Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Afisi ya Habari
Wilayah Misri

H.  12 Sha'aban 1445 Na: 1445/21
M.  Alhamisi, 22 Februari 2024

Taarifa kwa Vyombo vya Habari

Kinachopaswa kufanywa na Misri na Jeshi Lake ni Kuvunja Mipaka na Kuling'oa Umbile la Kiyahudi, Sio Kutafuta Usitishaji Vita na Kutoa Misaada!
(Imetafsiriwa)

Balozi Ahmed Abu Zaid, msemaji rasmi wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri, alisisitiza kuwa ‘Israel’ lazima ikomeshe ukiukaji wake, akithibitisha kuwa Israel inakiuka sheria za kimataifa. Alidokeza kuwa maamuzi ya haki ya kimataifa yanaifunga ‘Israel’. Msemaji rasmi wa Wizara ya Mashauri ya Kigeni ya Misri, alipopiga simu kwa Idhaa ya Habari ya Cairo, alithibitisha kwamba 'Israel' inahusika na kuwahamisha Wapalestina na inafanya kazi ya kuhujumu haki za watu wa Palestina. Amebainisha kuwa ‘Israel’ inafuata sera ya mauaji ya halaiki dhidi ya Wapalestina, na shinikizo lazima litolewe kwa ‘Israel’ kuacha matendo yake dhidi ya Wapalestina. Msemaji huyo wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri pia amesisitiza ulazima wa kusitisha mapigano katika Ukanda wa Gaza na kuthibitisha kuwa Washington haichukui msimamo unaoendana na wajibu wake, na hoja ya Washington ya kutumia kura ya turufu haina mashiko. Amesisitiza kuwa, Misri inafanya kila juhudi kufikia usitishaji vita katika Ukanda wa Gaza na inapiga hatua kubwa katika kutoa msaada zaidi kwa sekta hiyo. (Al-Yawm Al-Sabi’, 21/02/2024)

Wale wanaosikiliza maneno ya msemaji huyo wanaweza kufikiri kwamba anazungumza kwa niaba ya nchi huru yenye mamlaka yake ya kufanya maamuzi. Hata hivyo, ukweli ni kwamba utawala wa Misri unaenda tu kulingana na unavyoamriwa na Marekani na kile kinachotumikia maslahi yake ndani ya mfumo wa utekelezaji miradi ya Marekani. Ndio maana tunauona utawala wa Misri ukiregelea dira ya Marekani ya suluhisho la dola mbili kama njia ya kutatua kadhia ya Palestina. Sasa, katikati ya uchokozi wa Kiyahudi na kukaribia kwa mwezi mtukufu wa Ramadhan, Magharibi, ikiongozwa na Marekani, inahofia kuendelea kwa vita na mauaji yaliyokithiri, ambayo bila shaka yatachochea hisia za Waislamu kote ulimwenguni. Hili linaweza kusababisha matukio ya mlipuko, na pengine kusababisha kuporomoka kwa serikali za vibaraka wateja na nchi kujinasua kutokana kwa utiifu wa Magharibi, na pengine hata zaidi ya hapo. Uislamu unaweza kuingia madarakani, kuashiria mwisho kamili wa utawala wa Magharibi na mradi wao wa kikoloni, ikiwa ni pamoja na ngome yao ya juu katika ardhi zetu, umbile la Kiyahudi.

Jumuiya ya kimataifa, ikiongozwa na Marekani na washirika wake, imetabanni sera ya ukinzani wa maneno na vitendo kuhusu mauaji ya halaiki huko Gaza Hashem. Imedhihirika kwamba matamshi kama vile kulaani, mabishano na maombolezo yana lengo la kutuliza rai jumla na kutoa kuficha mauaji ya Mayahudi, wakati uhalisia unathibitisha uungaji mkono wa wazi, wa Marekani na wafuasi wake, kwa mauaji ya Mayahudi kupitia kifedha, kijeshi na msaada wa kidiplomasia. Vile vile, utawala wa Misri, kupitia sera zake za kigeni, haufanyi kazi kwa niaba ya watu wetu wa Palestina bali unalenga kuhifadhi umbile la Kiyahudi na kudumisha uthabiti wa ruwaza ya Marekani, ambayo inalenga kusuluhisha kadhia ya Palestina. Hata hivyo, kutatua kadhia ya Palestina hakutafikiwa kupitia sheria za kimataifa au Mahakama ya Kimataifa ya Uadilifu, na Mayahudi hawataacha ukiukaji wao maadamu kuna wale miongoni mwetu wanaoielekea jumuiya ya kimataifa na taasisi zake ambazo zimeunda na kuunga mkono bila kikomo umbile hili lemavu.

Hatua ya kweli itakayotawala kwa watu wetu katika Ardhi Iliyobarikiwa ni kuvunja mipaka na kuhamasisha majeshi kuling'oa umbile la Kiyahudi. Hakuna suluhisho jengine. Mayahudi na walio nyuma yao hawatazuiliwa isipokuwa kwa harakati ya ikhlasi kutoka kwa majeshi, hususan jeshi la Al-Kinanah, ambalo linaweza kuikomboa Palestina yote na kuling'oa umbile la Kiyahudi katika muda wa masaa machache. Lakini kabla ya hili, watawala wa nchi zetu wanaolinda umbile la Kiyahudi na kuba lake halisi la chuma lazima wang'olewe. Wao ndio wanaosimama kati ya Umma na majeshi yake, kati ya ukombozi wa Palestina na kunusuriwa kwa watu wake wanaodhulumiwa. Hili ndilo suluhisho, na kitu chengine chochote sio suluhisho bali ni majaribio ya kusuluhisha kadhia ya Palestina, ambayo ni kadhia ya Umma mzima. Hakuna faida ya mapatano au mikataba maadamu adui mnyakuzi na walinzi wake wanabaki wamejikita madarakani katika nchi zetu.

