Ijumaa, 24 Rabi' al-awwal 1446 | 2024/09/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Watoto wa Iraq … Uhalisia Unaoogofya na Mustakbali Unaotoa Bishara ya Miaka Mingi ya Kuzorota!

Hazina inayoshughulikia maswala ya watoto ya Umoja wa Mataifa (UNICEF) imesema katika ripoti iliyotolewa mnamo Ijumaa 19/1/2018 kuwa watoto 270 waliuwawa nchini Iraq mwaka jana kwa sababu ya vita vilivyo anzishwa na serikali ya Iraq dhidi ya ISIS. Vita hivi pia vilisababisha watoto 1.3 milioni kukosa makao miongoni mwa 2.6 milioni waliokosa makao kutokana na vita hivi vya miaka mitatu. Kulingana na taarifa hiyo, watoto milioni nne katika mikoa ya Nineveh na Anbar waliathirika na ghasia hizo na watoto wengi walilazimika kushiriki katika vita safu za mbele. Taarifa hiyo ilifichua kwamba umasikini na mizozo ilisababisha kusita kwa mchakato wa elimu kwa watoto milioni tatu kote nchini Iraq, baadhi yao wakikosa kabisa fursa ya kukaa ndani ya darasa katika maisha yao yote, huku zaidi ya robo ya watoto wa Iraq wakiishi ndani ya umasikini.

Soma zaidi...

Watoto wa Rohingya Wanadhalilishwa Mikononi mwa Mabudha! Je, Wanaye Mtetezi?

Shirika la misaada la Médecins Frontiéres, limeripoti kuwa zaidi ya nusu ya wasichana katika kambi ya wakimbizi wa Rohingya eneo la Cox's Bazar, Bangladesh ambao limewatibu baada ya kudhulimiwa kimapenzi na kubakwa nchini Myanmar wako chini ya umri wa miaka 18, na wengine wako chini ya miaka 10. Limeeleza kuwa mamia ya wasichana wa Rohingya wamepewa usaidizi wa kimatibabu na wa kisaikolojia katika kliniki yake mjini Kutupalong inayotibu wahanga wa dhulma za kijinsia lakini likasisitiza kuwa hao ni sehemu tu ya wale wanao amanika kudhulumiwa kimapenzi na kubakwa na majeshi katili ya kibudha tangu kutokea kwa kampeni ya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wa Rohingya mnamo Agosti

Soma zaidi...

Gharama Kubwa Inayolipwa na Raia Eneo la Deir al-Zour Na Watawala wa Waislamu katika Meza ya Majadiliano kwa Kuketi na Kukutana na Muuwaji

Ndege za kivita za Urusi, kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya kimaeneo kutoka Deir al-Zour, zimefanya mashambulizi ya msururu wa mabomu juu ya feri za mtoni zilizokuwa zimebeba maelfu ya raia wanaokimbia eneo la Deir al-Zour kuelekea maeneo mengine, yakisababisha zaidi ya vifo hamsini na maelfu kujeruhiwa, wengi wao wakiwa ni watoto na wanawake.

Soma zaidi...

Huku wakitelekezwa na Serikali Zisizo na Utu za Waislamu, Wanawake na Watoto wa Kiislamu Wakimbizi wa Rohingya Wanakabiliwa na Baa la Njaa, Maradhi na Vifo Nchini Bangladesh

Mnamo Jumapili 17 Septemba, shirika la msaada la ‘Save the Children’ lilionya kuwa wakimbizi wa Rohingya nchini Bangladesh huenda wakafariki kutokana na uhaba wa chakula, makao, na bidhaa msingi za usafi. Zaidi ya Waislamu wa Rohingya 410,000 wamekimbia Myanmar na kwenda Bangladesh tangu Agosti 25 kutokana na kampeni ya mauaji ya halaiki inayotekelezwa na jeshi la Burma. Kwa mujibu wa shirika la UNICEF, asilimia 80% ya wakimbizi hawa ni wanawake na watoto, 92,000 kati yao wako chini ya umri wa miaka 5, na takriban wanawake 52,000 ni waja wazito au wananyonyesha.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu