Jumamosi, 21 Muharram 1446 | 2024/07/27
Saa hii ni: (M.M.T)
Menu
Main menu
Main menu

Kwa Kukosekana Khilafah Wanawake Waheshimiwa wa Ash-Sham Wanakabiliwa na Kudhulumiwa Hata na Wale Wanaodai Kuwa Walinzi Wao!!!

Ripoti mpya ya shirika la Umoja wa Mataifa linalo shughulikia ufadhili wa watu (UNFPA) limesema kuwa wanawake katika kambi za wakimbizi nchini Syria wamekuwa wakidhulumiwa kimapenzi na wanaume wanaotoa misaada kwa niaba ya UM na mashirika ya kimisaada ya kimataifa. Ripoti hiyo, “Sauti kutoka Syria 2018”, ili eleza kwa kina namna wanawake wakimbizi wa Syria wanavyo lazimishwa kutoa ngono kama badali kwa chakula kutoka UM, na kwamba dhulma hii imeenea maeneo yote kusini mwa Syria.

Soma zaidi...

Watoto wa Mashariki Mwa Ghouta Wanaangamizwa! Ni Nani Atakaye Hifadhi Damu Zao?!!

Mnamo 22 Februari, shirika la Kiingereza la kuchunguza haki za kibinadamu za watu wa Syria lilisema kuwa zaidi ya watu 400 waliuwawa, ikiwemo watoto 150 katika shambulizi baya la mabomu lililopita la siku 5 Mashariki mwa Ghouta lililofanywa na majeshi katili ya Syria na Urusi, ambayo yanalenga kiholela nyumba za raia, maduka, mashule, mahospitali na masoko, yakiwaacha watoto wakiwa wamezikika katika vifusi vya majumba. Watoto wamelazimika kutafuta hifadhi katika mapango, mashimo au mivungu ya nyumba zao huku 'wakisubiri zamu yao kufa'.

Soma zaidi...

UN – Wanaotarajiwa Kuwa Walinzi Ndio Wauwaji!!

Gazeti la Uingereza la The Times, lilichapisha ripoti kwa kichwa "Wafanyikazi wa UM 'wanahusika na ubakaji 60000 kwa muda wa muongo mmoja'". Ripoti hii inajiri wakati ambapo kumetukia uenezaji mkubwa wa habari na gazeti hilo kuhusu kufichuka kwa kashfa hii iliyo yashtua mashirika ya "misaada"; ambapo lilichapisha katika ukurasa wake wa mbele ripoti inayofichua kuwa shirika la Oxfam lilikuwa limemteua Roland Van Hauwermeiren kama mkurugenzi wa tawi lake la Haiti, ambaye hatimaye alikuwa katikati ya kashfa ya kuhusika na makahaba wakati wa shughuli za uokozi za shirika hilo kwa waathiriwa wa tetemeko la ardhi nchini Haiti, miaka miwili baada ya kutimuliwa kutoka kwa shirika jengine la misaada la Kiingereza kwa madai ya kuwatumia makahaba vile vile!

Soma zaidi...

Makongamano ya Kimataifa, Mipango ya Amani, Pasi na Kukomesha Wala Kupunguza Mashambulizi ya Mabomu ya Urusi!

Matukio ya umwagikaji damu yanayojiri Mashariki mwa Ghouta na Idlib; Mtandao wa Kutetea Haki za Kibinadamu wa Syria umesema kwamba raia wapatao 370 wameuwawa Mashariki mwa Ghouta tangu mwanzoni mwa mwaka huu, ukitaja kuwa miongoni mwa wafu ni watoto 63 na wanawake 72. Katika eneo la Idlib, hususan mji wa Sarakib, ambao ndio uliolengwa kwa dhoruba hii tangu mnamo 25 Disemba, Warusi na serikali ya kihalifu ya Syria zimemwaga chuki zake dhidi yake, ikitangazwa na baraza lake la mji kuwa eneo lililo kabiliwa na janga, ambapo idadi ya vifo mwezi Januari ilikuwa ni watu wapatao 30 na zaidi ya raia 60 kujeruhiwa. Hii ni ikiongezewa na kulengwa kwa mashule na mahospitali, ambazo idadi yake kubwa haziendeshi tena shughuli zake.

Soma zaidi...

Watoto wa Iraq … Uhalisia Unaoogofya na Mustakbali Unaotoa Bishara ya Miaka Mingi ya Kuzorota!

Hazina inayoshughulikia maswala ya watoto ya Umoja wa Mataifa (UNICEF) imesema katika ripoti iliyotolewa mnamo Ijumaa 19/1/2018 kuwa watoto 270 waliuwawa nchini Iraq mwaka jana kwa sababu ya vita vilivyo anzishwa na serikali ya Iraq dhidi ya ISIS. Vita hivi pia vilisababisha watoto 1.3 milioni kukosa makao miongoni mwa 2.6 milioni waliokosa makao kutokana na vita hivi vya miaka mitatu. Kulingana na taarifa hiyo, watoto milioni nne katika mikoa ya Nineveh na Anbar waliathirika na ghasia hizo na watoto wengi walilazimika kushiriki katika vita safu za mbele. Taarifa hiyo ilifichua kwamba umasikini na mizozo ilisababisha kusita kwa mchakato wa elimu kwa watoto milioni tatu kote nchini Iraq, baadhi yao wakikosa kabisa fursa ya kukaa ndani ya darasa katika maisha yao yote, huku zaidi ya robo ya watoto wa Iraq wakiishi ndani ya umasikini.

Soma zaidi...

Watoto wa Rohingya Wanadhalilishwa Mikononi mwa Mabudha! Je, Wanaye Mtetezi?

Shirika la misaada la Médecins Frontiéres, limeripoti kuwa zaidi ya nusu ya wasichana katika kambi ya wakimbizi wa Rohingya eneo la Cox's Bazar, Bangladesh ambao limewatibu baada ya kudhulimiwa kimapenzi na kubakwa nchini Myanmar wako chini ya umri wa miaka 18, na wengine wako chini ya miaka 10. Limeeleza kuwa mamia ya wasichana wa Rohingya wamepewa usaidizi wa kimatibabu na wa kisaikolojia katika kliniki yake mjini Kutupalong inayotibu wahanga wa dhulma za kijinsia lakini likasisitiza kuwa hao ni sehemu tu ya wale wanao amanika kudhulumiwa kimapenzi na kubakwa na majeshi katili ya kibudha tangu kutokea kwa kampeni ya mauaji ya halaiki dhidi ya Waislamu wa Rohingya mnamo Agosti

Soma zaidi...

Gharama Kubwa Inayolipwa na Raia Eneo la Deir al-Zour Na Watawala wa Waislamu katika Meza ya Majadiliano kwa Kuketi na Kukutana na Muuwaji

Ndege za kivita za Urusi, kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya kimaeneo kutoka Deir al-Zour, zimefanya mashambulizi ya msururu wa mabomu juu ya feri za mtoni zilizokuwa zimebeba maelfu ya raia wanaokimbia eneo la Deir al-Zour kuelekea maeneo mengine, yakisababisha zaidi ya vifo hamsini na maelfu kujeruhiwa, wengi wao wakiwa ni watoto na wanawake.

Soma zaidi...

Huku wakitelekezwa na Serikali Zisizo na Utu za Waislamu, Wanawake na Watoto wa Kiislamu Wakimbizi wa Rohingya Wanakabiliwa na Baa la Njaa, Maradhi na Vifo Nchini Bangladesh

Mnamo Jumapili 17 Septemba, shirika la msaada la ‘Save the Children’ lilionya kuwa wakimbizi wa Rohingya nchini Bangladesh huenda wakafariki kutokana na uhaba wa chakula, makao, na bidhaa msingi za usafi. Zaidi ya Waislamu wa Rohingya 410,000 wamekimbia Myanmar na kwenda Bangladesh tangu Agosti 25 kutokana na kampeni ya mauaji ya halaiki inayotekelezwa na jeshi la Burma. Kwa mujibu wa shirika la UNICEF, asilimia 80% ya wakimbizi hawa ni wanawake na watoto, 92,000 kati yao wako chini ya umri wa miaka 5, na takriban wanawake 52,000 ni waja wazito au wananyonyesha.

Soma zaidi...

Vifungu vya Tovuti

Viunganishi

Magharibi

Ardhi za Waislamu

Ardhi za Waislamu