Enyi Askari wa Al-Kinanah: Sababu ya Palestina ni sababu ya Ummah na kitovu chake cha mazingatio; na ardhi yake ni ardhi ya Kharaji ambayo umiliki wake ni wa Ummah mzima. Wajibu wa kuikomboa unaangukia Ummah wote, hasa nchi zinazoizunguka. Ni wajibu wa faradhi zaidi juu ya Misri na jeshi lake. Leo, hakuna udhuru wa kuwa watiifu kwa watawala wanaowalinda Mayahudi. Bali, wajibu ni kuwang’oa, kuzikomboa ardhi zetu kutokana na uchafu wao, na mara moja kuyakusanya majeshi kuelekea ukombozi wa Masra ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) na usaidizi (nusrah) kwa watu wetu katika Ardhi Iliyobarikiwa. Huu ndio wajibu wa wakati huu, na chochote kidogo kuliko hicho ni fedheha ambayo itatusumbua sisi na watoto wetu, na haitafutika isipokuwa kwa vitendo na uchocheaji wa kuendelea kwa wenye ikhlasi katika majeshi. Mwenyezi Mungu amsikie na amjibu mtu mwema ambaye atang'oa mifumo ya dhulma na madhara, na kutangaza kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, Dola inayotekeleza Uislamu, inayowanusuru watu wake, na kuyakusanya majeshi ili kuregesha ardhi yake na matukufu yake.

Enyi Askari wa Al-Kinanah, enyi wapiganaji bora: Kheri inastahiki tu wale wanaobeba bendera (rayah) ya Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw) kwa haki, kama mujahidina katika njia ya Mwenyezi Mungu, wasaidizi wa wanaodhulumiwa, watiifu kwa Mwenyezi Mungu, Mtume wake na Dini yake. Hawamtii yeyote juu ya kumtii Mwenyezi Mungu na Mtume Wake, wala hawawatii watawala wanaofuata amri za Magharibi na kutekeleza miradi yao ya kikoloni, inayowazuia kukomboa matukufu ya Ummah na kuwasaidia wanaodhulumiwa miongoni mwao. Hawa ndio kweli wanaostahiki kheri. Je, nyinyi ni miongoni mwao? Kheri iko katika wale wanaofuata nyayo za Qutuz, ambaye anajifanya yeye na askari wake kuwa ngao kwa Ummah huu, wakiulinda na itikadi yake. Anawakusanya wenzake, akiwakumbusha Mwenyezi Mungu na siku zake na jihad katika njia yake, kutafuta pepo yake na radhi zake. Basi mko wapi, enyi vizazi wa Qutuz na Baybars, washindi wa Matartari, kutoka kwa Matartari wa zama hizi? Na mko wapi, enyi kizazi cha Salahuddin, warithi wa ukombozi wa Al-Aqsa, kutokana na unajisi wa Makruseda na vita vyao vipya dhidi ya Uislamu na watu wake? Nani atakaye unusuru Uislamu ikiwa si nyinyi pamoja na wanaounusuru?

Ni amana kutoka kwa Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), basi ilindeni na muwe watu wake, ngao kwa Umma huu, walinzi wake. Msiwe mashahidi wa uwongo ambao wanaona yanayotokea kwa Ummah kama viziwi na mabubu wasioelewa. Na lau kuwa Mwenyezi Mungu angelijua kheri yoyote ndani yao, angaliwafanya waisikie. Basi sikilizeni, huenda Mwenyezi Mungu akakuandikieni kheri na kupitia kwenu, na Uislamu na watu wake utakirimiwa kwa mikono yenu.

[وَالَّذِينَ آمَنُوا وَهَاجَرُوا وَجَاهَدُوا فِي سَبِيلِ اللَّهِ وَالَّذِينَ آوَوا وَّنَصَرُوا أُولَٰئِكَ هُمُ الْمُؤْمِنُونَ حَقًّا ۚ لَّهُم مَّغْفِرَةٌ وَرِزْقٌ كَرِيمٌ]

“Na walio amini wakahama na wakapigana Jihadi katika Njia ya Mwenyezi Mungu, na walio toa mahala pa kukaa na wakanusuru, hao ndio Waumini wa kweli. Watapata msamaha wa Mwenyezi Mungu na kuruzukiwa kwema.” [Al-Anfal:74].

Afisi ya Habari ya Hizb ut Tahrir katika Wilayah Misri

Hizb-ut Tahrir: Afisi ya Habari
Wilayah Misri
Address & Website
Tel: 
http://hizb.net/
E-Mail:  info@hizb.net

Andika maoni

Hakikisha umejaza (*) habari zinazohitajika palipoashiriwa. Kodi za HTML haziruhusiwi.

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu