wema.

Ijumaa, 21 Dhu al-Qa'adah 1442 H sawia na 02 Julai 2021 M

#FreeNaveedButt 

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

rudi juu

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu